Utata wa kifo cha Mwalimu Julius K. Nyerere: Siri zaidi zafichuka

Sioni sababu ya malumbano nani aliongea mara ya mwisho na Mwal. Ningeona kuna jambo la maana lolote kama hawa watu wangelikuwa wanasema waliongea na Mwalimu Nyerere aliongea nao nini kwa nyakati zao tofauti.

Kinachojalisha na kinachoweza kuwa ni cha maana ni nini alisema na siyo huu upumbavu wa kushindania mimi niliongea naye wa mwisho na si yule. Ujinga mtupu.

Wasaidizi wa marehemu Nyerere wanajua movie yote ilivyokuwa hapo wameamua kupingana na Msekwa ili kuwachanganya watu waone kuwa ni porojo waache kufuatilia lakini mama Maria Nyerere anayo Siri moyoni akibembelezwa vizuri ataitoa au pengine anaogopa asije yakamkuta ya kawawa ambaye alijidai kuwa na Siri za Nyerere lakini akafariki pasipo kuzitoa Hizo Siri .
 
Nyerere aliuawa baada ya kuonekana ni kero wakati akilalamikia uwekezaji usio na Tija , wizi wa pesa za umma , EPA nk , ilikuwa akirejea toka London aje kuwaelezea Watanzania jinsi asivyolizishwa na hali harisi ilivyokuwa kwenye Rasilimali za Nchi ndipo wasaidizi wakamtonya Mkapa kuwa Nyerere anakuja kuharibu hali ya hewa na ingeathili mambo mengi yake binafsi , ndipo anafunga Safari mwenyewe kwenda London lakini kabla ya kwenda huko alipitia sehemu Fulani alipofika London aliomba kuongea na Nyerere pasipo kuwepo na msaidi yeyote yaani wote waliondolewa kabsa akabaki yeye na Nyerere tu , baada ya kuondoka ndipo hali ya Nyerere ikabadilika ghafra na kuwa mbaya na hatimae mauti Msekwa anajua Movie yote ilivyo lakini kaamua kukwepa lawama lakini marehemu kawawa aliwahi kudokeza kidogo hata mama Maria Nyerere anajua kila kitu sema kaamua kuvumilia milele.

Mkuu umeongea mambo mazito sana kumuhusisha mutu yeyote na kifo cha Nyerere si neno dogo

Kwa upole kabisa naomba nijibu swali hili ukiombwa ushahidi wa hayo uliuoyasema unaweza kuutoa?
Kama taifa tutakuwa tumepata pa kuanzia.
 
Kwa sasa hoja ya kapoteza fahamu lini?nani Wa mwisho kuzungumza nae haina maana.
Acha Magufuli atumbue majipu ili nchi isonge mbele
 
Mkuu umeongea mambo mazito sana kumuhusisha mutu yeyote na kifo cha Nyerere si neno dogo

Kwa upole kabisa naomba nijibu swali hili ukiombwa ushahidi wa hayo uliuoyasema unaweza kuutoa?
Kama taifa tutakuwa tumepata pa kuanzia.

Kitu kinaitwa Ushahidi Tanzania hakijawahi kufanya kazi Kama unakumbuka aliyekuwa Mbunge wa Musoma mjini Vicent Nyerere aliwahi kusema kwenye vyombo vya habari kuwa Nyerere hakufariki Kwa mapenzi ya mungu Bali aliuwa Kama unataka ushahidi mtafute vicent Nyerere atakupa ushahidi .
 
Kitu kinaitwa Ushahidi Tanzania hakijawahi kufanya kazi Kama unakumbuka aliyekuwa Mbunge wa Musoma mjini Vicent Nyerere aliwahi kusema kwenye vyombo vya habari kuwa Nyerere hakufariki Kwa mapenzi ya mungu Bali aliuwa Kama unataka ushahidi mtafute vicent Nyerere atakupa ushahidi .

Mbona hukumunukuu vicenti nyerere mwanzoni
Naona kama unakwepa vile lakini nafikiri kama taifa tumepata pa kuanzia ni vizuri ujiandae kuwa tayari kutoa ushahidi.na kusimamia kauli yako pasipo kuikimbia.
 
Mkuu umeongea mambo mazito sana kumuhusisha mutu yeyote na kifo cha Nyerere si neno dogo

Kwa upole kabisa naomba nijibu swali hili ukiombwa ushahidi wa hayo uliuoyasema unaweza kuutoa?
Kama taifa tutakuwa tumepata pa kuanzia.

mkuu kwani hilo lina usiri gani mbona kishazungumzwa sana??
 
Hapa ni mbona rahisi?
Magufuli amtake Mkapa ajisafishe dhidi ya kashfa ya kumuua Nyerere iliyotolewa hadharani na Vincent Nyerere.
Akishindwa sisi tunaendelea kumwamini Vincent kuwa Mkapa alihusika
 
Back
Top Bottom