fiksiman
JF-Expert Member
- May 17, 2008
- 402
- 104
Makampuni ni miongoni mwa biashara inayotengeneza faida kubwa na haramu kupindukia huku zikihusisha wizi wa moja kwa moja kutokana na huduma zinazotolewa kwa lazima au bila wateja kujua kuwa wanalipia. Pia promosheni mbalimbali zimekuwa kichocheo kikubwa cha kuwaibia wateja hasa wale wapenda njia ya mkato kuelekea utajiri. Sitaki kuzitaja huduma hizo kwani si agenda iliyonipelekea kuweka thread hii.
Hivi karibuni kampuni ya simu za mkononi Zain imeanzisha huduma nyingine ya kitapeli kwa mtazamo wangu ili kuendeleza libeneke la wizi wa kimachomacho kwa wateja ambao wengi ni ignorant na namna makato yanavyofanywa. Huduma hiyo ambayo imepachikwa jina la Zap ambayo humuwezesha mteja kufanya manunuzi kupitia akaunti yake aliyoweka kwenye mtandao huo. Huduma kama kununua Luku, kujua balance yako kutoka akaunti yako ya benki na pamoja na kuhamisha pesa kutoka kwenye benki kwenda Zap ni mambo ambayo niliyaona mazuri na nikavaa mkenge wa kujiunga.
Utapeli unaanzia hapa: Kwanza kwa kila huduma utakayotumia utakatwa pesa si chini ya 150 na kuendelea kulingana na aina ya huduma. Pia lazima simu yako iwe na credit iliuweze kutumia huduma hiyo, Huduma ya kuhamisha salio kutoka kwenye akaunti yako ya benk haifanyi kazi japo watakuta kila unapotumia. Kibaya zaidi walidai huduma zote zitafanywa na mawakala wao ambao hadi sasa hawajaanza kufanya kazi hivyo utalazimika kuzngumka mji mzima kutafuta wakala wa kuwekea pesa au kuchukua. Yote tisa kubwa ni kitendo cha kuwakata wateja hata kama hakuna huduma kwangu nahisi ni utapeli wa hali ya juu.
Kama unataarifa zaidi tafadhali nijlishe ili watanzania wengine wasiuvae mkenge wa kutapeliwa kama wanavyofanya Zain na bila shaka kampuni zingine ziko njiani kuanzisha huduma hii isyo na maana.
Hivi karibuni kampuni ya simu za mkononi Zain imeanzisha huduma nyingine ya kitapeli kwa mtazamo wangu ili kuendeleza libeneke la wizi wa kimachomacho kwa wateja ambao wengi ni ignorant na namna makato yanavyofanywa. Huduma hiyo ambayo imepachikwa jina la Zap ambayo humuwezesha mteja kufanya manunuzi kupitia akaunti yake aliyoweka kwenye mtandao huo. Huduma kama kununua Luku, kujua balance yako kutoka akaunti yako ya benki na pamoja na kuhamisha pesa kutoka kwenye benki kwenda Zap ni mambo ambayo niliyaona mazuri na nikavaa mkenge wa kujiunga.
Utapeli unaanzia hapa: Kwanza kwa kila huduma utakayotumia utakatwa pesa si chini ya 150 na kuendelea kulingana na aina ya huduma. Pia lazima simu yako iwe na credit iliuweze kutumia huduma hiyo, Huduma ya kuhamisha salio kutoka kwenye akaunti yako ya benk haifanyi kazi japo watakuta kila unapotumia. Kibaya zaidi walidai huduma zote zitafanywa na mawakala wao ambao hadi sasa hawajaanza kufanya kazi hivyo utalazimika kuzngumka mji mzima kutafuta wakala wa kuwekea pesa au kuchukua. Yote tisa kubwa ni kitendo cha kuwakata wateja hata kama hakuna huduma kwangu nahisi ni utapeli wa hali ya juu.
Kama unataarifa zaidi tafadhali nijlishe ili watanzania wengine wasiuvae mkenge wa kutapeliwa kama wanavyofanya Zain na bila shaka kampuni zingine ziko njiani kuanzisha huduma hii isyo na maana.