Kwa pamoja naomba niwashauri yafuatayo:
Kwa kuwa wote mmewahi kuwa viongozi wa juu ndani ya CCM nawashauri bakini kwenye siasa lakini suala la kugombea Urais acheni, kwanza mmelitumikia Taifa kwa kadri mlivyoweza,mmetenda mema na mapungufu mengi kama wanadamu. Tanzania ina watu wengi wenye sifa waacheni nao waonyeshe uwezo wao.
Sumaye, umekuwa kiongozi kwa muda wa miaka 10,mmefanya mambo makubwa pamoja na mambo makubwa kuna mapungufu mengi ikiwa ni pamoja kuuza nyumba za serikali,kubinafisisha viwanda vyetu na mengine mengi wewe ukiwa waziri mkuu leo hii pamoja na mapungufu hayo ambayo yameleta usumbufu mkubwa kwa Taifa hivi leo unataka leo ugombee urais? Nakushauri kaa pembeni ukishauri serikali bila kujali itikadi ya chama.
Lowassa, Umekaa katika uongozi kwa muda mrefu umefanya mengi mazuri hasa ulipokuwa waziri wa ardhi. Ulipokuwa waziri mkuu ulifanya mengi mazuri kwa kuwa mfuatiliaji mzuri lakini kuna mambo mengi ambayo leo hii yamo mioyoni mwa watu kwa kuingiza Taifa pabaya hasa mkataba wa Richmond, mara ukataka mvua za kutengeneza. Hiv husikilizi hotuba za Nyerere kuwa anayependa sana kwenda ikulu hatufai? Pumzika waachie watu wengine wewe umefanya inatosha tuwape nafasi na wengine.
Mwisho, mkumbuke watanzania si wale wa kununuliwa na kofia na vitenge.
Kwa wale ambao bado wanamtazamo finyu ule ule nawaasa waache kusafisha watu waliochafuka.
Kwa kuwa wote mmewahi kuwa viongozi wa juu ndani ya CCM nawashauri bakini kwenye siasa lakini suala la kugombea Urais acheni, kwanza mmelitumikia Taifa kwa kadri mlivyoweza,mmetenda mema na mapungufu mengi kama wanadamu. Tanzania ina watu wengi wenye sifa waacheni nao waonyeshe uwezo wao.
Sumaye, umekuwa kiongozi kwa muda wa miaka 10,mmefanya mambo makubwa pamoja na mambo makubwa kuna mapungufu mengi ikiwa ni pamoja kuuza nyumba za serikali,kubinafisisha viwanda vyetu na mengine mengi wewe ukiwa waziri mkuu leo hii pamoja na mapungufu hayo ambayo yameleta usumbufu mkubwa kwa Taifa hivi leo unataka leo ugombee urais? Nakushauri kaa pembeni ukishauri serikali bila kujali itikadi ya chama.
Lowassa, Umekaa katika uongozi kwa muda mrefu umefanya mengi mazuri hasa ulipokuwa waziri wa ardhi. Ulipokuwa waziri mkuu ulifanya mengi mazuri kwa kuwa mfuatiliaji mzuri lakini kuna mambo mengi ambayo leo hii yamo mioyoni mwa watu kwa kuingiza Taifa pabaya hasa mkataba wa Richmond, mara ukataka mvua za kutengeneza. Hiv husikilizi hotuba za Nyerere kuwa anayependa sana kwenda ikulu hatufai? Pumzika waachie watu wengine wewe umefanya inatosha tuwape nafasi na wengine.
Mwisho, mkumbuke watanzania si wale wa kununuliwa na kofia na vitenge.
Kwa wale ambao bado wanamtazamo finyu ule ule nawaasa waache kusafisha watu waliochafuka.