Utaratibu wa uhamisho kwa watumishi wa umma

Black Walker

Senior Member
Oct 8, 2018
107
238
Wakuu poleni na majukumu, hoja yangu ni moja tu! Kuna hii issue ya watumishi wa umma kutakiwa kufungua ankaunt maalumu kwa ajili ya taarifa zao za kiutumishi lakini pia likiwemo suala la uhamisho kufanyika mtandaoni.

Yaani nasikia hakutakuwa na ule utaratibu wa awali wa kuandika barua. Wasiwasi wangu ni kwamba naona kama hii njia haitafanyika kwa ufanisi na huenda inalenga kuondoa kasi ya watumishi kuhama. Kwa upande wa Tamisemi naona kabisa uwajibikaji wao utapungua.

Kwa mfano kama tu kwenye ule mfumo wa kawaida mtu anaandika barua ya kuomba nafasi kupitia kwa mkurugenzi wake barua inakaliwa ofisini zaidi ya miezi mitatu bila kupitishwa sasa kwa huu mfumo si ndo kabisa watu wataumia sana na wale ambao tuko mbali na wenza wetu tutasahau kabisa.

Mwisho kabisa naomba kuelimishwa kwa namna utakavyoratibiwa maana ni watumishi wengi hawajui namna unavyofanya kazi.
 
Kuna jamaa jana usiku tukiwa kazini tunapiga story za maisha akaniambia "...angalia matajiri wote hata hapa nchini au duniani nani anafanya kazi ya mtu? Hakuna, wote wanafanya kazi/miradi yao na wanaajiri watu ili wawanyonye"

Ndio kusema kuajiriwa ni utumwa mkubwa sana. Tusiridhike na ajira hizi bali tuzitumie kama stepping stone tuweze kujiajiri na kuwa na mishe zetu wenyewe.
 
Mwisho kuna barua mtapata we kacheki video
Unajua huu utaratibu kwa watumishi wa kada za chini au wasio na connection itakuwa ngumu sana kuhama kwa wakati mwafaka, hii ni tofauti na maboss wenyewe anahama leo kesho pia utamu wake unamfuata lakini akina sisi kila siku ni kuumizwa tu. Hivi navyokwambia mke wangu aliandika barua hata kabla ya kuanzishwa kwa mfumo huu lakini Mkurugenzi wake alikalia barua tangu mwezi July bila kupitisha hadi kakutwa na hii kitu.
 
mfumo ni mzuri maana wakuu wa vituom ukitaka kuanza kugombana nao basi we omba uhamisho boss anakuchukia sana
mfumo huu utasaidia sana
 
Mbona sijasikia sehemu ya mwisho kama maombi yakikubaliwa unapata barua
Sehemu hiyo IPO,changamoto kubwa ni kuwa inawachukua mda mrefu ofisini ya raisi utumishi kukamilisha vibali,tulitegemea kwa utaratib wa mfumo,hata wiki itoshe kukamilika kwa mchakato wa uhamisho kupitia mfumo ila sasa inachukua mda,na sidhani kama Kuna mtu ashapata kibali kupitia mfumo huu mpya
Utumishi waache kucheleweshea watu vibali vya uhamisho,maana kama mfumo ukishakubali kuwa nafasi ipo, vikwazo vya ikama,sijui taratibu ,kanuni na Sheria viziwe visingizio na kuwabania watumishi kuhama,kwani ni hakika
Usharudi kwa utumishi,wajitahidi kukamilisha vibali ndani ya mda mfupi,angalau ndani ya siku 14 tokea status inaposoma kwao,vibali viwe vimetoka,waache urasimu
 
Back
Top Bottom