No body deserves kujibiwa kifedhuli awe mkeo, mume wako au mfanyakazi wako..
Ngoja waje waponde; ila uzuri wengi huponda lkn hufanyia kazi kisirisiri!
Very true! Kwa mwanamke imekuwa issue kwa vile kuna reaction itafuata after action ingawa yaweza chukua ages. Nani anapenda kuwa hit back?
Ideally, unapaswa kutenda wema for the sake of it na sio kwa kutegemea kutendewa in return!
majibu ya dharau yanapunguza mapenzi ndani ya nyumba. Haijalishi yupi anamjibu mwenzio. Kuheshimiana ni muhimu.
Mahusiano kati ya wapendanao hujengwa zaidi na hisia za moyo (Feelings), zikipotea hakuna mapenzi yanabaki mazoea!!
kati ya mambo ambayo yanavuruga mapenzi kati ya wanaume na wanawake ni majibu ya kifidhuli ambayo wanaume huyatoa kwa wake zao. Kuna mwanamke mmoja aliwahi kumnunulia mume wake shati jeusi la mikono mirefu pale mnazi mmoja Dar es salaam mwaka 1974. Kwa bahati mbaya yule mwanaume hakulipenda lile shati kwani mashati ya mikono mirefu si stahili yake ya mtindo.
Sasa badala ya kujibu kistaarabu jamaa likamtoka la kumtoka " wewe ina maana ni kipofu huoni mashati ambayo huwa navaa?" binti wa watu akanyong'onyea asijue la kufanya na shati lake mkononi. Miaka 30 baadaye wakiwa wazee jamaa aliletewa shati nyumbani na wauza mitumba, kwa bahati mbaya hakuwepo ila mkewe alikuwepo. Wauza mitumba walishindwa kuuza kwani mkewe akajibu mwenyewe kulihitaji hayupo.
Mzee kurudi anauliza kama kuna wauza mitumba walikuja kuleta mashati, akaambiwa walikuja. Alipouliza ni kwa nini mkewe hakumchukulia akajibiwa kwamba " tangu lini nikajua aina ya mashati unayovaa?" Mzee akakumbushwa kisa cha miaka 30 iliyopita. Wajukuu zake kusikia ilivyokuwa wakabaki na butwaa kumbe babu yao aliwahi kununuliwa shati na bibi yao akalikataa!!
Wanawake wanaweza wasiwe na kinyongo lakini wana uwezo wa kuweka mambo mioyoni mwao kwa muda mrefu sana. Kwa mfano kama mkeo akikuuliza "nikupikie nini leo" anatarajia umjibu kwa staha. Na kwa bahati mbaya sana wanaume wengi hawaelewi maana ya hili swali. Wanawake hawawezi kusema leo nimetamani kula na wewe chakula cha jioni kwa hiyo wahi kurudi badala ya kwenda kwenye pombe. Wao swali la nikupikie nini linabeba maana kubwa sana.
Wanaume tujifunze kutokuwajibu kifidhuli wake zetu!!
mdau,hli umelifanyia utafiti?
Then do you believe in the saying that.....
Men forget but never forgive.., women forgive but never forget...🙂
No body deserves kujibiwa kifedhuli awe mkeo, mume wako au mfanyakazi wako..
Sija generalize ndugu yangu nimetumia asilimia. Asilimia kubwa ya wanaume ndiyo wanakuwa wa kwanza kuwajibu wenzi wao kifidhuli.Good message, but dont generalize it, both Men and Women need to strike a balance! that is the fact, kuna situation a Man has to do more, likewise the Woman, shida ni unapogeneralize kwamba wanaume ndo wawe hivyo.
Mimi niliwahi shuhudia mke anamtukana mumewe tusi.Alimwambia mumewe wewe mseng............ huku akifoka. Hao wanandoa walikuwa wana zaidi ya miaka 30 wakati huo,ilikuwa mwishoni mwa miaka ya 90. Mume ni tumgambile, mama ni mtu wa kaskazini huko.
Alipoondoka mkewe, yule mzee alinipa maneno ya husia baada ya hapo,nikaona kama ananipotezea muda tu kwa sababu nilikuwa na miaka kama 16, hata mapenzi sijui. Ila maneno yake nayakumbumbuka mpaka leo.
Narudi kwa mtoa mada, haitakiwi kumjibu mtu yoyote ovyo hata kidogo, hata wanawake wanawajibu vibaya waume ua wapenzi wao. Kujibu ovyo hakuna gender ila tabia ya mtu tu
Then do you believe in the saying that.....
Men forget but never forgive.., women forgive but never forget...