Usiwe mwepesi wa kulaumu

Usiwe mwepesi wa kulaumu

Hiyo barua ni very extreme mpaka najiuliza kama ndo sample halisi ya maombi mengi yanayokataliwa.

Pia na hao Sekretariati wasijikoshe maana na tangazo lao la kazi ni shida tupu.

Sekretarieti wasijikoshe, lakini uongo ukisemwa sana unakuwa ukweli na wana haki ya kujisafisha.

Mkuu makosa ya kufuata maelekezo ni mengi sana kwenye barua za maombi, kuanzia uambatanishaji wa nyaraka, muundo wa barua yenyewe, na wakati mwingine hata anuani.

Jamaa wanaoajiri wanazingatia kigezo kuwa kushindwa kufuata maelekezo madogo ya ukurasa mmoja ni udhaifu mkubwa kwa muombaji wa kazi na zaidi unaonesha kuwa hukuwa makini/ulipuuzia mchakato wao, kwanini wakuamini na kukupa kazi?

NB: Wametoa mfano extreme ili na sisi tuone ukubwa wa shida yenyewe, wangetoa kigezo cha kukosea anuani au kuambatanisha nyaraka ungesema wanakompliketi, mbona tatizo lenyewe dogo hilo?
 
Boi unajua hesabu za makadirio?

Wimbi la wataka kazi ni kubwa sana kuliko ajira ambazo Serikali inaweza kutoa kwa hiyo usishangae ukaomba kila siku, kila mwaka na bado ukakosa.

Huwezi kutetea ukichaa kwa kigezo cha uonevu aisee, maana yake ni kuwa huyu mtu akiajiriwa wakimtibua tu kidogo kazi hazifanyiki, sio?

Sijui hasa ubora wa elimu yetu, lakini ukweli ni kuwa watu hawajui kuandika 'kava leta' bila kujali elimu yao, ushahidi mdogo ni hata uandishi wao wa mtandaoni na SMS, chunguza vema.

Kingine ni uvivu wa kusaka fursa mkuu, fikiria CV mtu anaomba template afanye kuhariri tu, barua za kazi hivyo hivyo na kadhalika. Inakuwaje kama huyu unaemuomba akutumie mfano wa barua wewe ujaze taarifa zako tu anakuwa amekosea, na wewe unakosea automatikale...

Kingine kinachoonesha uvivu ni kale kamtindo ka nisaidie kupost, kuna watu kadha niliwaonesha fursa, anakuambia ukiandika barua muandikie na yeye, si umburula huu kaka? Mtu ambae kazi ndio mkombozi wake anataka kijana mwenzake umfanyie harakati.

Ukishaona dalili kama hizi jiulize hao watu wana kiwango gani cha kujitoa na kufanya kweli harakati za kusaka kazi... Kumbuka harakati za kutafuta kibarua haziishi kwenye kuandika maombi ya kazi na kungoja kuitwa usaili pekee, ni jambo pana na mtambuka!

Well said mkuu, but nliposimamia ni kwa huyu mjOmba rushwa na kubebana, kumbuka ukifanya research uwez kosa wa type iyo makazini ambao hawajui pia baadh ya vitu vya kazi yao, that is why makadirio yangu 1980's based on corruption na kubebana...
 
Back
Top Bottom