Wild sniper
JF-Expert Member
- Apr 3, 2015
- 4,353
- 8,465
Mungu ibariki Tanzania.
Story yangu ilikua hivi...
Siku moja nilienda kumtembelea girl wangu mitaa ya kwao ilikua jioni ya kama saa 1,nilikua na rafiki yangu kanisindikiza, kufika pale yeye akaenda kutembea akatuacha pale. Sasa kuna sehemu tukaenda kukaa karibu na kwao huyo mpenzi maana kwa mda huo asingeweza kwenda mbali si mnajua tena geti kali ..
Ilikua sehemu ya uwanja pia kuna jengo la ghorofa limezungushiwa fensi flani ya kizushi basi tukawa tumekaa chini,, hiyo sehemu ina majani kama uwanja wa mpira hivi... Sasa tukiwa pale mtoto akawa kanikalia kwa juu na lita za hapa na pale zinaendelea . Yani unaweza kudhani tupo kwenye mambo yaleee kumbe walaaaa.
Sasa ghafla tukaona mtu kavaa nguo kama askari hivi anakuja spidi na bonge la RUNGU mkononi aisee yule dada si alikua juu nilimrusha huko nikasimama MBIO sikugeuka hata viatu niliacha pale kitu peku .
Basi mdada akakamatwa pale ikabidi anipigie simu mimi shemeji mtu sasa ambae ndo naandika hapa. Ona sasa walidhani mimi ndo nimekimbia mimi nahadithia tu..
Basi akaniambia njoo kuna ishu imetokea rafiki yako amenikimbia dah basi nikaenda pale kweli amedakwa na walinzi wa ile sehemu nakuta viatu jamaa simuoni.. Basi nikaongea nao pale wakataka wampeleke kwa M/kiti wa S/mtaa eti halafu pale mitaa ya kwao nikawapiga kiswahili nikawapa 10000 ndo wakatuacha wakaanza kumcheka mshkaji aliekimbia tukaongea pale tukawa marafiki tena Pesa hizi wallahi ..
Jamaa nilimkuta mbali sana nikambebea viatu vyake, Yale mahusiano hayakuchukua wiki waliachana kabisa na dharau juu..
Sitakaa nisahau maana huwaga nacheka sana nikikumbuka...
Story yangu ilikua hivi...
Siku moja nilienda kumtembelea girl wangu mitaa ya kwao ilikua jioni ya kama saa 1,nilikua na rafiki yangu kanisindikiza, kufika pale yeye akaenda kutembea akatuacha pale. Sasa kuna sehemu tukaenda kukaa karibu na kwao huyo mpenzi maana kwa mda huo asingeweza kwenda mbali si mnajua tena geti kali ..
Ilikua sehemu ya uwanja pia kuna jengo la ghorofa limezungushiwa fensi flani ya kizushi basi tukawa tumekaa chini,, hiyo sehemu ina majani kama uwanja wa mpira hivi... Sasa tukiwa pale mtoto akawa kanikalia kwa juu na lita za hapa na pale zinaendelea . Yani unaweza kudhani tupo kwenye mambo yaleee kumbe walaaaa.
Sasa ghafla tukaona mtu kavaa nguo kama askari hivi anakuja spidi na bonge la RUNGU mkononi aisee yule dada si alikua juu nilimrusha huko nikasimama MBIO sikugeuka hata viatu niliacha pale kitu peku .
Basi mdada akakamatwa pale ikabidi anipigie simu mimi shemeji mtu sasa ambae ndo naandika hapa. Ona sasa walidhani mimi ndo nimekimbia mimi nahadithia tu..
Basi akaniambia njoo kuna ishu imetokea rafiki yako amenikimbia dah basi nikaenda pale kweli amedakwa na walinzi wa ile sehemu nakuta viatu jamaa simuoni.. Basi nikaongea nao pale wakataka wampeleke kwa M/kiti wa S/mtaa eti halafu pale mitaa ya kwao nikawapiga kiswahili nikawapa 10000 ndo wakatuacha wakaanza kumcheka mshkaji aliekimbia tukaongea pale tukawa marafiki tena Pesa hizi wallahi ..
Jamaa nilimkuta mbali sana nikambebea viatu vyake, Yale mahusiano hayakuchukua wiki waliachana kabisa na dharau juu..
Sitakaa nisahau maana huwaga nacheka sana nikikumbuka...