Utajiri wa kishirikina/kichawi

Utajiri wa kishirikina/kichawi

Dini ni imani.Matendo ni mtu binafsi
Imani ya kweli uja kwa kusikia neno la Kristo na imani pasipo matendo imekufa uwezi kusema unampenda Mungu au unamuamini halafu unakwenda kinyume na neno au utaratibu wake hiyo imani no bure kwa namna hiyo.

Ndio maana kwenye Yohana Yesu anawaambia wanafafunzi wake ukinipenda utashika amri zangu.
 
Sijakataa Mungu hashindwi, ila nioneshe hata Kanisa moja ambalo vipofu wanaona, viwete wanatembea, nk maana hizo ndo kazi zinatakiwa kuonekana katika nyumba za Mungu wa kweli...

Ndio sababu nimesema Imani kwa nyakati hizi, zinalea uovu...
Kanisa nalochunga Mimi tu watu wamefunguliwa na wamepokea miujiza yao Sana tu.Karibu na wewe upokee muujiza wako mpendwa...
 
Uchawi na ushirikina ni upumbavu na hauna faida kabisa kwenye Jamii.
 
Utajiri wa shetani una masharti ya mateso wa Mungu ni baraka tele.
Utajiri unatoka pande mbili umepewa na Mungu ama shetani
 
Ukimng'ang'ania Yesu aliyekataa utajiri mbele ya shetani atakupa utajiri kweli? Alisema maisha ni mafupi, utajiri wa nini? Ila wasioangalia makunyanzi ndio matajiri. Anaepasua sala kwa kwenda mbele na kutoka moyoni ni kapuku wa kutupwa.
 
Hakuna utajiri wa namna hiyo.

Kama wewe ni Mkristo naamini una ufahamu wa maneno haya;

Mathayo 4
8 Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mlima mrefu mno, akamwonyesha milki zote za ulimwengu, na fahari yake,

9 akamwambia, Haya yote nitakupa, ukianguka kunisujudia.
 
Dini ni imani.Matendo ni mtu binafsi
Dini si Imani;Dini Ni mfumo mwanadamu aliojiwekea kumtafuta Mungu.

Imani inatokana na Neno kuamini;Imani Ni kile kitendo Cha kuamini kitu au Jambo Fulani.
 
Utajiri kutoka kwa Yesu ni uwongo uliokubuhu. Yeye anasema tafuteni ufalme wa Mungu, mengine yote ni kwa ziada. Yesu alipochukuliwa na shetani pake mlimani ilidhihirisha wazi kuwa utajiri wa dunia ni mali ya shetani. Zingatia " kwa tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu ni sawa na ngamia kupita kwenye tundu la sindano." Ndugu yangu unavyoviona sivyo vilivyo, Kuna ushetani wa ajabu.
Ukisoma Zaburi 24 Biblia inasema nchi na vyote vijazavyo Dunia pamoja na wewe Ni Mali ya Bwana.

Pia inasema fedha na fhahabu Ni Mali yake pia inasema Bwana ndie atupaye UTAJIRI.
 
Pastor Silla Ni Kwanini Muumini anapotaka GARI au kitu kingine Chenye thamani kubwa, mchungaji huagiza aombewe ili Ikipate kitu hicho LAKINI Sasa mchungaji anapohitaji kitu chenye thamani kubwa anaomba Waumini wake Wamchangie..!?
[emoji848][emoji848][emoji848][emoji848]
Kwasababu mchungaji Bosi wake Ni Mungu na watenda kazi ni waumini.Na Mungu ameweka mfumo huo na amesema afanyae kazi ya Injili atapata riziki kupitia Injili.
 
Sijakataa Mungu hashindwi, ila nioneshe hata Kanisa moja ambalo vipofu wanaona, viwete wanatembea, nk maana hizo ndo kazi zinatakiwa kuonekana katika nyumba za Mungu wa kweli...

Ndio sababu nimesema Imani kwa nyakati hizi, zinalea uovu...
Sasa utaprove vipi ikiwa UNATAKIWA uone tukio likifanyika.Miujiza ya kweli ipo ndugu Tena wewe ukiokoka utaweza kumuombea mtu na kupona.
 
Ukimng'ang'ania Yesu aliyekataa utajiri mbele ya shetani atakupa utajiri kweli? Alisema maisha ni mafupi, utajiri wa nini? Ila wasioangalia makunyanzi ndio matajiri. Anaepasua sala kwa kwenda mbele na kutoka moyoni ni kapuku wa kutupwa.
2Wakor 8:8 Biblia inasema Yeye(Yesu) alijifanya masikini ili sisi tuwe matajiri.
 
Back
Top Bottom