Utafanyaje kama umeongezewa chenchi?

Marco Seth

JF-Expert Member
Joined
Oct 21, 2022
Posts
4,710
Reaction score
5,700


Kuna muda unakuta Dukani amenunua kitu alafu muuzaji anajisahau anakuongezea chenchi pasipo yeye kujua

Je ghafla ghafla tu umepokea chenchi umeona umeongezewa alf muuzaji yupo busy

Utafanyaje ?

Na Unajiskiaje na alf ulikuwa hauna hela ?
 
Angalia aina ya Duka ulilonunua kama unaona anajiweza unapita nayo ila kama ni la kuunga unga rudisha tu..
Kuna duka walikuwa na utaratibu ,Kuna muda mkienda kuzidishiwa chenji kawaida ,ukirudisha wanachukua hata hawasemi Asante ila ndio hata usoni hawakuangalii,


Msimamo wangu rudisha chenji, huwezi kula ambako hukupanda maadam wewe ni mwanadamu
 
Unarejesha mara moja maana si pesa yako. La sivyo ni kosa la uwizi. Uaminifu ni pamoja na kupokea kilicho halali kwako tu. Au jiulize: je, ungekuwa wewe ungefurahi unaporejeshewa chenji uliyokosea kumpa mteja? Kumbuka kuwa unachopenda kutendewa, vivyo hivyo watendee wengine.
 

Sasa vichenji hivyo vya elfu moja au mbili vitakupeleka wapi? Unavirudisha tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…