Ushauri: Wafanyakazi kazini hawanipendi

Ushauri: Wafanyakazi kazini hawanipendi

Shaban Mwiga

Member
Joined
Apr 18, 2017
Posts
14
Reaction score
10
Kazini kwangu watumishi wenzangu hawanipendi kutokana na mimi kupendwa sana na wanafunzi kutokana na kuwafundisha vizuri na somo langu kufanya vizuri kuliko masomo mengine na wanafunzi hao kuonyesha kunipenda zaidi mimi kuliko wenzangu, sasa wenzangu wananitenga nifanyaje?
 
Tambua tu wajibu wako na utimize ikupasavyo!
 
Kuna zaidi ya hilo. Hakuna mfanyakazi atakayekuchukia kwa wewe kufaulisha watoto, kwa sababu wanapofaulu wewe huongezewi mshahara wala wao kupunguziwa. Angalia ukaribu wako na uongozi na nini unazungumza uwapo na uongozi au wanafunzi.
 
Ongeza juhudi katika kazi yako, wanafunzi wako wazidi kufaulu viziri kwa idadi kubwa,

Hao wanaokitenda watakuja kukuomba uwafundishe mbinu unayo itumia kufundishia hadi wanafunzi wanafanya vizuri kwenye somo lako unalo wafundisha
 
chapa kaz
nadhani lengo lako si kupendwa na wenzio bali kuelimisha wanafunzi.
pia sku zote penye rizik hapakosi fitna
 
Utachukiwaje na wafanyakazi wote? Jitazame vizuri mkuu.
 
Mwalimu anayefundisha vizuri huwa ni mtembeza fimbo na wanafunzi huwa wanampenda baada ya kumaliza shule na kufaulu.

Kama wewe unapendwa na wanafunzi na kuchukiwa na walimu nachelea kusema kuwa wewe ndio una matatizo binafsi.
 
Sema tu hajitambui. Utaanza kuniogopa mimi maana una sifa za ovyo halafu unadai kuchukiwa.
Hauchukiwi na kufaulisha huko ni uongo.
 
Una hakika hyo ndo sababu pekee,kama ipo jirekebishe,kama hamna kazana,kaza mwendo,piga kazi.
 
Back
Top Bottom