Utamshauri nini kijana huyu?

Utamshauri nini kijana huyu?

DASA

JF-Expert Member
Joined
Jan 6, 2011
Posts
1,031
Reaction score
302
Kijana yangu mmoja ambaye sasa ni mwalimu wa chuo fulani maarufu kaja akaniambia kaka haya maisha sio kabisa, labda amerogwa. Akasema alikuwa anachat whatsapp na marafiki zake aliomaliza nao degree miaka 8 iliyopita, mmoja wa hao marafiki alikuwa anawajulisha wenzake kuwa ameomba kazi mahali na anategemea kufanya interview siku kadhaa baadae kwahiyo alikuwa anaomba baraka zao, sasa katika maongezi ikaonekana mshahara anaoenda kudai huko si chini ya milioni 8, huko alipo kwa sasa anapokea milioni 5, wengine wakasema hiyo hela ya kawaida sana.

Sasa yeye tangu amalize degree alibahatika kubaki kama tutorial assistant(TA) kwenye chuo hicho baada ya kuonekana amefaulu kwa kiwango cha first class, tangu abaki hapo amekuwa akisota na kusoma kila siku ili apande ngazi mbali mbali ili aufikie uprofessor. Kwenye udadisi wake amegundua Full Professor mshahara wake wa juu kabisa kwa sasa hauzidi millioni 5. Na ili yeye afike ngazi hiyo inabidi asote kwelikweli mpaka nywele zibadilike rangi ndio apate hiyo hela ambayo wenzake aliomaliza nao wanaofanya kazi sehemu zingine wanapata zaidi ya kiasi hicho kwa sasa pamoja na allowance zingine za kutosha.

Huko nyuma alishawishika kwamba ukiwa mwalimu wa chuo kuna mambo mengi utafanya au kushirikishwa kama projects mbalimbali au consultancy mbalimbali kitu ambacho anasema sio vile ilivyo kama vile watu wengi wanavyofikiria. Hata wenzake ambao wamemtangulia hawana maendeleo ya maana, ni kama watu waliokata tamaa.

Zamani kuna wazee tulikuwa tunawaona ambao ni walimu wa vyuo mambo yao yalikuwa ni mazuri sana. Kwahiyo yeye alikuwa na ndoto za kufanya vizuri sana darasani ili awe kama wao, lakini anaona imekuwa kinyume chake.

Sasa anaona kuwa mwalimu wa chuo atasota sana kuileta familia yake maendeleo. Mfano wenzake wamepeleka watoto wao kwenye shule nzuri za private wanapata elimu nzuri yeye uwezo huo hana kabisa hata ndoto hazipo. Sasa yeye bahati yake miaka hiyo aliweza kuungaunga akafanya vizuri, watoto wake atawasaidia vipi kufika huko kwa kipato anachopata!.

Sasa ni kwamba kijana ana bahati mbaya au ndio maisha ya walimu wa vyuo yalivyo miaka hii?
 
Duuuuh!
Na hapo ni mwalimu wa chuo! Pata picha Angekuwa wa msingi au sekondar
 
Ukisha kua mwalimu unakua mwalimu tu haijalishi unafundisha wapi,chuo au sekondari. Maisha ya walimu ni yale yale.

Ukiwa mwalimu na ukategemea mshahara tu utakufa masikini,tutorial assistants ni sawa tu na mwalumu wa sekondari,tofauti yao kimshahara ni ndogo sana.

Watu hawana malengo,huwa hawajui hasa hitaji lao ni lipi,hufanya kwa kua fulani alifanya au kumfurahisha fulani.

Mwambie atafute kazi nyingine kama haridhiki na aliyonayo,kwa ufaulu wake na kama yuko smart atapata kazi nyingine yenye mshahara mzuri au aendelee na kazi aliyonayo sasa ila aanzishe mradi wa kibiashara wa kumuingizia kipato cha ziada.
 
Ila wabongo kwa kujifanya babu kubwa hatujambo,yani mtu anadiriki kusema salary ya 8M ni pesa ya kawaida kwa maisha haya?wkt wengine wanatafuta hata mshahara wa laki mbili.
 
Duuuuh kama alimaliza chuo kwann wasimuunganishie na yy job sehem waliyopo wao kama wanaona rafk yao analipwa kiduchu
 
Ila wabongo kwa kujifanya babu kubwa hatujambo,yani mtu anadiriki kusema salary ya 8M ni pesa ya kawaida kwa maisha haya?wkt wengine wanatafuta hata mshahara wa laki mbili.

Mshahara wa kawaida kwa wafanyakazi wa level Fulani! Sio wa kawaida kwa kila level!
 
bakishuu
Ukweli ukitaka kuishi kwa amani na kujiona mshindi kila siku, angalia walio nyuma yako kwa kipato tazama analipwa m tano kasoro lkn anatamani m nane kuna wengine kwa mwaka kipato chao hakifiki milioni yaani inakera sana
 
Last edited by a moderator:
Kwa hizo mbwembwe tamaa ya kupata maisha kwa haraka ndo vitu vinavyotutesa vijana. Nimelelewa na mwalimu wa primary sijawah kulala njaa na alikuwa akikimbiza mbaya saiz ya maisha ya kati tu na kusoma vizur bila shida maisha ni mipango tu.
 
wazazi wetu walikuwa walimu wametusomesha na hatukuwahi kulala bila kula, milo 3 nyama/dagaa/samaki/majani ya maboga/matembele tulikula na leo hii tunasonga mbele

Walimu HOyeeee
 
mweeeeee!!!!! mmmh!!!!!!!! bora kujiajiri, unachokiingiza hufananishi nacha jirani, wewe unacheza na mtaji wako over.
 
Mpe pole yake, ninachoweza sema huyo anaweza kuwa mvivu wa kujituma. Consultation hazikufati bali unazitafuta na zinawalipa wanaojituma. Ni kweli mshahara anaweza uona mdogo huo kwa sasa ila anamuda mrefu/kutosha kuutumia ili kuongeza kipato zaidi kwa kutumia elimu yake.

Natambua pia wasongo wengi class huwa hawana muda kujichanganya na jamii kujua opportunities wanaamini kusoma tuu ndo anapata hela. Ukweli ni kuwa kujituma kwako SMART ndo mtaji wa hela ndefu.

Nilikuwa inspired na mwalimu wangu wa shule ya msingi huko kijijini kwangu, kwa macho yangu nilimuona anajituma na kujenga nyumba nzuri miongoni mwao zilizokuwepo kijijini hapo na alikuwa na maisha fresh.
 
Mada kama hizi ndio maana sisi wengine huwa tunashindwa kuchangia unalipwa milioni5 kwa mwezi halafu unasema unashindwa kumpeleka mwanao hata shule ya private? Mwenyewe unaweka heshima bar halafu unasingizia mshahara mdogo aaarrrrgh
 
Duuuuh kama alimaliza chuo kwann wasimuunganishie na yy job sehem waliyopo wao kama wanaona rafk yao analipwa kiduchu

Unajua siku zote akiwa na hao marafiki wanaongea habari za kazi lakini hawaongei vipato vyao, saa ndio amejua kuwa hapati kitu kabisa. Na hapa tambua wamesoma pamoja, degree hiyo hiyo, yeye ameongeza ya pili na yupo njiani kupata ya tatu. Shule ilivyo ngumu na anachotegemea anatamani kuacha.
 
wa ukae
M5 sio yeye, yeye hata nusu ya hiyo hafiki, na amefanya kazi miaka 8. M5 ni mshahara wa huyo rafiki anaopata sasa.
 
Last edited by a moderator:
Hawa ndiyo wakiwa viongozi huwa ni mafisadi..huo ndiyo ukweli.
 
Back
Top Bottom