Ushauri Wangu kwa Graduates wa 2013

Ushauri Wangu kwa Graduates wa 2013

TEMBO WANGU

JF-Expert Member
Joined
Feb 21, 2014
Posts
930
Reaction score
1,297
Wakuu matumaini yangu ni wazima wa afya!

Mimi ni miongoni mwa hawa graduate wa mwaka 2013, leo napenda niwashauri wale tu ambao hawana kigogo yoyote au mtu yoyote wa kumpigia pande kwenye nafasi za kazi. Mimi nawaombeni bila ya kupoteza mda hapa, nafasi za kusomea ualimu zinakaribia kutangazwa kwa ngazi tofauti tofauti ya cheti au diploma, kozi hizi kwani ni gharama ndogo sana na hasa ukipata vyuo vya selikarini.

Ila kama wewe una kijiuwezo kachukue postgraduate ya uwalimu, ndugu yangu utapoteza muda wa miaka miwili tu baada ya hapo unajihakikishia ajira, japo hutolipwa nyingi lakini la kinne hukosi.

Nimetoa ushauri huu kwa sababu nimeona watu wamekaa mtaani miaka mitatu bila ajira, sasa je ukienda kusomea uwalimu si ungekuwa unazungumza mengine kwa sasa! Kumbuka ni maamuzi magumu yanahitajika kwa sasa, mimi ni mmoja wapo nishachukua maamuzi magumu, hivyo nasubiri muda ufike nikajiunge na uwalimu. Ni kheri kupata mia tano kuliko kusubili elfu tano ya kufikirika.

Natumaini mmenielewa, akiri za kupewa.......
 
usiende kuwa mwalimu kwa sababu ya shida ya hela,kawe mwalimu kwa lengo la kufundisha.
ukitaka hela tafuta shule ukafundishe huku unapigania career yako
 
usiende kuwa mwalimu kwa sababu ya shida ya hela,kawe mwalimu kwa lengo la kufundisha.
ukitaka hela tafuta shule ukafundishe huku unapigania career yako

Na hizi ajira za ualimu nakupa miaka 2 tu zitakuwa za kuomba na kufanya usaili we subiri baada ya 2015 uone unaweza ukasoma ukapoteza muda na kazi ukakosa
 
but kama unataka kusoma kwa ajili ya maarifa all the best
 
Kuanzia mwaka walimu wenyewe wanaanza kuapply kama wengine, hivyo usishangae miaka michache ijayo walimu nao ukawaona wanazunguka na bahasha mjini
 
Na hizi ajira za ualimu nakupa miaka 2 tu zitakuwa za kuomba na kufanya usaili we subiri baada ya 2015 uone unaweza ukasoma ukapoteza muda na kazi ukakosa

kweli mkuu. cha msingi timiza ndoto yako. Msomi huwa anachelewa kufanikiwa but huwa ni lazima afanikiwe iwapo anajituma
 
Na hizi ajira za ualimu nakupa miaka 2 tu zitakuwa za kuomba na kufanya usaili we subiri baada ya 2015 uone unaweza ukasoma ukapoteza muda na kazi ukakosa

wewe ni great thinker unaona mbali,kwann hyo pesa mtu asiinvest let say in agriculture or livestock keeping!
 
Umesoma kozi gani kaka ,cha msingi ni kufanya business hata ya pesa ndogo kwa kuanzia coz ww ni msomi ww unaweza kufa nya kitu kaka kwa umakini kwa hiyo anza na hilo bro
 
uoga wa maisha mkuu, ushauri wako km nguvu za giza...
Cha msingi jitume its just matter of time kwani kila jambo na wakati wake n Mpaji ni Mungu.
 
Sasa hyo pesa ya kulipia postgraduate kwa nini usifanyie ujasiliamal kuliko kusoma tena miaka miwil then ndipo uanze kulipwa hzo laki 4. kwa mtaji wa milion 2 ambazo ungetumia kusoma kusoma postgraduate,baada ya hyo miaka miwili unaweza kuwa unaingiza zaid ya hyo laki nne. Huu ni ushauri wangu
 
Sasa hyo pesa ya kulipia postgraduate kwa nini usifanyie ujasiliamal kuliko kusoma tena miaka miwil then ndipo uanze kulipwa hzo laki 4. kwa mtaji wa milion 2 ambazo ungetumia kusoma kusoma postgraduate,baada ya hyo miaka miwili unaweza kuwa unaingiza zaid ya hyo laki nne. Huu ni ushauri wangu

Umemshauri vizuri mkuu,ni bora awekeze pesa hiyo kwenye biashara akifanya vizuri atasahau hata hiyo ajira
 
Back
Top Bottom