Ojuolegbha
JF-Expert Member
- Sep 6, 2020
- 741
- 479
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema utamaduni wa kuiombea nchi na Viongozi ni wa kuendelezwa na kudumishwa hakuna jambo jema zaidi ya kumuomba Mwenyezi Mungu atuepushe na mabalaa mbalimbali ikiwemo ya vita, mabadiliko ya tabia ya nchi, mabadiliko ya mazingira akitolea mfano ukame na mafuriko sehemu mbalimbali.
Rais Dkt. Mwinyi amesema hayo katika Dua Maalum ya kumuombea iliyoandaliwa na Wazee wa Jimbo la Makunduchi iliyofanyika Msikiti wa Mtegani Makunduchi Wilaya ya Kusini Mkoa wa Kusini Unguja tarehe: 16 Desemba, 2023.
Aidha Rais Dk. Mwinyi ameeleza kuwa ni muhimu Kumuomba Mwenyezi Mungu atudumishe katika amani na utulivu pamoja na mshikamano, umoja na upendo kwa wananchi wote.
Rais Dkt. Mwinyi amesema hayo katika Dua Maalum ya kumuombea iliyoandaliwa na Wazee wa Jimbo la Makunduchi iliyofanyika Msikiti wa Mtegani Makunduchi Wilaya ya Kusini Mkoa wa Kusini Unguja tarehe: 16 Desemba, 2023.
Aidha Rais Dk. Mwinyi ameeleza kuwa ni muhimu Kumuomba Mwenyezi Mungu atudumishe katika amani na utulivu pamoja na mshikamano, umoja na upendo kwa wananchi wote.