Rich Woman
JF-Expert Member
- Dec 18, 2012
- 867
- 558
Wengi tumekua wepesi wa kulaumu hasa linapokuja swala la kutokuitwa kwenye usaili ilihali unaamini una vigezo vyote na wakati mwingine tumekua tukisema watu fulani wanapendelewa ila unapolaumu, je ni kweli ulifuata maelekezo yote uliyotakiwa kuyafuata kabla ya kutuma maombi ya kazi? au unalaumu tu ili uonekane umeeonewa.
Leo sekretariati ya ajira wamewatolea uvivu watu wasiokidhi vigezo na kulalamika hawaitwi kwenye usaili bahati nzuri walitoa kabisa na ushahidi ili kwamba kila mtu apate kujionea mambo ambayo huwa yanajitokeza huko.
Mfano mmojawapo: Zilitangazwa kazi za tutorial assistant na kuna mtu alikua anakidhi vigezo vyote ila alichokifanya sijui labda ungekeua wewe ungempa ajira
hii hapo chini ndiyo barua yake ya maombi ya kazi aliyoituma huko sekretariati
alichokifanya ni kuhighlight sifa zote alizonazo hiyo ndiyo barua yake, na badala ya kuambatanisha passport size hapo chini kuna picha ambazo ndizo alizoambatanisha
Mtu huyo ana shahada ya uzamili ila hicho ndicho alichotuma huko utumishi kweli mtu huyu asipoitwa kwenye usaili anamlaumu nani mimi nilifikiri labda mtu akiwa na shahada ya uzamili akili inakua inafikiri vizuri zaid ya yule mwenye shahada ya kwanza mtazamo wangu.
Kulingana na maelezo ya sekretariati mtu huyo alipigiwa simu na kuulizwa kulikoni kutuma barua kama hiyo huyo mtu maelezo yake alisema kwamba barua yake ya maombi alimpa mpenzi wake amtumie na haakuituma yeye.
NB: Linapokuja swala la future yako usicheze nayo hata ukiwa una mambo mengi kiasi gani kwanini umuachie mtu akufanyie fanya mwenyewe sasa hapo hakuna ajuaye kama ni kweli alitumiwa na mpenzi wake au alituma mwenyewe.
Mifano iko mingi ila huo kwa leo unatosha
kabla hujalaumu hakikisha umefuata hatua zote ulizoagizwa kuzifuata sio unalaumu kumbe mambo uliyoyafanya sio basi jirekebishe maana mara nyingi watu wanaolaumu tu mara nyingi ukijaribu kufuatilia utagundua nyuma ya pazia kuna kitu japo wapo wanaolaumu na wana haki ya kufanya hivyo.
kila la heri katika michakato ya kutafuta kazi ila MAKE SURE YOUR HANDS ARE CLEAN BEFORE YOU POINT A FINGER.
Leo sekretariati ya ajira wamewatolea uvivu watu wasiokidhi vigezo na kulalamika hawaitwi kwenye usaili bahati nzuri walitoa kabisa na ushahidi ili kwamba kila mtu apate kujionea mambo ambayo huwa yanajitokeza huko.
Mfano mmojawapo: Zilitangazwa kazi za tutorial assistant na kuna mtu alikua anakidhi vigezo vyote ila alichokifanya sijui labda ungekeua wewe ungempa ajira
hii hapo chini ndiyo barua yake ya maombi ya kazi aliyoituma huko sekretariati
alichokifanya ni kuhighlight sifa zote alizonazo hiyo ndiyo barua yake, na badala ya kuambatanisha passport size hapo chini kuna picha ambazo ndizo alizoambatanisha
Mtu huyo ana shahada ya uzamili ila hicho ndicho alichotuma huko utumishi kweli mtu huyu asipoitwa kwenye usaili anamlaumu nani mimi nilifikiri labda mtu akiwa na shahada ya uzamili akili inakua inafikiri vizuri zaid ya yule mwenye shahada ya kwanza mtazamo wangu.
Kulingana na maelezo ya sekretariati mtu huyo alipigiwa simu na kuulizwa kulikoni kutuma barua kama hiyo huyo mtu maelezo yake alisema kwamba barua yake ya maombi alimpa mpenzi wake amtumie na haakuituma yeye.
NB: Linapokuja swala la future yako usicheze nayo hata ukiwa una mambo mengi kiasi gani kwanini umuachie mtu akufanyie fanya mwenyewe sasa hapo hakuna ajuaye kama ni kweli alitumiwa na mpenzi wake au alituma mwenyewe.
Mifano iko mingi ila huo kwa leo unatosha
kabla hujalaumu hakikisha umefuata hatua zote ulizoagizwa kuzifuata sio unalaumu kumbe mambo uliyoyafanya sio basi jirekebishe maana mara nyingi watu wanaolaumu tu mara nyingi ukijaribu kufuatilia utagundua nyuma ya pazia kuna kitu japo wapo wanaolaumu na wana haki ya kufanya hivyo.
kila la heri katika michakato ya kutafuta kazi ila MAKE SURE YOUR HANDS ARE CLEAN BEFORE YOU POINT A FINGER.