Mwanamziki wa kimataifa Rayvanny Boy mwenye sauti tamu Kama vanilla au ukipenda unaweza kumwita chui kutoka kwenye moja ya label kubwa Africa WCB, hivi karibuni ameandaa project inayoitwa Flowers ambayo ataitoa kwenye siku maalumu ya Valentine's Day yenye track 8 zikiwa zimekuwa produced na maproducers wakalii wa Bongo Fleva Kama Zesc, Maneck n.k
Katika hii project nimevutiwa Sana na nguo zake ni nzuri sana kama unavyoona kwenye picha lakini tatizo la wasanii wengi wa Bongo wanaishiaga kuzivaa wao wenyewe na crew zao kwenye project waliyoitengeneza kwenye kipindi hicho, baada ya hapo nothing happened.
Ushauri wangu: Rayvanny hizo nguo ni kali sana, ni vizuri ukafanyia biashara usiishie tu kuvaa wewe mwenyewe pekee na zitauza kwelikweli, ukiangalia mwenyewe tu zinauzika bila hata promo kubwa kutokana na uzuri wake ni vizuri ushauri wangu akaufanyia kazi.