Usiumie wala kuhuzunika pale unapopoteza marafiki

Usiumie wala kuhuzunika pale unapopoteza marafiki

Veteran Sailor

JF-Expert Member
Joined
May 28, 2025
Posts
1,670
Reaction score
3,269
Habari za wakati huu wana JF..
Naomba niende moja kwa moja kwenye mada..
Tumekuwa tukisikia au kuona baadhi ya ndugu au rafiki zetu wakilalamika kuwa marafiki zao wamewatenga..
wengine wamebadilika hawawakumbuki tena kama ilivyokuw hapo kabla..
Naomba nikukumbushe kitu katika maisha..

Kawaida Marafiki huja na kwenda kulingana na sababu zifuatazo
1. Mazingira
Unaweza kupata rafiki kwa sababu ya mazingira mliyopo inaweza kuwa kazini na baadaye kazi inapoisha au mmoja kuhamishwa na urafiki unaishia hapo.

2. UMRI
Kuna umri mtu atafikia na kuona baadhi ya marafiki hawana faida kwake akaamua kuwapunguza.

3. Ndoto tofauti
Mkiwa kwenye urafiki na mkajikuta kila mtu ana ndoto yake ktk maisha mara nying urafik huo huwa haudumu muda mrefu..

4. Mafanikio
Hapa ndipo urafiki mara nyingi hufa kwa baadh ya watu..

Wengi ambao wanakuwa wamefanikiwa huanza kujitenga na marafik zao wa zaman(ambao wanajitafuta) na kuunda urafiki na watu wapya waliofanikiwa..
 
Mimi niko upande wa pili, Kifo
Niliumia sana pale nilipokwenda Tanga na kuambiwa kuwa rafiki yangu wa utotoni alifariki miaka kama 3 nyuma kwa ajali ya basi.

Nilikuwa nae na kusoma nae na kucheza nae, ila kumbe alifariki miaka 3 nyuma.
 
Nakumbuka kuna mzee wangu mmoja alikuwa akinipigia simu kila siku . Akiniita mkuu ili nimnunulie kinywaji. Namnunulia hadi anatosheka na nauli juu nampatia. Mambo yalivyobadilika kidogo ahhh. Hata simu alikuwa hapokei kabisa
Pole mkuu..
Asilimia kubwa ya watu hivi sasa umpenda mtu kutokana na Kitu chake na sio utu wake
 
Mimi niko upande wa pili, Kifo
Niliumia sana pale nilipokwenda Tanga na kuambiwa kuwa rafiki yangu wa utotoni alifariki miaka kama 3 nyuma kwa ajali ya basi.

Nilikuwa nae na kusoma nae na kucheza nae, ila kumbe alifariki miaka 3 nyuma.
Pole sana ndugu yangu
 
Nimepoteza marafiki wengi kwa kuwakopesha, ukikopesha rafiki fanya kama umetoa sadaka maana wachache hulipa deni.
 
Back
Top Bottom