Ushuhuda: Mkojo wangu wa asubuhi ulivoniponya

Mkurya mweupe

JF-Expert Member
Aug 10, 2023
218
740
Hii dunia bhana ina maarifa mengi yaliyojificha. Kuna kipindi niliwahi pata vifungo vya kichawi, nikawa naenda kinyume na dunia inavyotaka. Basi, baada ya kupambana muda mrefu bila kupona, nilikutana na rafiki yangu mmoja ambaye tulikuwa tumepotezana muda mrefu baada ya kuwa tumeachana 823 KJ, Msange JKT. Basi, yule ndugu yangu alinambia tiba ya haya mambo yote ni mkojo wa asubuhi ukifanya kwa imani.

Jamaa yangu alinielezea kwamba ukiamka asubuhi kabla hujaongea na mtu yoyote ule mkojo wa kwanza wa asubuhi kabla hujaongea na mtu yoyote, hakikisha unauweka kwenye chombo unanuia kuondoa mabaya, yaani vifungo, laana, na huku unanuia ukuletee mazuri, then unakunywa kidogo, mwingine unaobaki unaweka kwenye maji huku ukinuia unaenda kuoga, na ukimaliza haujikaushi kwa manuizi, kwa siku saba mfululizo.

Basi, zilikuwa hazijafika hizo siku saba. Mambo yalianza kufunguka, sehemu ambazo nilikuwa nimeomba kazi bila mafanikio nikaanza kuitwa hadi za Serikali ni, mpaka nikawa na uchaguzi wapi niende. Kunywa mkojo ule kulifanya niharishe na kutapika uchafu mwingi sana.

Katika kipindi hicho cha dozi ya mkojo nilishangaa naanza kukubalika sana kwa watu katika mtaa wetu, kitu chochote kilichotaka kufanyika ilikuwa lazima nihusishwe, yaani ile nafsi ya kutambulika kwa watu ikawa kubwa. Kingine katika kipindi natumia dozi ya mkojo, wale watu walionifanyia ubaya nilikuwa nawaota ndotoni napambana nao, nawashinda mpaka muda mwingine nilikuwa nikisema sasa hamwezi kuniroga tena, au nilikuwa naota wananifukuza mbio na kuwaacha huku nikiwatambia na kauli ya hamniwezi tena hata mfanyeje.

Kitu kingine katika siku ya tatu ya dozi ya mkojo nilikuwa addicted sana na betting, basi niliweza kuwin Perfect 12 ya Mbet milioni 125, ambayo ilifanya nifungue kampuni ya kukopesha na kutengeneza ajira kwa jamaa zangu, pamoja na uwakala wa huduma za kibenki na simu.

Kiukweli, tokea kipindi kile mpaka sasa, huwa natumia dozi ya mkojo nikiona mambo hayako sawa, na huwa inalipa. Pia, huwa najitibu wakati wa full moon, nitaelezea full moon huwa inanisaidia vipi kujitibu siku nyingine, kwa hiyo ni marufuku kwenda kwa waganga kwangu mimi. Pia, huwa nafanya meditation, na kamwe huwa siachi kufanya affirmation, yaani kushukuru kwa kile nilicho nacho na ambacho sina. Kuna nguvu kubwa katika kushukuru kwa ulivyo navyo na ambavyo hauna.
 
Back
Top Bottom