Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 359,869
- 828,403
Utangulizi wa Mengineyo Kwanza. Likizo imeisha, tetesi zimekoma, tarahuki zimeisha. Hakuna breaking news! Kilichopangwa kiwe tukio kubwa la kufunika mitandao na media zote limefifia kwa kishindo cha ajabu. Hizi si dalili njema! Wakati ni ukuta, usishindane nao!
Mnenguaji mahiri hujua ni wakati gani wa kuondoka ukingoni, kwani kushangiliwa sana kunapokoma, kifuatacho ni kuzomewa.
Tuendelee na Mada Yetu Sasa. Ulimwengu wa roho ni timilifu. Haupangiwi, haushurutishwi, haupokei maagizo ya kimwili, haudanganyi, na haubatilishwi. Badala yake, ulimwengu huu hufanya kinyume na hayo yote kwa kuwa huona yajayo kabla ya macho ya mwili kuona.
Katika medani za siasa za vyama vingi, ni kawaida watu kuhama chama kwa sababu mbalimbali, njema au ovu. Wahamao kwa utashi wa kiroho na kwa nia njema huwa hawahukumiwi na nafsi zao wala hawaweweseki kila fikra za walikotoka zikiwajia. Lakini, wahamao kwa silika za kimwili huku utashi wa kiroho haujatoa kibali hujikuta wakitaabika sana.
Hali hii hutokea pia kwenye mahusiano na hukera sana, ikizidi kuwa ngumu kuzuilika kwa namna yoyote ile kwa kuwa huendeshwa na utashi wa kiroho!
Upendo Peneza na Mchungaji Peter Msigwa, waliokuwa wanachama na viongozi wa CHADEMA, walihama kwa sababu zozote zile zilizowafanya waondoke CHADEMA na kujiunga na CCM. Walilazimisha kinyume na utashi wa kiroho, wakitegemea silika za kimwili ziwe na nguvu zaidi ya utashi wa kiroho – lakini ikashindikana kabisa. Ndio maana mawazo ya CHADEMA hayawatoki kabisa.
Silika hizo za kujiona bado wako CHADEMA kwenye majukwaa ya CCM ni utashi wa kiroho usiopangiwa wala kushurutishwa! Wako kwenye mtanziko mkubwa sana; nyuma ya kelele za majukwaani wanapopewa vipaza sauti, kuna kihoro cha usaliti kinachowandama.
Kwa upande mwingine, hili ni suala la Msigwa na Peneza, lakini vipi kuhusu hiki chombo cha habari? Unaweza kusema ni 'typing error,' lakini uhalisia ni kwamba mafunuo ya kiroho yana nguvu kubwa kuliko silika za kimwili.
Thread: "Ulimwengu wa Roho ni Timilifu"
Tundu Lissu keshatia nia.
Good morning Tanganyika ❤
Mnenguaji mahiri hujua ni wakati gani wa kuondoka ukingoni, kwani kushangiliwa sana kunapokoma, kifuatacho ni kuzomewa.
Tuendelee na Mada Yetu Sasa. Ulimwengu wa roho ni timilifu. Haupangiwi, haushurutishwi, haupokei maagizo ya kimwili, haudanganyi, na haubatilishwi. Badala yake, ulimwengu huu hufanya kinyume na hayo yote kwa kuwa huona yajayo kabla ya macho ya mwili kuona.
Katika medani za siasa za vyama vingi, ni kawaida watu kuhama chama kwa sababu mbalimbali, njema au ovu. Wahamao kwa utashi wa kiroho na kwa nia njema huwa hawahukumiwi na nafsi zao wala hawaweweseki kila fikra za walikotoka zikiwajia. Lakini, wahamao kwa silika za kimwili huku utashi wa kiroho haujatoa kibali hujikuta wakitaabika sana.
Hali hii hutokea pia kwenye mahusiano na hukera sana, ikizidi kuwa ngumu kuzuilika kwa namna yoyote ile kwa kuwa huendeshwa na utashi wa kiroho!
Upendo Peneza na Mchungaji Peter Msigwa, waliokuwa wanachama na viongozi wa CHADEMA, walihama kwa sababu zozote zile zilizowafanya waondoke CHADEMA na kujiunga na CCM. Walilazimisha kinyume na utashi wa kiroho, wakitegemea silika za kimwili ziwe na nguvu zaidi ya utashi wa kiroho – lakini ikashindikana kabisa. Ndio maana mawazo ya CHADEMA hayawatoki kabisa.
Silika hizo za kujiona bado wako CHADEMA kwenye majukwaa ya CCM ni utashi wa kiroho usiopangiwa wala kushurutishwa! Wako kwenye mtanziko mkubwa sana; nyuma ya kelele za majukwaani wanapopewa vipaza sauti, kuna kihoro cha usaliti kinachowandama.
Kwa upande mwingine, hili ni suala la Msigwa na Peneza, lakini vipi kuhusu hiki chombo cha habari? Unaweza kusema ni 'typing error,' lakini uhalisia ni kwamba mafunuo ya kiroho yana nguvu kubwa kuliko silika za kimwili.
Thread: "Ulimwengu wa Roho ni Timilifu"
Tundu Lissu keshatia nia.
Good morning Tanganyika ❤




