Utafiti: Wadada wengi wako radhi kutafutiwa wenzi!

Usedcountrynewpipo

JF-Expert Member
Aug 1, 2012
3,638
2,720
Kwa takwimu nilizozikusanya inaonekana wadada wengi wako radhi kutafutiwa wapenzi na marafiki zao wa karibu au na marafiki zao wa kiume ambao wanaonekana kuwa ni mfano wa kuigwa kwenye jamii. Idadi kubwa ya wadada wa aina hii ni wale walioumizwa hasa kwa kutokuwa na wapenzi waaminifu au ambao wako dedicated.

Nimejaribu mara kadhaa kuwaambia wadada mbali mbali kuwa wako tayari niwatafuite mahali pa 'kujiweka'? Wengi wao wameonesha utayari wa hali ya juu na wengine wamekuwa hata wakinipigia kufuatilia wajue nimefikia wapi.

Hii inanidhirishia kuwa hata wazazi wetu kutafutiwa wenzi ilikuwa ni jambo ambalo 'walilifurahia' tofauti na picha ambayo tunaipata sasa hivi kuwa walinyimwa haki yao ya kujitafutia wenzi wa maisha.

Hata mimi sasa tu vitoto vyetu na vitoto vya ndugu zangu ambavyo hata miaka minne havijafikisha, lakini nimeshaanza kuona watoto wa marafiki na jama wengine kama potentially wana ndoa wa uzao wetu. Mara nyingi nawataniaga rafiki zangu kuwa binti yako ataolewa kwetu and they seems to be fine with that...
 
Hao wanaokubali hua wanaanzia kukubali wakiwa na umri gani? kama wameshapita umri wakupata wenza na wako kwenye deadline ni sawa sababau demand ya Nyumba Masaki ,Range,pesa kede kede inapungua mpaka unashanga,mwisho anasema
yoyote utakae jaaliwa,lakini mwanzo huyo huyo anasema yoyote alikua na Package ili umpate...
 
Inawezeakana wewe Ni mwanaume unaechunika au una vijihela kwahiyo hao mademu wanadhani watapata kama wewe, Na acha kutolewa mfano Enzi za mama zetu, wengi wao walikuwa na mapenzi ya kweli sasa hivi ni pesa tu ndicho wanachowaza
 
Na nzuri zaidi utafiti wetu hauhitaji verification. Ukiridhika nao wewe mtafiti kwa kutumia source of research kuwa personal experience yako mwenyewe basi ishaqualify kuwa fact. Long live TZ.
Inawezekana Tanzania ikawa moja ya nchi zenye watafiti wengi sana duniani. Inawezekana hata nachosema, kina-qualify kama utafiti pia.
 
Nadhani kama kungekuwa na huu mchezo vya matumizi ya viungo vya uzazi huko olimpiki......tungejinyakulia medali sana kama sio zote.........

More practice make it perfect.....
 
Kwa takwimu nilizozikusanya inaonekana wadada wengi wako radhi kutafutiwa wapenzi na marafiki zao wa karibu au na marafiki zao wa kiume ambao wanaonekana kuwa ni mfano wa kuigwa kwenye jamii. Idadi kubwa ya wadada wa aina hii ni wale walioumizwa hasa kwa kutokuwa na wapenzi waaminifu au ambao wako dedicated.

Nimejaribu mara kadhaa kuwaambia wadada mbali mbali kuwa wako tayari niwatafuite mahali pa 'kujiweka'? Wengi wao wameonesha utayari wa hali ya juu na wengine wamekuwa hata wakinipigia kufuatilia wajue nimefikia wapi.

Hii inanidhirishia kuwa hata wazazi wetu kutafutiwa wenzi ilikuwa ni jambo ambalo 'walilifurahia' tofauti na picha ambayo tunaipata sasa hivi kuwa walinyimwa haki yao ya kujitafutia wenzi wa maisha.

Hata mimi sasa tu vitoto vyetu na vitoto vya ndugu zangu ambavyo hata miaka minne havijafikisha, lakini nimeshaanza kuona watoto wa marafiki na jama wengine kama potentially wana ndoa wa uzao wetu. Mara nyingi nawataniaga rafiki zangu kuwa binti yako ataolewa kwetu and they seems to be fine with that...
Mi mwenyewee nilielekezwa kwako untafutie..
 
Back
Top Bottom