Lekanjobe Kubinika
JF-Expert Member
- Dec 6, 2006
- 3,020
- 577
Sirudii tena!!!
Posted by GLOBAL on April 14, 2010 at 9:16am
View GLOBAL's News
Jamaa mmoja alikuwa na mke mzuri sana. Kwa kuwa jamaa huyu kazi yake ilikuwa ni udereva wa malori , muda mwingi alikuwa safarini na hilo lilimyima raha, maana alikuwa akiogopa watoto wa mjini wasije wakamchukulia mke wake!
Jamaa ili kuweka sawa hilo akaamua atafute mlinzi kwa ajili ya kumlinda mke wake asimwendee kinyume. Ndipo akaamua amfuate mdogo wake kijijini ili aje aifanye kazi hiyo.
Yule mke baada ya kuona amebanwa sana kiasi cha kushindwa kabisa kwenda kokote, ikambidi aanze kumshawishi yule mlinzi mdogo mtu mradi amsaidie kumaliza haja yake kutokana na jamaa kutokuwepo kwa muda mrefu.
Dogo huyo kwanza alikataa katakata kumgeuka kaka yake, lakini alipolazimishwa sana alikubali kutembea huku akitetemeka kwa hofu kwamba kaka yake akijua itakuwa soo, hata alipomaliza kuvunja amri ya sita na shemeji yake aliendelea kumsisitiza shemeji yake kuwa iwe siri kubwa.
Siku iliyofuata kaka yake alirudi safari. Dogo akawa na mchecheto kupita kiasi basi akawa anatetemeka muda wote hasa alipokuwa anasalimiana na kaka yake.
Wakati wamekaa sebuleni akanyanyuka na kutoka nje ili japo asiwe karibu na kaka yake maana vile alivyokuwa akimtazama hofu ilimzidi akawa anatetemeka utadhani alikuwa ana homa!
Basi bwana ile anafungua tu mlango kutoka nje, shati lake kubwa alilovaa likanasa kwenye kitasa cha mlango kwa nyuma.
Mara moja dogo akadhani kaka yake alishajua juu ya uchafu waliofanya, hivyo ndiyo anamvuta kwa hasira ajieleze. Hapo hapo bila hata kugeuka nyuma akaanza kupiga kelele kwa hofu Samahani kaka sirudii tena! Lakini yote haya kayataka shemeji!
Kaka mtu aliyekuwa kimya kitini, alishangazwa na hilo akamwangalia mdogo wake kisha akamwangalia mkewe na kumuuliza,
Vipi huyu amechanganyikiwa? Mkewe aye akatoa macho akipepesa huku na huko huku akitetemeka.
Other:
Posted by GLOBAL on April 14, 2010 at 9:16am
View GLOBAL's News
Jamaa mmoja alikuwa na mke mzuri sana. Kwa kuwa jamaa huyu kazi yake ilikuwa ni udereva wa malori , muda mwingi alikuwa safarini na hilo lilimyima raha, maana alikuwa akiogopa watoto wa mjini wasije wakamchukulia mke wake!
Jamaa ili kuweka sawa hilo akaamua atafute mlinzi kwa ajili ya kumlinda mke wake asimwendee kinyume. Ndipo akaamua amfuate mdogo wake kijijini ili aje aifanye kazi hiyo.
Yule mke baada ya kuona amebanwa sana kiasi cha kushindwa kabisa kwenda kokote, ikambidi aanze kumshawishi yule mlinzi mdogo mtu mradi amsaidie kumaliza haja yake kutokana na jamaa kutokuwepo kwa muda mrefu.
Dogo huyo kwanza alikataa katakata kumgeuka kaka yake, lakini alipolazimishwa sana alikubali kutembea huku akitetemeka kwa hofu kwamba kaka yake akijua itakuwa soo, hata alipomaliza kuvunja amri ya sita na shemeji yake aliendelea kumsisitiza shemeji yake kuwa iwe siri kubwa.
Siku iliyofuata kaka yake alirudi safari. Dogo akawa na mchecheto kupita kiasi basi akawa anatetemeka muda wote hasa alipokuwa anasalimiana na kaka yake.
Wakati wamekaa sebuleni akanyanyuka na kutoka nje ili japo asiwe karibu na kaka yake maana vile alivyokuwa akimtazama hofu ilimzidi akawa anatetemeka utadhani alikuwa ana homa!
Basi bwana ile anafungua tu mlango kutoka nje, shati lake kubwa alilovaa likanasa kwenye kitasa cha mlango kwa nyuma.
Mara moja dogo akadhani kaka yake alishajua juu ya uchafu waliofanya, hivyo ndiyo anamvuta kwa hasira ajieleze. Hapo hapo bila hata kugeuka nyuma akaanza kupiga kelele kwa hofu Samahani kaka sirudii tena! Lakini yote haya kayataka shemeji!
Kaka mtu aliyekuwa kimya kitini, alishangazwa na hilo akamwangalia mdogo wake kisha akamwangalia mkewe na kumuuliza,
Vipi huyu amechanganyikiwa? Mkewe aye akatoa macho akipepesa huku na huko huku akitetemeka.
Other: