- Thread starter
- #21
Hao unaowazungumzia hapo nawafahamu vilivyo. Sasa ni hivi
Huyo kaka alimpa ruhusa mke wake akamuuguze dada yake, wiki imekatika dada yake bado hali haikuwa nzuri akaomba kuendelea, kilichotokea baada ya hapo sasa. Huyo kaka akaandika kwenye wall yake ya fb "nimemruhusu mke wangu akasalimie wiki moja kaongeza sasa ni wiki ya pili naomba mnishauri nifanyeje?" sasa mtu kama huyo mambo ya yeye na mke wake akayaanike huko hiyo ni nzuri kweli?
lutolucy@ kweli hili suala nimemuuliza ni kitu gani kilichopelekea yeye mpaka akaamua kwenda kwenye wall yake kuomba ushauri na kweli amekiri kufanya hivyo ila siyo kama ulivyoeleza hapo juu yeye kaniambia hivi wakati mkewe akiwa Dar walikuwa wakiwasiliana kama kawaida ilipofika siku ya kurudi kama walivyoagana akamuuliza vipi mwenzangu lina utakuja akamjibu kuwa atakuja jumatatu kwa kumwambia kuwa anamsubiria mdada kutoka dodoma ili aendele na kumwangalia mdada pia kumbuka anasema alikuwa ni mjamzito aliyekuwa akisubiria kujifingua kwa kipindi hicho alikuwa ameshajifungua tayari kwa hiyo hakumwambia kuwa hiyo extension ni kwa ajili ya mzazi.
wiki hiyo ya pili ikawa imepita ikaenda wiki ya tatu ilipofika wiki ya tatu akaendelea kuwasiliana kama kawaida anasema kilichokuwa kinamkwaza ni kwamba mbali na kuwa huko dar mkewe hajawai kumpigia simu kumwambia kinachoendelea mpaka mumewe ampigie ndio anapewa majibu ya kuongeza siku mbele .basi akasema yeye hakujali kwa kuwa ni mtu mzima atajitunza tu.
Pia ansema kuwa ikumbuke kuwa mtoto wao alikuwa ameachwa kwa bibi yake hivyo huyu rafiki yangu alikuwa akimjulia hali kila anapopta huku wakiwasiliana na mama mkwe wake pamoja na mashemeji zake kama kuna kitu kinahitajika aweze kusaidia na ndivyo ilivyokuwa. ilipofika wiki ya nne aliwambia shemeji zake kuwa wamuandae mtoto atakuja kumchukua ili ashinde naye siku ya jumamosi nyumbane kwake. basialivyopiga akapata ushirikiano kwa kuambiwa kuwa hakuna shida kuwa atamfuata.Alivyopiga tena simu kuwa anakuja wakamwambia kuwa mtoto amelala hivyo aje badae kumfuata akasema hakuna shida,ilipofika hiyo baadae akapiga simu tena kuulizia kama yupo tayari akaambiwa kuwa ameenda na bibi yake kwa babu yake kwa hiyo siku hiyo hakuweza kumfuata. kilichokuja mkukwaza mpaka akaenda keweka kwenye wall yake ni pale alipopta bip kutoka kwa mke wake usiku wa saa tatu alivyojaribu kumpigia kujua nini akakumbana na sauti ya mwanae kwenye simu. Alihamaki huku akidhani kuwa huenda mkewe karudi na kufikia kwao hivyo alikuwa akipewa taarifa ili awafuate.na kwakuwa ilikuwa muda wa saa nne akaacha.
kesho yake kuna mdada wa kazi alikuwa amemuacha nyumba basi huyo rafiki yangu akasema awe anakuja tu mchana kwa ajili ya usafi na kuanda chakula ikifika jioni arudi kule aliko mtoto. basi siku ya Jumapili aliporudi muda wa saa nne asubuhi ndipo alipomuuliza vipi mtoto umemuacha kwa bibi yake.yule mdada akamwambia kuwa huyo mtoto hayupo toka jana hivyo walimpeleka kwa mama yake Dar.
Sasa lutolucy... anasema hapo ndipo alipoghabika kwa kusema iweje ukweni wasimwambie ukweli kuwa mtoto alikuwa safarini kuelekea Dar kipindi chote cha mawasiliano?ndipo jiuliza kuna nini kinachoendelea mpaka kufika sehemu wanamsafirisha mtoto 200km bila kumtaarifu mzazi mwenza?kweli ameniambia alijiuliza mambo mengi sana.
sema alichokosea zaidi kwenye hili ilibidi ampigie mama mkwe na kumuuliza jamani amewakosea nini mpaka wanamficha mtoto kuhusu safari aliyokuwanayo kwenda dar wakati kipindi cha siku nzima iliyopita walikuwa wakiwasiliana vizuri?Hapo kwa mjibu wa rafiki yangu ndipo alipokuja kuambiwa kuwa mama mkwe hakupendezwa na kusemwa vile kwa kuwa yeye alifuata maelekezo ya mwanae hivyo huyu rafiki yangu hakupashwa kumpigia yeye ila alitakiwa kumpigia mkewe.
hapo ndi tatizo lilipoanzia mpaka kugombana na mkewe kwenye simu sana na kuona kuwa huenda wanamdharau kwa walichomfanyia.
Kwanza mkewe amekewe amekaa dar wiki nne bila ridhaa yake ?
pili kwa kipindi chote hicho mkewe hampigi simu ya kumtakia heri yoyote mmewe mpaka mume ampigie?
Tatu kumbuka ni kipindi cha likizo kwa hiyo aliyokuwa ametarajia ayafanye na mkewe hayakutimia kwa kuwa mkewe alikuwa amashawaaga rafiki zake kuwa kipindi cha likizo hatakuwa kwake ila atamalizia Dar.
hivyo ikampelekea kujua kuwa kumuomba ruhusa ya wiki moja ilikuwa geresha tu kwa kuwa yeye alikuwa ameshapanga bila hata kumshirikisha mumewe kitambo na marafiki zake.
Nitaendelea kweli tuliongea mengi na ameniomba nimsaidie yaishe mkewe arudi nyumbani mpaka imefika amekuwa akimtumia ujumbie wa maneno ya biblia ili asome na kusamehe yaishe.mfano alimtumia zaburi:130,Mathayo18:21,wagharatia 6:10 na warumi 15:1-2.
Someni na naendelea
___________________________________________________________________________________________