Bush Dokta
JF-Expert Member
- Apr 11, 2023
- 12,160
- 20,337
Kwenye nyanja za kupigana vibomu ambavyo kwakweli vinapendezesha mahusiano, unajua bila kuhonga wengine hatujisikii raha na huwa tunapenda watu wanaotuombe hela. Asikudanganye mtu bwana, ukiwa unamhonga anakuwa mtumwa wako.
Sasa bwana katika pita pita za hapa napale nikakutana na vijana wana hustle maisha. Wamepinda kinyama wanajituma ili kuhakikisha Uchumi wa kati unafikiwa. Pamoja na yote wanahonga sana na wanahonga kwa wanawake wanaowazidi vipato!
Yaani wewe unashindia wali maharage kila siku ila unayemuhonga yeye anakula BBQ, chips kuku, pilau na supu.
Sasa unawaza hawa vijana vipi? Wanajua lakini kinachoendelea? Anatokea mwanamke wako siku hizi za weekend anakupigia simu anakwambia nina shida ya laki na 30.
Kumbe wewe unahenya kuipata mwenzako anabeba mashoga zake wanaenda kupiga pombe huku wame-tune ile nyimbo ya "Enjoy" ya Jux maisha mafupi ni Simple ungana nami upoze koo.
Wakati huo wewe umekula maandazi na chai, sana sana plus maharage kwa mama ntilie hapo Gongo la Mboto na uchovu juu.
Wanawake kuweni na huruma basi.
Sasa bwana katika pita pita za hapa napale nikakutana na vijana wana hustle maisha. Wamepinda kinyama wanajituma ili kuhakikisha Uchumi wa kati unafikiwa. Pamoja na yote wanahonga sana na wanahonga kwa wanawake wanaowazidi vipato!
Yaani wewe unashindia wali maharage kila siku ila unayemuhonga yeye anakula BBQ, chips kuku, pilau na supu.
Sasa unawaza hawa vijana vipi? Wanajua lakini kinachoendelea? Anatokea mwanamke wako siku hizi za weekend anakupigia simu anakwambia nina shida ya laki na 30.
Kumbe wewe unahenya kuipata mwenzako anabeba mashoga zake wanaenda kupiga pombe huku wame-tune ile nyimbo ya "Enjoy" ya Jux maisha mafupi ni Simple ungana nami upoze koo.
Wakati huo wewe umekula maandazi na chai, sana sana plus maharage kwa mama ntilie hapo Gongo la Mboto na uchovu juu.
Wanawake kuweni na huruma basi.