Yona F. Maro
R I P
- Nov 2, 2006
- 4,202
- 218
UTAMADUNI WA KUSOMA/KUJISOMEA
Siku chache zilizopita nilikuwa na kasafari ka kwenda mkoani morogoro kwenye basi nililopanda mimi mwenyewe ndio nilikuwa na gazeti la kusoma nakumbuka nilikuwa nasoma gazeti la mwanahalisi , kwenye basi hakukuwa na mtu aliyeshika kitabu cha kusoma wala gazeti wala jarida lolote sembuse yule ambaye anasikiliza radio za nyumbani kusikiliza yanayojiri .
Nyakazi za asubuhi zile wakati wa mchaka mchaka wa makazini na mashuleni ingia kwenye daladala uone wanafunzi ukiona ameshika kitu cha kusoma basi ujue ana mtihani baadaye ana kariri cha kwenda kujibu kwenye mtihani huo kama hakuna mtihani utafikiri hata sio mwanafunzi hata shuleni anachelewa kwa dakika chache .
Ukipita vyuoni napo ndio utashangaa zaidi ukienda kwenye internet café angalia history ya search ujue wanafunzi walikuwa wana search nini au kuangalia aina ya tovuti walizokuwa wanatembelea utashangaa na kustaajabu mfano wa UDSM samahani kwa sasa hakuna huduma ya internet café kwa miezi 2 sasa ila ni asilimia chini ya 10 ya wanafunzi wanaotembelea tovuti hiyo kwa siku kwa ajili ya kazi za kila siku hapo vyuoni .
Ukitembelea stationary zao kuangalia kwa mfano kinachoandikwa utashangaa mfano watu 20 wameandika jibu moja kwenye swali waliloulizwa si inaonekana kwenye print out pale tofauti ni majina ya wanafunzi tu ingawa hii zaidi inatokea kwenye taarifa za field
Hii ni tofauti sana na Nairobi au mombasa ambapo huwa naenda mara kwa mara kule watu wanapenda kusoma kuanzia wanafunzi mpaka wafanyakazi pamoja wadau wengine wa masuala ya nchi yao .
Hata unapoingia kwa mfano kwenye forum za nchi jirani utaona na kuamini watu wengi wanapenda kusoma na kuandika tofauti ya nyumbani kwetu kwa mbali kidogo nimeona hili kwa sababu nimetunga riwaya kadhaa zimesomwa sana na watu wa huko mpaka sasa hivi naendelea kuandaa fupi fupi .
Naona zifanyike jitihada za dhati kabisa kuamsha utamaduni wa kusoma kwa watanzania wote hii ni pamoja na wadau wa kuandika na utunzi kukaa pamoja kufanya utafiti na kujua kitu hichi kifanywaje ili hali iwe nzuri .
Mfano kwa mimi nimegundua wengi wanapenda vitu vifupi fupi ila ukimwandikia mwanamke wa kikuyu kitu kifupi ataomba uendelezee kuandika mpaka umalizie yote uliyotaka kusema .
Siku chache zilizopita nilikuwa na kasafari ka kwenda mkoani morogoro kwenye basi nililopanda mimi mwenyewe ndio nilikuwa na gazeti la kusoma nakumbuka nilikuwa nasoma gazeti la mwanahalisi , kwenye basi hakukuwa na mtu aliyeshika kitabu cha kusoma wala gazeti wala jarida lolote sembuse yule ambaye anasikiliza radio za nyumbani kusikiliza yanayojiri .
Nyakazi za asubuhi zile wakati wa mchaka mchaka wa makazini na mashuleni ingia kwenye daladala uone wanafunzi ukiona ameshika kitu cha kusoma basi ujue ana mtihani baadaye ana kariri cha kwenda kujibu kwenye mtihani huo kama hakuna mtihani utafikiri hata sio mwanafunzi hata shuleni anachelewa kwa dakika chache .
Ukipita vyuoni napo ndio utashangaa zaidi ukienda kwenye internet café angalia history ya search ujue wanafunzi walikuwa wana search nini au kuangalia aina ya tovuti walizokuwa wanatembelea utashangaa na kustaajabu mfano wa UDSM samahani kwa sasa hakuna huduma ya internet café kwa miezi 2 sasa ila ni asilimia chini ya 10 ya wanafunzi wanaotembelea tovuti hiyo kwa siku kwa ajili ya kazi za kila siku hapo vyuoni .
Ukitembelea stationary zao kuangalia kwa mfano kinachoandikwa utashangaa mfano watu 20 wameandika jibu moja kwenye swali waliloulizwa si inaonekana kwenye print out pale tofauti ni majina ya wanafunzi tu ingawa hii zaidi inatokea kwenye taarifa za field
Hii ni tofauti sana na Nairobi au mombasa ambapo huwa naenda mara kwa mara kule watu wanapenda kusoma kuanzia wanafunzi mpaka wafanyakazi pamoja wadau wengine wa masuala ya nchi yao .
Hata unapoingia kwa mfano kwenye forum za nchi jirani utaona na kuamini watu wengi wanapenda kusoma na kuandika tofauti ya nyumbani kwetu kwa mbali kidogo nimeona hili kwa sababu nimetunga riwaya kadhaa zimesomwa sana na watu wa huko mpaka sasa hivi naendelea kuandaa fupi fupi .
Naona zifanyike jitihada za dhati kabisa kuamsha utamaduni wa kusoma kwa watanzania wote hii ni pamoja na wadau wa kuandika na utunzi kukaa pamoja kufanya utafiti na kujua kitu hichi kifanywaje ili hali iwe nzuri .
Mfano kwa mimi nimegundua wengi wanapenda vitu vifupi fupi ila ukimwandikia mwanamke wa kikuyu kitu kifupi ataomba uendelezee kuandika mpaka umalizie yote uliyotaka kusema .