Shida na raha
JF-Expert Member
- Aug 8, 2014
- 3,774
- 3,460
Natumai marafiki zangu nyote mko salama na pia hatuna budi kumshukuru Muumba wetu ambae ndo muweza wa yote.
Katika kipindi chote cha maisha tunayoishi tunakutana na mitihani ambayo wengi wao wameshindwa kufaulu hususan kwenye kipindi cha mpito (teenage) kwa lugha ya kueleweka kipindi cha ujana maji ya moto.
Kipindi hiki unakutana na mambo mengi ambayo ukibahatika kuyaepuka mshukuru muumba wako kwa kuwa sio uwezo wako bali ni uwezo wa Mungu wako.
Vitu ambavyo tunakutana navyo ni kama ifutavyo:-
Epuka marafiki walevi: Hawa ni marafiki ambao ukijumuika nao hakuna kitu chochote kitakachoongelewa zaidi ya pombe ambayo haitaleta faida bali hasara kwako. Kikundi hiki niliepukana nacho hadi leo sijawahi kuonja hata kwenye kijiko cha chai.
Epuka marafiki wasio na malengo ya baadae: Hawa wanaingia kwenye makundi mawili,.. Wenye kazi na wasio kazi... Kuna wengine wana kazi na kipato kizuri tu ila hawakushawishi ufanye kitu cha maendeleo bali wanakurudisha nyuma... Kwa wale wasio na kazi, hata wapate kazi za vibarua basi pesa zao huishia kwenye kuponda mali mwisho wa siku wanarudi kwako kukuomba masaada ilihali za kwao wametumia ndivyo sivyo.
Epuka marafiki wanaozungumzia sana masuala ya punyeto: Hawa wanauwa kila kitu mwisho wa siku unajikuta unajaribu yanakukuta ya kuishia kwa waganga kutafuta dawa za kuongeza nguvu za kiume hawa nao ni marafiki feki.
Epuka marafiki wenye kupenda night club: Hawa nao sio wazuri watakufanya uwe zwazwa hautakua unawaza vitu vyovyote vya maelendeleo zaidi za kuponda mali.
Kwa kumalizia ikiwa una msimamo wako uliokuwa nzuri baki nao...
Katika kipindi chote cha maisha tunayoishi tunakutana na mitihani ambayo wengi wao wameshindwa kufaulu hususan kwenye kipindi cha mpito (teenage) kwa lugha ya kueleweka kipindi cha ujana maji ya moto.
Kipindi hiki unakutana na mambo mengi ambayo ukibahatika kuyaepuka mshukuru muumba wako kwa kuwa sio uwezo wako bali ni uwezo wa Mungu wako.
Vitu ambavyo tunakutana navyo ni kama ifutavyo:-
Epuka marafiki walevi: Hawa ni marafiki ambao ukijumuika nao hakuna kitu chochote kitakachoongelewa zaidi ya pombe ambayo haitaleta faida bali hasara kwako. Kikundi hiki niliepukana nacho hadi leo sijawahi kuonja hata kwenye kijiko cha chai.
Epuka marafiki wasio na malengo ya baadae: Hawa wanaingia kwenye makundi mawili,.. Wenye kazi na wasio kazi... Kuna wengine wana kazi na kipato kizuri tu ila hawakushawishi ufanye kitu cha maendeleo bali wanakurudisha nyuma... Kwa wale wasio na kazi, hata wapate kazi za vibarua basi pesa zao huishia kwenye kuponda mali mwisho wa siku wanarudi kwako kukuomba masaada ilihali za kwao wametumia ndivyo sivyo.
Epuka marafiki wanaozungumzia sana masuala ya punyeto: Hawa wanauwa kila kitu mwisho wa siku unajikuta unajaribu yanakukuta ya kuishia kwa waganga kutafuta dawa za kuongeza nguvu za kiume hawa nao ni marafiki feki.
Epuka marafiki wenye kupenda night club: Hawa nao sio wazuri watakufanya uwe zwazwa hautakua unawaza vitu vyovyote vya maelendeleo zaidi za kuponda mali.
Kwa kumalizia ikiwa una msimamo wako uliokuwa nzuri baki nao...