Ustaraabu Huu Utaingia Lini Bongo?

Kana-Ka-Nsungu

JF-Expert Member
Oct 4, 2007
2,257
353
Nilifanikiwa kupiga picha hii katika sendoff party moja iliyofanyika huko Manchester weekend hii.

Baada ya DJ kuanza kupiga mduara, kina dada waliokua kwenye meza hiyo walikimbilia kwenye dancing floor na kuacha simu, kamera pamoja na handbags zao kama unavyoona hapo.

Nikajiuliza kimoyomoyo- ingekua bongo wangethubutu kuviacha hivyo vitu hapo? na kama wangeviacha yangewasibu yepi?......
 
S8300114.jpg


Nilifanikiwa kupiga picha hii katika sendoff party moja iliyofanyika huko Manchester weekend hii. Baada ya DJ kuanza kupiga mduara, kina dada waliokua kwenye meza hiyo walikimbilia kwenye dancing floor na kuacha simu, kamera pamoja na handbags zao kama unavyoona hapo.Nikajiuliza kimoyomoyo- ingekua bongo wangethubutu kuviacha hivyo vitu hapo? na kama wangeviacha yangewasibu yepi?......

Teh he teh he teh he.. ingekuwa bongo hata hilo swali lisingekuwepo.. siku hizi hawaibi hizi utilities tu..wanakutoesha na wewe mwenyewe!
 
Mimi nafikiri soo kila sehemu bongo ni wezi, party zinazofanyika New Africa, Kilimanjaro na hotel kama hizo usitegemee kama vibaka uswahili ambao simu ya mkoni wao wanaona dili watakuwepo.

Lakini pia, angalia na mazingira ya nchi yenyewe. Bongo kuna wezi wengi wa mikoba na mifukoni kwa kuwa silimia kubwa ya watu wanatembea na cash mifukoni au kwenye mikoba, lakini tukiwa na utaratibu wa CREDIT/DEBIT card nani atakuibia, hata ukiiba card huwezi kuitumia. Hivyo, huko Europe wakati mwingine wizi wa kijinga kama huo haupo kwa kuwa no cash in the pockets, hata ukiwa nazo ni kidogo sana.
 
Huu mtego Kana, hapo ukipiga hesabu za haraka haraka kuna kama milioni ya kibongo imetelekezwa hapo, ingekua ni kupimana imani tu. Bongo tena kilongalonga chako kikiwa cha gharama sio lazima ukiweke chini ndo wachukue, watakufwata kwenye mduara!Kuna watu wanaenda kwenye shughuli kuiba tu, na wezi wengine ni hao vibarua wa wapambaji- wanaiba mpaka makoti!
 
Ustaarabu wa namna hiyo uliondoka na watu wa kizazi cha mwalimu, ulikuwepo. Kuurudisha sasa itakuwa ngumu sana, ama itatugharimu. Unajua hata mimi nilishangaa sana hapa ofisini kwangu hivi majuzi (niko nje ya nchi), katibu muhtasi akatuma email kwa kila mtumishi, kuwa kama kuna mtu kadondosha noti 'garage' (noti husika ilikuwa ina thamani kama elfu 20 za madafu) aende akachukue kwake. Hiki ni kitu cha kawaida sana hapa mahali, lakini sio uswazi. Hata kanisanani ama msikitini, nina uhakika ukidondosha noti watu hawakurejeshei, wanasunda chini.
 
Ustaarabu wa namna hiyo uliondoka na watu wa kizazi cha mwalimu, ulikuwepo. Kuurudisha sasa itakuwa ngumu sana, ama itatugharimu. Unajua hata mimi nilishangaa sana hapa ofisini kwangu hivi majuzi (niko nje ya nchi), katibu muhtasi akatuma email kwa kila mtumishi, kuwa kama kuna mtu kadondosha noti 'garage' (noti husika ilikuwa ina thamani kama elfu 20 za madafu) aende akachukue kwake. Hiki ni kitu cha kawaida sana hapa mahali, lakini sio uswazi. Hata kanisanani ama msikitini, nina uhakika ukidondosha noti watu hawakurejeshei, wanasunda chini.

Nafikiri umaskini wetu ndio unatutia tamaa ndogondogo, na ukubwa wa gap uliopo kati ya maskini na matajiri, itakuwa ni vigumu ukiokota elfu 20 uirudishe kwa mwenyewe wakati unajua hujaacha hela mboga nyumbani na hujui kesho wanao watakula nini, hiyo bongo ingekua kama bahati na tena unamshukuru Mungu kabisa. Nahisi sehemu kama hiyo kila mtu ana mobile, na hata ukiiba utakamatwa kwa kuwa kuna kamera.
 
..ustaarabu huu utarejea bongo pale kila mtu atakapokuwa na maisha bora!otherwise it's a dream!
 
Back
Top Bottom