Utajiri wa kishirikina/kichawi

Utajiri wa kishirikina/kichawi

Pastor Silla

Senior Member
Joined
Sep 22, 2020
Posts
162
Reaction score
166
Nyakati za Sasa dunia pamoja na nchi yetu ya Tanzania imekumbwa na roho chafu ya kutafuta au kupenda mali au utajiri wa kichawi na kishirikina.

Watu waliowengi wapo tayari kuua au kumiliki majini na kutia kafara mbalimbali za damu kwa Shetani ilimradi wapate pesa ,mali na utajiri.

Wapo ambao wanashirikina tendo na Mama zao wazazi,wapo waliowafanya watoto wao mazombi na wapo wengine wanaingiliwa kinyume na maumbile na wapo ambao hawazai au jogoo hapandi mtungi na hana mtoto;wengine wamefunga mizukule kwenye vyumba maalum kwenye nyumba zao.

Ukifanya tafiti utakuta mara nyingi utajiri wowote unaopatikana kutoka kwa Shetani uwa una majuto mengi Sana na uwa haudumu kama utajiri utokao kwa Mungu;pia matajiri hao wakifilisika ushia kuwa masikini wa kutupa .

Neno la Mungu linasema utajiri na heshima upo kwa Bwana.Pia kwenye Mithali inasema "Baraka za Mungu hazina huzuni ndani yake" tofauti na za Shetani zimejaa huzuni nyingi ndani yake ikiwemo kuteseka kwa kafara,kutokwa vidonda ndugu,kujamiana na Mama mzazi ,kutolala usiku na kuua mke au mtoto wako umpendae.

Zingatia;Kataa kuvutwa na utajiri wa kipepo au kishetani utakutesa Sana.Yupo Yesu kwa ajili yako ukimwamini atakusaidia mqamini na fanya kazi kwa bidii utafanikiwa.Hacha tamaa maana tamaa ilisababisha fisi kukosa vyote maana utajiri wa kishetani ukukosesha furaha na amani pia utaishia Jehanamu.

Mithali 3:5-6 inasema vyema Sana kwamba"Mtumaini Bwana kwa kila Jambo Wala usitegemee akili yako peke yako na katika njia zako mkiri yeye naye atanyoosha mapito yako.Kumbuka utajiri na heshima vipo kwa Bwana na si kwa Shetani.

KATAA UTAJIRI WA KICHAWI NA KISHIRIKINA.JENGA MAHUSIANO NA MUNGU NA FANYA KAZI KWA BIDII.

Pastor Silla.
 
Imeandikwa Isaya 45:3
“nami nitakupa hazina za gizani, na mali zilizofichwa za mahali pa siri, upate kujua ya kuwa mimi ni BWANA, nikuitaye kwa jina lako, naam, Mungu wa Israeli.”

Bwana ndiye mtoaji ukimcha atakupa hazina
 
Dini ndio zinafuga wachawi wanaoharibu maisha ya watu na mtu anapoharibiwa maisha ndo anajikuta anafanya mambo ya aina hiyo.

Kimsingi ukienda kwenye nyumba yeyote ya ibada kuna wachawi wengi kuliko mtaani hao walio na utajiri wa majini, nashangaa hata viongozi wa Dini wanatimba kwa waganga wa kienyeji.

Chanzo cha hayo uloleta humu ni Dini...
 
Ukisoma Mathayo 4 unakuta shetani alimwambia Yesu atampa milki ya dunia hii akimtukia.

Kwahiyo basi Kuna pande mbili za utajiri;Utajiri wa KiUngu na utajiri wa kishetani.
 
Hela ya shetani haiendi bure at the end ni lzm akutoe kafara.
 
Dini ndio zinafuga wachawi wanaoharibu maisha ya watu na mtu anapoharibiwa maisha ndo anajikuta anafanya mambo ya aina hiyo.

Kimsingi ukienda kwenye nyumba yeyote ya ibada kuna wachawi wengi kuliko mtaani hao walio na utajiri wa majini, nashangaa hata viongozi wa Dini wanatimba kwa waganga wa kienyeji.

Chanzo cha hayo uloleta humu ni Dini...
Dini ni imani.Matendo ni mtu binafsi
 
Utajiri kutoka kwa Yesu ni uwongo uliokubuhu. Yeye anasema tafuteni ufalme wa Mungu, mengine yote ni kwa ziada. Yesu alipochukuliwa na shetani pake mlimani ilidhihirisha wazi kuwa utajiri wa dunia ni mali ya shetani. Zingatia " kwa tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu ni sawa na ngamia kupita kwenye tundu la sindano." Ndugu yangu unavyoviona sivyo vilivyo, Kuna ushetani wa ajabu.
 
Kwa mungu ni wapi?!
Kwa Mungu Jehovah ni utajiri wa raha unainjoi na ndugu zako utajiri wako Pasipokuteseka wala masharti mfano mfanye msukule kisha mlawiti mama,baba, mtoto wako Ili kumfurahisha shetani Ili akupe mali,akikinai ukutoa kafara anywe damu yako.
 
Kuna imani mbili ya Mungu na ya shetani ya Mungu haishindwi.
Sijakataa Mungu hashindwi, ila nioneshe hata Kanisa moja ambalo vipofu wanaona, viwete wanatembea, nk maana hizo ndo kazi zinatakiwa kuonekana katika nyumba za Mungu wa kweli...

Ndio sababu nimesema Imani kwa nyakati hizi, zinalea uovu...
 
Sijakataa Mungu hashindwi, ila nioneshe hata Kanisa moja ambalo vipofu wanaona, viwete wanatembea, nk maana hizo ndo kazi zinatakiwa kuonekana katika nyumba za Mungu wa kweli...

Ndio sababu nimesema Imani kwa nyakati hizi, zinalea uovu...
Waliopata ulemavu na upofu,magonjwa kwa kulogwa wanapona.Waliozaliwa kwa mapenzi ya Mungu Mungu kaweka kusudi.
 
Nyakati za Sasa dunia pamoja na nchi yetu ya Tanzania imekumbwa na roho chafu ya kutafuta au kupenda mali au utajiri wa kichawi na kishirikina.

Watu waliowengi wapo tayari kuua au kumiliki majini na kutia kafara mbalimbali za damu kwa Shetani ilimradi wapate pesa ,mali na utajiri.

Wapo ambao wanashirikina tendo na Mama zao wazazi,wapo waliowafanya watoto wao mazombi na wapo wengine wanaingiliwa kinyume na maumbile na wapo ambao hawazai au jogoo hapandi mtungi na hana mtoto;wengine wamefunga mizukule kwenye vyumba maalum kwenye nyumba zao.

Ukifanya tafiti utakuta mara nyingi utajiri wowote unaopatikana kutoka kwa Shetani uwa una majuto mengi Sana na uwa haudumu kama utajiri utokao kwa Mungu;pia matajiri hao wakifilisika ushia kuwa masikini wa kutupa .


Neno la Mungu linasema utajiri na heshima upo kwa Bwana.Pia kwenye Mithali inasema "Baraka za Mungu hazina huzuni ndani yake" tofauti na za Shetani zimejaa huzuni nyingi ndani yake ikiwemo kuteseka kwa kafara,kutokwa vidonda ndugu,kujamiana na Mama mzazi ,kutolala usiku na kuua mke au mtoto wako umpendae.

Zingatia;Kataa kuvutwa na utajiri wa kipepo au kishetani utakutesa Sana.Yupo Yesu kwa ajili yako ukimwamini atakusaidia mqamini na fanya kazi kwa bidii utafanikiwa.Hacha tamaa maana tamaa ilisababisha fisi kukosa vyote maana utajiri wa kishetani ukukosesha furaha na amani pia utaishia Jehanamu.


Mithali 3:5-6 inasema vyema Sana kwamba"Mtumaini Bwana kwa kila Jambo Wala usitegemee akili yako peke yako na katika njia zako mkiri yeye naye atanyoosha mapito yako.Kumbuka utajiri na heshima vipo kwa Bwana na si kwa Shetani.

KATAA UTAJIRI WA KICHAWI NA KISHIRIKINA.JENGA MAHUSIANO NA MUNGU NA FANYA KAZI KWA BIDII.

Pastor Silla.
Ni imani potofu na mawazo ya kimaskini yaliyokubuhu. Juhudi na maarifa ndiyo njia pekee ya kufikia malengo yako ya utajiri.
 
Back
Top Bottom