SankaraBoukaka
JF-Expert Member
- Jul 2, 2019
- 3,189
- 4,981
- Thread starter
- #21
Bado hujanielewa,, SIASA kama kitu kinachohusisha wanadamu lazima kitaandamana na uhalifu kama huo kwasababu siyo wote wanaoingia kwenye SIASA ni wasafi, ila SIASA yenyewe ni mchezo tu kama nilivyoeleza hapo juu.. Kwahiyo ilitakiwa MWANASIASA mwenye uwezo wa KU-MANIPULATE watumwa vizuri ndo awe anashinda UCHAGUZI.., lakini wengine wanapoona nguvu ya ushawishi unapungua ndo wanatumia nguvu za ziada kama hizo UTEKAJI, Kufukuza wenzao uanachama, kuwaondoa kwenye nafasi za kugombea il hali wameshinda kwenye maoni, Kufunga Makanisa n.kUnawezaje kutenganisha utekwaji wa wanasiasa kimfumo na siasa!?
Kwahiyo utekaji, kudhulumiana, mauaji na kukomoana kutatokea tu kwasababu ya wale walio kwenye hiyo SIASA, ila si sehemu ya SIASA.
Mfano mwanafunzi anayeingia na NYENZO kwenye MTIHANI hapotoshi maana halisi ya MTIHANI kama KIPIMO cha KUKARIRI na UELEWA wa MWANAFUNZI, au ELIMU ila ni UAHALIFU unaofanyika kwenye MTIHANI au ELIMU husika....
Kwenye kila kitu kinachofanywa na binadamu kuna UHALIFU unafanyika ili malengo ya hao WAHALIFU yatimie, ila huo UHALIFU hauondoi maana ya hiko kitu...