Usikate tamaa

Soja p

Senior Member
Joined
Aug 24, 2017
Posts
190
Reaction score
223
Katika maisha , unapoanza kufanikiwa katika kila nyanja,
Nakuhakikishia shetani atakuja na kila aina ya uharibifu, Hasa kupitia kwa watu wako wa karibu.

Ataleta majaribu kutoka pande zote,
Kila mtu atakuzungumzia vibaya, wapo watakao kukatisha tamaa, kukudhalilisha, kukufanya ujihisi mwenye hatia, kukufedhehesha na wengine watakuonea wivu, . . . . etc.
Ni kawaida kujisikia vibaya kwa sababu wewe ni binadamu kama mimi, na kila binadamu ana hisia.

Katika kipindi hiki unaweza hata kumsahau Mungu nakuhisi Mungu hayupo kwakuwa unaona kila unacho Muomba hakuna majibu.

Sikia nikwambie, hilo ni suala la muda tu na kila mtu anapitia, mambo yote yatakuwa sawa.

Ni kipindi kigumu sana kwakuwa katika kipindi hichi utasalitiwa, utaonewa, utahukumiwa, na kusingiziwa. Lakini Mungu atawafichua na kuwaondoa rafiki wabaya wanaokuzuia usisonge mbele.

Wakati umekata tamaa kabisa kwa hayo unayopitia ndipo Mungu atakapokushangaza kwa Ukuu wake, atakubariki kuliko vile ulivyomuomba. Atakufungulia milango ya Baraka na Neema kila kona, Atawaaibisha adui zako. Hapo waliokudharau watatamani wawe hata vijakazi wako. Watakuamkia hata kama una umri mdogo kuliko wao.

Kazana kupambana, usikate tamaa Mungu yupo na wewe. Wewe ni mshindi , Pambana hadi ingwe ya mwisho, ndiyo unaweza. Kwa sababu una Mungu na Mungu ndio kila kitu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Best thread

Sent using Jamii Forums mobile app from my Android phone
 
Sawa lakini jiulize kwa nini wenye hali ngumu ni wengi sana. Nadhani kikubwa ni kuelewa Ndoto ya Mungu juu yako na makusudi yake .. Amani yake itakufunika

Sent using Jamii Forums mobile app
 


-Ndumilakuwili-
 
sometimes mambo yanaharibika mpaka inafikia stage unastack...yaani unakuwa nusu hai nusu mfuu... unakufa ganzi... plan zote zinakuwa locked down... hapo ndo unakaa kimyaaa huku una vuta pumzi ndeeeefuuuu na kuitoa polepole huku ukiwa unaomba patokee muujiza wowote ule wawakukupa faraja... kwa mbaali machozi yakiwa yanakulenga unapokea ujumbe wa msiba wa mtu wako wa karibu ... hapo ndo unamwona aliyekufa ndo shujaaa na mshindi... unaamka na kujiahidi kerekebisha kila kitu...

hii dunia ni ngumu mno... hamna anayefurahia kwa 100%
 
Huwez kupata furaha na aman 100% ......coz kila mtu ana mambo yanayo msonga na kila mtu anaona bola yule kuliko yeye

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ujumbe mzuri sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hakika.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…