masatujr1985
JF-Expert Member
- Oct 27, 2011
- 1,980
- 780
Ninaandika kwa masikitiko juu ya usumbufu wa watendaji hasa watu wa ofisi za masijala za Manispaa ya Temeke.
Tafadhalini sana acheni tabia zenu za kuzungusha watumishi wa kada mbalimbali wanaofika hapo kupata huduma. Haiwezekani mtumishi afike na kuzungushwa kuwa file lake halionekani kwa wiki 3 mfululizo.
Hii ni tabia ya kurudisha nyuma maendeleo ya nchi kwa kuwa watumishi wanalazimika kutumia muda wa kazi ili kupata document ambazo ingechukua si zaidi ya nusu saa!!! Muda wa kufanya kazi unapunguzwa kwa tabia chafu za ninyi watendaji waovu na wenye kutaka rushwa.
File linapo-move kutoka ofisi moja kwenda nyingine kiutaratibu linakuwa documented kwenye dispatch, kwa nini ionekane file halionekani ofisi zote alhali kwa muhusika mkuu linakuwa lilishatoka?
Hizo rushwa mnazozitaka toka kwa watumishi zitawatokea puani...tahadhari sana kwenu. Msilazimishe watu kuwa wabaya na kuwasababishia matatizo kwa rushwa za 10000 au 50000.
Hili ni andiko la onyo kwenu. Next time nitataja ofisi husika na watu husika mbali ya kuwapeleka TAKUKURU kwa ajili ya rushwa mnazozitafuta.
Muhanga wa ofisi hizi.
Tafadhalini sana acheni tabia zenu za kuzungusha watumishi wa kada mbalimbali wanaofika hapo kupata huduma. Haiwezekani mtumishi afike na kuzungushwa kuwa file lake halionekani kwa wiki 3 mfululizo.
Hii ni tabia ya kurudisha nyuma maendeleo ya nchi kwa kuwa watumishi wanalazimika kutumia muda wa kazi ili kupata document ambazo ingechukua si zaidi ya nusu saa!!! Muda wa kufanya kazi unapunguzwa kwa tabia chafu za ninyi watendaji waovu na wenye kutaka rushwa.
File linapo-move kutoka ofisi moja kwenda nyingine kiutaratibu linakuwa documented kwenye dispatch, kwa nini ionekane file halionekani ofisi zote alhali kwa muhusika mkuu linakuwa lilishatoka?
Hizo rushwa mnazozitaka toka kwa watumishi zitawatokea puani...tahadhari sana kwenu. Msilazimishe watu kuwa wabaya na kuwasababishia matatizo kwa rushwa za 10000 au 50000.
Hili ni andiko la onyo kwenu. Next time nitataja ofisi husika na watu husika mbali ya kuwapeleka TAKUKURU kwa ajili ya rushwa mnazozitafuta.
Muhanga wa ofisi hizi.