Usiombee kukosa hela


Maisha ni kupanda na kushuka....ni kujifunza kutokana na makosa..boranukipata helanununue msos wa kutosha ..ukipata tena unaongezea msos..hakikisha kastock ka msos hakakauki..maisha haya kutegemea rafiki yalishapitaga
 
Duh! Pole sana mkuu,mimi nina changamoto ila kuna watu mnapitia magumu zaidi.
 
mkuu si ungewapigia watu wote uliokuwa nao kwenye simu angetokea mtu tu akutumie hata elfu 5
Weee! Ogopa sana Mkuu..

Hapo kumbuka sina mazoea na watu kabisa ya ya kimawasiliano + kingine kuna hali flani inatokea hata ukimtafuta kabisa jamaa wa karibu akupige tafu ndio hana muda au anajivuta zaidi ya siku tatu...ndio maana niliamua kuchagua maisha ya kuwa kivyangu tuu

Siku zote huwa nasema vijana waliozaliwa na kukuta wazazi wao wana hali nzuri ya kimaisha wamshukuru Mungu sana + wawe na Financial discipline.

Pia siku zote mtoto wa maskini akifanikiwa huwa hawachezei furksa kabisa au starehe za hovyo hovyo.

Maisha yana changamoto sana na ndio maana naamini kupitia kazi mpaka siku nitakayokufa.

Sent from my SM-J500H using JamiiForums mobile app
 
Mkuu Kuna hela ya songesha 16,500 voda kopa alaf tupa laini yao.
3,500 nunua karanga kilo, alaf buku nununua mkaa, buku jero nunua ile mifuko ya plastic ya kufungia karanga, mia mbili nunua mshumaa, kaanga karanga alaf zifunge ukauze stand

mfukon utabaki na 10,300 hapo buni biashara nyingine inayo endana na karanga hapo weka hata fegi
 
Hahahaa huko shule mzee mtoto ata digest sunlight au lazima apige food tena liuji la dona wanasagia huko na magunzi kidogo ili washibe haraka
Kumbe magunzi ni dili
 
aisee nimejifunza mengi, kumbe tupo wengi tunapitia hali hii, ila kukata tamaa mwiko, one day yes. Daa jana jioni niliktembea kwa miguu toka town mpaka home nikijifariji nafanya mazoezi kumbe nauli sina
"Shuka hapo kituoni chukua boda akulete hapa, ni buku tu"
Hii kauli nilikuwa naiona ni kauli ya kawaida sana, ebwanaehe kuna siku sina hata mia then mwamba ananiambia hivyo, nililengwa na machozi, anyway yalishapita hayo ila kikubwa usikate tamaa
 
Hahahaa huko shule mzee mtoto ata digest sunlight au lazima apige food tena liuji la dona wanasagia huko na magunzi kidogo ili washibe haraka
We jamaa comments zako zinanichekesha hadi naonekana Kama chizi hapa nilipo.
 
So kwa kifupi voda wanatoa mtaji kwa wateja wao
 
Niliwahi shinda njaa siku mbili Sina hata Mia ,
Afu nilikuwa nafanya special exam so washikaji wengi wameenda kwao,
ghafla watot wa jirani wakanambia uncle mama alinunua vitumbua asubuhi ,

Dah nilivila kwa uzuni kinoma nikashushia na maji ,
Kesho yake asubuhi kwenye paper,
Cha kusikitisha mbaka saizi hali ni hovyo.

Umasikini ni mazafaka
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…