Utawale mwilii wako – uanze kuishi

Utawale mwilii wako – uanze kuishi

The redemeer

JF-Expert Member
Joined
Jan 28, 2025
Posts
4,778
Reaction score
8,209
Watu wengi wamekuwa wakiishi maisha yao kwa kuongozwa na mwili pekee. Si kwa sababu wao ni wabaya au hawana akili, bali kwa sababu mfumo wa dunia umetufundisha kujiamini kama miili, si kama nafsi wala roho. Tangu tunapozaliwa, tunafundishwa kula ili kukua kimwili, kufikiria kuhusu nguo, mali, uzuri, na starehe za mwili.

Tunaelekezwa kusikiliza njaa, maumivu, hamu, na hisia za mwili kama ndiyo dira ya maisha. Lakini ukweli mchungu na wa ajabu ni huu: mtu anayeishi kwa makwa ya mwili pekee, bado haja anza kuishi .

Mwili ni mzuri. Ni hekalu. Ni chombo muhimu. Lakini mwili si wewe. Mwili si mfalme. Mwili ni mtumwa. Ukimpa nafasi ya kuamua kila kitu, ataangamiza kila kitu kilicho na maana ndani yako. Mwili hautaki kusubiri, hautaki maumivu, hautaki kukataliwa, hautaki subira. Mwili hutaka kila kitu sasa.

Utakula bila mpango, utalala bila kazi, utapenda bila kujitoa, utajichanganya bila mwelekeo. Mwili hukimbilia raha ya haraka haraka, na kuikimbia nuru ya kudumu. Mwili haujui kusudi – mwili hutafuta kutulizwa tu.

Ndiyo maana ukianza kutawala mwili wako, ndipo unapoanza kuamka. Unapoamua kuamka mapema licha ya uzito wa macho, unajifunza kuwa wewe si usingizi.

Unapoacha kula chakula cha tamaa na kuchagua lishe ya mwili wa nuru, unajifunza kuwa wewe si hamu ya ulimi. Unapoamua kukaa kimya na kutafakari badala ya kupiga kelele na kujihusisha na drama za dunia, unajua kuwa wewe si kelele – wewe ni ukimya. Huo ndiyo mwanzo wa kuishi.

Kujitawala ni kazi. Ni kama vita ya ndani. Mwili hupiga kelele. Huomba ulale, ule, uzinifu, uogope, ujitetee, upende ukipendwa tu. Lakini roho yako haijui haya mambo. Roho yako ni kimya lakini ina nguvu ya ajabu.

Roho haipigi kelele, lakini ikipewa nafasi – hutuliza dhoruba za tamaa. Ndipo unaanza kugundua kuwa wewe ni mfalme wa ndani, sio mtumwa wa mihemko ya mwili.

Na hii haimaanishi kuuchukia mwili. Hapana. Mwili ni zawadi. Lakini lazima uwe chini ya utawala wa roho. Mwili ukiwa mtiifu – unakuwa mtumishi mwema. Unakuwa na afya, nguvu, urefu wa maisha, mwonekano wa kung’aa.

Lakini ukiachiwa ujiendeshe – utajiletea magonjwa, uchovu, kuchanganyikiwa, na mwisho wake, mauti ya kiroho. Wengi wanaonekana wako hai, lakini ni waendao huku roho zao zikiwa zimelala kabisa. Si kwa sababu hawajui, bali kwa sababu walimpa mwili usukani. Mwili ukikalia roho, utaua kila kitu cha thamani: maono, imani, heshima, uzito wa kiroho, na nguvu ya kweli ya ndani.

Ukitawala mwili wako, unamkomboa. Mwili huhitaji nidhamu ili uangaze. Anza kwa utulivu. Sikiliza mwili wako lakini usiufuate moja kwa moja. Jifunze kusema “hapana” hata kama una hamu. Jifunze kula kwa makusudi, si kwa kujaza tumbo tu.

Jifunze kusali hata kama mwili hauna hamu. Jifunze kufanya kazi hata kama unahisi kuchoka. Kadri unavyotawala mwili, ndivyo roho yako inavyong’aa. Ndipo unapoanza KUISHI.

Maisha si kula tu na kupumua. Maisha ni kuamka ndani. Maisha ni kuiona nuru yako na kuitembea. Maisha ni kutumikia kusudi lililokuwepo kabla hujazaliwa.

Maisha si kusubiria likizo au pesa tu – maisha ni kufungua macho ya ndani na kuona kuwa wewe si mwili huu unaouona, wewe ni roho iliyovaa mwili huu kwa muda mfupi tu. Na siku uamuzi wa kweli unapofanyika moyoni, pale unaposema “Tosha! Sitaongozwa na mwili tena!” – hapo ndipo safari halisi huanza.

Kumbuka, mwili bila roho ni mzoga. Na roho bila mwili haiwezi kutenda duniani. Kwa hiyo viunganishe – lakini kwa mpangilio. Roho mbele, nafsi imetakaswa, mwili chini ya amri. Ukiona kuna vita ndani yako – tambua hiyo ni ishara ya mabadiliko.

Hakuna mabadiliko bila mapambano. Lakini ukishinda – mwili wako utakushukuru, nafsi yako itatulia, na roho yako itang’aa kama taa ya mbinguni.

Usiogope kujitenga na mazoea ya mwili. Usiogope kusema hapana kwa yale ambayo yamekuwa yakikunyonga kwa jina la starehe. Usiogope maumivu ya nidhamu – ogopa maumivu ya maisha ya kiholela. Maana mwisho wa yote, si kuishi tu ndicho cha muhimu – bali KUISHI KWA NURU, kwa KUSUDI, na kwa NGUVU ya ROHO.

Na hapo ndipo safari ya kweli ya mwanadamu huanza. Safari ya ndani, safari ya kutawala mwili kwa utulivu wa roho. Safari ya kutoka kwa wanyama kwenda kwa miungu. Safari ya kuamka.
Ukitawala mwili wako – unaanza kuishi.
 
Ukitaka matakataka yote yakupite kushoto sijui uchawi, kulogwa, magonjwa laana matatizo nk ishi maisha ya kiroho.
Ipo tofauti ya maisha ya kiroho na maisha ya kidini.
Kuishi kiroho ni kuishi kutokea ndani yako na sio kuishi kutokea nje yako.
 
. MWILI ushiba chakula
. NAFSI ushiba amani
. ROHO ushiba upendo
. AKILI ushiba maarifa
Jitahidi kila vyote vishibe ili uishi maisha halisi na ya amani ya ndani na ufanyike Nuru halisi uwaangaze wengine waliogizani
 
Elimu sio tatizo , elimu zipo nyingi sana ,wewe ndio unadai unavyote hivyo hii haihitaji elimu ni wewe kututhibitishia hapa hiyo roho yako ipoje.
Mwili wa mwanadamu umejengwa kwa vitu vitatu vilivyounganishwa na kamba nyepesi rangi ya dhahabu.
Navyo ni mwili,Roho na nafsi
.MWILI umetokana na udongo ukiwa unarudi udongo kuoza
.NAFSI ni photocopy yako wewe yaani mwili wa ndani pana mwili wa ndani na mwili wa nje
.ROHO ni pumzi ya uhai itokayo kwa Muumba
 
Mwili wa mwanadamu umejengwa kwa vitu vitatu vilivyounganishwa na kamba nyepesi rangi ya dhahabu.
Navyo ni mwili,Roho na nafsi
.MWILI umetokana na udongo ukiwa unarudi udongo kuoza
.NAFSI ni photocopy yako wewe yaani mwili wa ndani pana mwili wa ndani na mwili wa nje
.ROHO ni pumzi ya uhai itokayo kwa Muumba
Hizi ni theories je umeshawahi Thibitisha hili?
 
Pia cha kuongezea apo ili uutawale mwili lazima utoke kwenye low self material Ambal ni ukanda unao tawaliwa na sex ,food and power .
Low self material uwa wanatabia ya kuwaza vitu vidogo vidigo .anawaza atakula nini na ajawai kulala njaa ,anawaza nguo za kuvaa ndio low self material walivyo ivyo .
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom