Acha kupotosha umma...... Kama unauwezo wa kujenga ni bora ukajenga kwanza sababu
1. Nyumba ni asset ambayo value yake inaongezeka kadiri muda unavyokwenda.
2.Nyumba unaweza kuitumia kama dhamana ili upate pesa ya kuweza kukuza mtaji au kuongeza vyanzo vya kipato chako.
3. Kwa hali ya kichumi ya sasa unapoanzisha chanzo kipya cha kipato ni kama kutake risk, mazingira si mazuri na nirahisi kupoteza kuliko kuongeza, hivyo kama hela yako si endelevu basi ni bora ukawekeza kwenye kitu chenye uhakika ambacho kitaonekana kuliko kucheza pata potea.
4.Ukiwa na nyumba unakuwa na aman, hata Ukitoka kutafuta umepata au hujapata ila unajua jioni unarudi kwako ambapo hakuna atakaekubuguzi.
5.Ukiwa na nyumba inakuongezea confidence, unakuwa unajiamini, unaweza kufanya unachotaka kwenye eneo lako, tofauti ukiwa nyumba ya kupanga lazima uombe ridhaa ya mwenye nyumba, hata hitilafu ya umeme huwez ita fundi bila kuwasiliana na mwenye nyumba .
6. Nyumba ni security ya maisha yako, hata mambo yakiyumba inaweza kukusitiri badae, tofauti na biashara ambayo haitabiriki... Mda wowote inaweza kufa.
Points zipo nyingi.... Ila kwa hizo chache mkuu natumai nimekuonesha kuwa kujenga ni muhimu sana kuliko kuongeza chanzo cha mapato... Hasa kama hela yako si endelevu..