Mkwaruzo
JF-Expert Member
- Feb 21, 2011
- 563
- 98
Tumetoka mbali jamani. Japokua nchi yetu haina maendeleo yakuridhisha (ni moja kati ya nchi masikini) bali yapo mambo mengi ya kujisifia na kujivunia kuanzia mtu mmoja mmoja hadi kufikia taifa zima. Ninachotaka kukiongelea ni mfumo mzima wa utumiaji wa simu na
ofa zinazopatikana kupitia maongezi (kupiga simu) na utumaji wa ujumbe mfupi wa maandishi ( short message service). Lakini kwanza acha niwakumbushe kuhusu kipindi cha nyuma kidogo wakati
mtandao unaotumika ulikuwa ni mmoja tu (TTCL) na ikiwa wenye simu walikuwa ni wachache, nao katika kipindi hicho waliweza kuhesabika kama walivyokuwa wanahisabika wenye luninga (Television). Mawasiliano kwa wakati huo hayakuwa ya urahisi sana lakini yaliridhisha kiutumiaje kwa kiasi kikubwa. Kwani utumiaji wa simu kwa wakati huo ulitawaliwa na ustaarabu wa aina ya pekee. Mfano, kwa mtu aliyekuwepo
ng'ambo (nje ya nchi) na akataka aongee na ndugu, jamaa au rafiki yake aliyekuwepo nchini ilimbidi apige simu siku ya/za kabla ili
atowe taarifa ya muda na siku aliyokusudia kuongea nae huyo amtakae (mpigiwaji). Na katika kipindi hicho ilikuwa hakuna kutuma message.
Mambo yalianza kubadilika baada ya kuingia simu za mkononi. Mwanzo aliyekuwa na simu hizo za mkononi (mobile phone) alionekana kuwa ni mtu mmoja kati ya watu wenye hadhi au kipato kizuri. Haikuishia hapo, mabadiliko yaliendelea kwa kadri siku zilivyozidi kusonga hadi kufikia leo hata watoto wadogo wanamiliki/
wanamilikishwa simu.
Kasheshe likaanzia
hapo kwani sasa imekuwa tabu/kero kwa baadhi ya watu kumiliki simu. Au ndiyo limbukeni akipata.............? Imenibidi nitumie neno limbukeni kwasababu mtu ambaye ni mstaarabu hawezi kutumia simu ovyo ovyo.
Unakuta mtu anakupigia simu usiku wa manane, ukimuuliza cha mno nini, eti anakusalimia.
Kweli ndiyo ofa, basi ndiyo kufikia kukosa muda muafaka wa kumpigia mtu kwa kumsalimia au kwa shida zake ndogo ndogo? Huu ni ujinga.
Basi huyo ana afadhali....
kwani kuna huyu anaebip kwa private namba. Na wala siyo
kusema atakubip mara moja kisha yakaisha. Sasa iweje au kujua namba ya mtu ndiyo imekuwa tatizo?
Kana kwamba
haitoshi, kuna na huyu anaekung'ang'aniza umpigie kutokana na staili yake anayokubip. Utaona anakubip zaidi ya mara 20. Ukiwahi kupokea, yeye kakata. Hata ukiamua kumpigia, unakuta namba yake ipo bize kwa kukupigia wewe. Sasa huyu anaeamua kufanya hivi, kama yeye kashindwa kukupigia, anaijua hali yako ikoje hata aamue kukufanyia hivyo? Sijuwi ni lini tutabadilika na kuacha upuuzi kama huu?
Pia inanisikitisha kuwaona hawa dada zetu wanaoingizwa tabuni baada ya kuchukuliwa namba zao za simu na kuingizwa kwenye mtandao au katika magazeti eti wanatafuta wachumba. Wewe unaeamua kumfanyia mwenzako hivi, sijuwi unafaidika kitu gani? Jamani hebu tujistahi nasi tustahiwe, tusikuwe miguu na vimo akili zikabaki za kitoto.
Afadhali ya wote hao, hawa naweza kuwapa namba 1 kwa
kituko chao. Huamua kutembea na ma-hand bag makubwa ili kubebea simu za ndani ambazo ni wireless kusudi apate kudanganya anapopigiwa. Utasikia "ndiyo nimeamka sasa hivi na nilikuwa naelekea bafuni kukoga". Kumbe yupo mtaa wa saba kufuata umbea/mabwana. Hivi niulize, hawa
huwa hawajuwi kuwa za mwizi arobaini? Ninachotaka
kuwakumbusha ni kwamba siku ya ukweli kudhihirika, uongo hujitenga. Napenda
nikuambie wewe msomaji wa thread hii kuwa, siku utakayopata nafasi ya kueleza hisia zako juu ya kitu chochote kile, hakikisha unaitumia vizuri nafasi hiyo. Nami kwa kutumia
nafasi hii sitopenda kuwasahau hawa wenye tabia ya kuchukua simu za watu na kusoma message au kuingia
katika gallary kuangalia vilivyomo au hata kujitumia katika simu zao, na wabaya zaidi ni hawa wanaozifanya simu za wenzao kuwa ndiyo kitega uchumi cha wao kupata muda
wa maongezi (credit) kwa kujirushushiya pesa bila ya ridhaa ya mwenye simu. Jamani hii ni haki?
Huyu mwengine kwa kutojua umuhimu uliyotimia wa kuwa
na simu, huwa hazipi
umuhimu simu anazopigiwa sawa na zile anazopiga yeye eti kwasababu namba iliyompigia (iliyotumika) ni ngeni kwake bila ya kujali huyo mtu anaweza kuwa ni mtu wa karibu kwake au kuna umuhimu fulani kiupande wake kwa kupokea simu hiyo.
Na si jambo la kushangaza kusikia mtu kanuniwa eti kwasababu ya kutaka amfahamu mtu wa upande wa pili (aliyepiga simu). Kwa ufinyu wa mawazo, huyo aliyepiga simu baada ya kuulizwa 'wewe ni nani', huchukia na kujiona hajapewa umuhimu hadi kufikia namba yake kufutwa katika simu ya yule aliyempigia bila ya kuangalia kuwa simu ni kifaa kinachoweza kuletahitilafu aidha ikawa kioo (screen) hakiwezi kuonyesha maandishi yoyote yale au laini ya simu ilipotea na ikabidi kuchongesha laini nyengine yenye namba sawa na ile iliyopotea (swaping). Binafsi naweza kumpigia simu mtu anayenijuwa kwa namba yoyote ile na akanitambuwa bila ya kuniuliza kuwa mimi ni nani. Ila mimi siyo rahisi kwangu kuweza kutambua sauti za waliowengi hadi inanibidi nimuulize mtu aliyenipigia simu kuhakikisha kama ndiye yeye au laa japokuwa katumia namba yake ya kawaida. Na watu kama mimi wapo wengi tu.
Mwisho ni kwa hayu anaeweka picha za ngono/uchi (pornograph) katika simu yake wakati anajuwa kuwa hawezkumnyima mtu simu hiyo. Cha kusikitisha zaidi unakuta mtu huyo anakuwa msambazaji mzuri wa picha hizo, kama vile kaajiriwa.
Wengine wanadiriki kuplay (picha hizo za ngono) katika kundi la watu na kuwasikilizisha sauti za miguno ya kimapenzi hata wale wasiyotaka. Tunaelekea wapi jamani? Au huu ndiyo
ustaarabu wa utandawazi? Kama ni dada/kaka yako aliyepigwa picha akiwa uchi, ungediriki kuisambaza/kumrushia mtu?
Kweli teknolojia imekuja wakati tukiwa bado hatujajipanga na ndiyo maana tunaitumia vibaya zaidi kuliko inavyotakiwa. Wala siyo kama nimekusudia kuwafundisha jinsi ya kutumia simu, la hasha.
Nilichokusudia mimi ni kuvitaja vile vinavyoweza kukukera ima wewe au kumkera mwenzako pindi anapofanyiwa. Sidhanikama kuna shule maalum inayofundisha watu ustaarabu bali ni sisi wenyewe kukumbushana kwa mule tunamofanya mambo kinyume na (maadili) inavyotakiwa. Basi ni wajibu wetu kubadilika.
ofa zinazopatikana kupitia maongezi (kupiga simu) na utumaji wa ujumbe mfupi wa maandishi ( short message service). Lakini kwanza acha niwakumbushe kuhusu kipindi cha nyuma kidogo wakati
mtandao unaotumika ulikuwa ni mmoja tu (TTCL) na ikiwa wenye simu walikuwa ni wachache, nao katika kipindi hicho waliweza kuhesabika kama walivyokuwa wanahisabika wenye luninga (Television). Mawasiliano kwa wakati huo hayakuwa ya urahisi sana lakini yaliridhisha kiutumiaje kwa kiasi kikubwa. Kwani utumiaji wa simu kwa wakati huo ulitawaliwa na ustaarabu wa aina ya pekee. Mfano, kwa mtu aliyekuwepo
ng'ambo (nje ya nchi) na akataka aongee na ndugu, jamaa au rafiki yake aliyekuwepo nchini ilimbidi apige simu siku ya/za kabla ili
atowe taarifa ya muda na siku aliyokusudia kuongea nae huyo amtakae (mpigiwaji). Na katika kipindi hicho ilikuwa hakuna kutuma message.
Mambo yalianza kubadilika baada ya kuingia simu za mkononi. Mwanzo aliyekuwa na simu hizo za mkononi (mobile phone) alionekana kuwa ni mtu mmoja kati ya watu wenye hadhi au kipato kizuri. Haikuishia hapo, mabadiliko yaliendelea kwa kadri siku zilivyozidi kusonga hadi kufikia leo hata watoto wadogo wanamiliki/
wanamilikishwa simu.
Kasheshe likaanzia
hapo kwani sasa imekuwa tabu/kero kwa baadhi ya watu kumiliki simu. Au ndiyo limbukeni akipata.............? Imenibidi nitumie neno limbukeni kwasababu mtu ambaye ni mstaarabu hawezi kutumia simu ovyo ovyo.
Unakuta mtu anakupigia simu usiku wa manane, ukimuuliza cha mno nini, eti anakusalimia.
Kweli ndiyo ofa, basi ndiyo kufikia kukosa muda muafaka wa kumpigia mtu kwa kumsalimia au kwa shida zake ndogo ndogo? Huu ni ujinga.
Basi huyo ana afadhali....
kwani kuna huyu anaebip kwa private namba. Na wala siyo
kusema atakubip mara moja kisha yakaisha. Sasa iweje au kujua namba ya mtu ndiyo imekuwa tatizo?
Kana kwamba
haitoshi, kuna na huyu anaekung'ang'aniza umpigie kutokana na staili yake anayokubip. Utaona anakubip zaidi ya mara 20. Ukiwahi kupokea, yeye kakata. Hata ukiamua kumpigia, unakuta namba yake ipo bize kwa kukupigia wewe. Sasa huyu anaeamua kufanya hivi, kama yeye kashindwa kukupigia, anaijua hali yako ikoje hata aamue kukufanyia hivyo? Sijuwi ni lini tutabadilika na kuacha upuuzi kama huu?
Pia inanisikitisha kuwaona hawa dada zetu wanaoingizwa tabuni baada ya kuchukuliwa namba zao za simu na kuingizwa kwenye mtandao au katika magazeti eti wanatafuta wachumba. Wewe unaeamua kumfanyia mwenzako hivi, sijuwi unafaidika kitu gani? Jamani hebu tujistahi nasi tustahiwe, tusikuwe miguu na vimo akili zikabaki za kitoto.
Afadhali ya wote hao, hawa naweza kuwapa namba 1 kwa
kituko chao. Huamua kutembea na ma-hand bag makubwa ili kubebea simu za ndani ambazo ni wireless kusudi apate kudanganya anapopigiwa. Utasikia "ndiyo nimeamka sasa hivi na nilikuwa naelekea bafuni kukoga". Kumbe yupo mtaa wa saba kufuata umbea/mabwana. Hivi niulize, hawa
huwa hawajuwi kuwa za mwizi arobaini? Ninachotaka
kuwakumbusha ni kwamba siku ya ukweli kudhihirika, uongo hujitenga. Napenda
nikuambie wewe msomaji wa thread hii kuwa, siku utakayopata nafasi ya kueleza hisia zako juu ya kitu chochote kile, hakikisha unaitumia vizuri nafasi hiyo. Nami kwa kutumia
nafasi hii sitopenda kuwasahau hawa wenye tabia ya kuchukua simu za watu na kusoma message au kuingia
katika gallary kuangalia vilivyomo au hata kujitumia katika simu zao, na wabaya zaidi ni hawa wanaozifanya simu za wenzao kuwa ndiyo kitega uchumi cha wao kupata muda
wa maongezi (credit) kwa kujirushushiya pesa bila ya ridhaa ya mwenye simu. Jamani hii ni haki?
Huyu mwengine kwa kutojua umuhimu uliyotimia wa kuwa
na simu, huwa hazipi
umuhimu simu anazopigiwa sawa na zile anazopiga yeye eti kwasababu namba iliyompigia (iliyotumika) ni ngeni kwake bila ya kujali huyo mtu anaweza kuwa ni mtu wa karibu kwake au kuna umuhimu fulani kiupande wake kwa kupokea simu hiyo.
Na si jambo la kushangaza kusikia mtu kanuniwa eti kwasababu ya kutaka amfahamu mtu wa upande wa pili (aliyepiga simu). Kwa ufinyu wa mawazo, huyo aliyepiga simu baada ya kuulizwa 'wewe ni nani', huchukia na kujiona hajapewa umuhimu hadi kufikia namba yake kufutwa katika simu ya yule aliyempigia bila ya kuangalia kuwa simu ni kifaa kinachoweza kuletahitilafu aidha ikawa kioo (screen) hakiwezi kuonyesha maandishi yoyote yale au laini ya simu ilipotea na ikabidi kuchongesha laini nyengine yenye namba sawa na ile iliyopotea (swaping). Binafsi naweza kumpigia simu mtu anayenijuwa kwa namba yoyote ile na akanitambuwa bila ya kuniuliza kuwa mimi ni nani. Ila mimi siyo rahisi kwangu kuweza kutambua sauti za waliowengi hadi inanibidi nimuulize mtu aliyenipigia simu kuhakikisha kama ndiye yeye au laa japokuwa katumia namba yake ya kawaida. Na watu kama mimi wapo wengi tu.
Mwisho ni kwa hayu anaeweka picha za ngono/uchi (pornograph) katika simu yake wakati anajuwa kuwa hawezkumnyima mtu simu hiyo. Cha kusikitisha zaidi unakuta mtu huyo anakuwa msambazaji mzuri wa picha hizo, kama vile kaajiriwa.
Wengine wanadiriki kuplay (picha hizo za ngono) katika kundi la watu na kuwasikilizisha sauti za miguno ya kimapenzi hata wale wasiyotaka. Tunaelekea wapi jamani? Au huu ndiyo
ustaarabu wa utandawazi? Kama ni dada/kaka yako aliyepigwa picha akiwa uchi, ungediriki kuisambaza/kumrushia mtu?
Kweli teknolojia imekuja wakati tukiwa bado hatujajipanga na ndiyo maana tunaitumia vibaya zaidi kuliko inavyotakiwa. Wala siyo kama nimekusudia kuwafundisha jinsi ya kutumia simu, la hasha.
Nilichokusudia mimi ni kuvitaja vile vinavyoweza kukukera ima wewe au kumkera mwenzako pindi anapofanyiwa. Sidhanikama kuna shule maalum inayofundisha watu ustaarabu bali ni sisi wenyewe kukumbushana kwa mule tunamofanya mambo kinyume na (maadili) inavyotakiwa. Basi ni wajibu wetu kubadilika.