Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,501
- 9,280
Uswizi imepiga kura ya kuunga mkono marufuku ya kuvaa Hijabu katika maeneo ya Umma ikiwemo Burka na Niqab zinazovaliwa na wanawake wa dini ya Kiislamu.
Matokeo rasmi yanaonesha kwamba waliounga mkono kura hiyo ya maoni iliyofanyika Jumapili ni asilimia 51.2 huku idadi ya waliopinga ikiwa ni asilimia 48.8.
Mswada huo uliwasilishwa na mrengo wa kulia wa chama cha Swiss People’s Party (SVP) ambacho kilifanya kampeni yake kwa kutumia misemo kama vile “Sitisha itikadi kali”.
Kundi kubwa la Kiislamu nchini Uswizi limesema kuwa hiyo ni “siku ya huzuni kubwa” kwa Waislamu.
“Uamuzi wa leo umefungua vidonda vya kale, na kuongeza pengo la ukosefu wa usawa kisheria, na ishara ya wazi ya kutengwa kwa kundi la Waislamu waliowachache,” Baraza la Waislamu nchini humo limesema katika taarifa iliyotoa, na kuongeza kwamba huenda likapinga uamuzi huo mahakamani.
Serikali ya Uswizi ilikuwa imejitetea dhidi ya marufuku hiyo kwamba siyo jukumu la serikali kuamua kile watakachovaa wanawake.
Kulingana na utafiti uliofanywa na chuo kikuu cha Lucerne nchini Ujerumani, ni sawa na kusema hakuna anayevaa burka na ni wanawake takriban 30 tu wanovaa niqab. Karibu asilimia 5 ya idadi ya watu nchini Uswizi ambayo ni milioni 8.6 ni Waislamu, wengi wao wakiwa wanatoka chuo kikuu cha Uturuki, Bosnia na Kosovo.
Watu nchini Uswizi wana uhuru katika masuala yao binafsi chini ya mfumo wa nchi hiyo unaozingatia demokrasia.
Na mara nyingi huwa kunafanyika kura za maoni juu ya masuala mbalimbali ya kitaifa au eneo.
Hii sio mara ya kwanza suala linalohusu Uislamu kufanyiwa kura ya maoni nchini Uswizi.
Mwaka 2009, raia walipinga ushauri wa serikali na kupiga kura ya maoni inayounga mkono kupiga marufuku majengo yenye minara kama misikiti – hoja iliyowasilishwa na chama hicho hicho cha SVP na kusema kuwa minara ni ishara ya Uislamu.
Bongo5
Matokeo rasmi yanaonesha kwamba waliounga mkono kura hiyo ya maoni iliyofanyika Jumapili ni asilimia 51.2 huku idadi ya waliopinga ikiwa ni asilimia 48.8.
Mswada huo uliwasilishwa na mrengo wa kulia wa chama cha Swiss People’s Party (SVP) ambacho kilifanya kampeni yake kwa kutumia misemo kama vile “Sitisha itikadi kali”.
Kundi kubwa la Kiislamu nchini Uswizi limesema kuwa hiyo ni “siku ya huzuni kubwa” kwa Waislamu.
“Uamuzi wa leo umefungua vidonda vya kale, na kuongeza pengo la ukosefu wa usawa kisheria, na ishara ya wazi ya kutengwa kwa kundi la Waislamu waliowachache,” Baraza la Waislamu nchini humo limesema katika taarifa iliyotoa, na kuongeza kwamba huenda likapinga uamuzi huo mahakamani.
Serikali ya Uswizi ilikuwa imejitetea dhidi ya marufuku hiyo kwamba siyo jukumu la serikali kuamua kile watakachovaa wanawake.
Kulingana na utafiti uliofanywa na chuo kikuu cha Lucerne nchini Ujerumani, ni sawa na kusema hakuna anayevaa burka na ni wanawake takriban 30 tu wanovaa niqab. Karibu asilimia 5 ya idadi ya watu nchini Uswizi ambayo ni milioni 8.6 ni Waislamu, wengi wao wakiwa wanatoka chuo kikuu cha Uturuki, Bosnia na Kosovo.
Watu nchini Uswizi wana uhuru katika masuala yao binafsi chini ya mfumo wa nchi hiyo unaozingatia demokrasia.
Na mara nyingi huwa kunafanyika kura za maoni juu ya masuala mbalimbali ya kitaifa au eneo.
Hii sio mara ya kwanza suala linalohusu Uislamu kufanyiwa kura ya maoni nchini Uswizi.
Mwaka 2009, raia walipinga ushauri wa serikali na kupiga kura ya maoni inayounga mkono kupiga marufuku majengo yenye minara kama misikiti – hoja iliyowasilishwa na chama hicho hicho cha SVP na kusema kuwa minara ni ishara ya Uislamu.
Bongo5