Ushauri wa haraka unahitajika, ndoa inapumulia oksijeni

WA KISHUA

JF-Expert Member
Dec 11, 2012
365
130
Habari zenu wafuasi wa mtandao pendwa na wale wapenzi wa jukwaa hili la mahusiano, natumaini wote ni wazima na mko imara kama Simba sema sio Simba hii ya kina Manara ni uimara wa Simba mnyama.

Pasi na kupoteza wasaha ningependa niendee moja kwa moja kwenye dhumuni la kuandika uzi huu ambao umekuwa sponsered na kampuni yangu inayojihusisha na masuala ya usafirishaji mizigo ndani ya Tanzania na nchi jirani.

Baada ya kupambana na kuweza kuhamia kwenye kibanda changu(Ghorofa moja) maeneo ya Tabata Kinyerezi, nikaona ni vyema nikafanya mambo mengine ya kimaendeleo maana Wahenga husema Muda ni Mali.

Sasa nikawa nimehifadhi gunia za mahindi kama 300 hivi lengo nije kuuza kwa bei ya juu zaidi, hilo suala nikawa nimemshirikisha wife, tatizo ni kwamba kulikuwa kuna kama milioni 25 kwenye akaunti yangu ambayo nilitaka ninunue hizi gari aina ya 'Toyota Crown Athlete' jambo ambalo Wife alilipa baraka kwa mikono miwili.

Lakini wakati nikiwa kwenye mchakato wa kuanza kuagiza nikapata habari njema ya kwamba kuna eneo moja Bagamoyo wanauza viwanja kwa bei poa kabisa na vimepimwa, ikabidi nifunge safari kwenda kuviangalia na jamaa yangu mmoja yupo pale wizara ya Lukuvi.

Basi nikaona ni vyema ninunue hivi viwanja chapchap, kwaiyo ile hela ya gari nika-invest kwenye viwanja viwili nilivyovipata huku bwagamoyo japo sikumshirikisha mke.

Sasa baada ya kupita kama mwezi mke akawa ananiuliza kuhusiana na gari maendeleo yake, nikamwmbia bwana kusema ukweli sikuagiza sema kuna jambo nimefanya, akahoji! jambo gani? nikamwambia nimeamua kununua viwanja.

Baada ya kumwambia hivyo, maneno yakaanza kumtoka kama mtu aliyefungwa mota, mara ooh! utakuwa na mwanamke mwingine nje umeamua kumnunulia ndio maana sikuamua kumshirikisha.

Amenuna sio kawaida, yaani hapo napoandika nimenyimwa unyumba inaelekea mwezi sasa, tunalala mzungu wa nne, no story na amani hakuna, anasema atanipa mpaka atakapomjua mwizi wake.

...Maana uzalendo naona unanishinda... Ushauri wenu

NB : Sio kama gari hatuna, tuna gari mbili, Rav 4 pamoja na Noah, ambayo nilikuwa kwenye mpango wa kuiuza tubaki na gari mbili tuu.
 
Mmmh kuwa makini isije kuwa yeye ndio anayetafuta nafasi ya kuwa na mwingine.

Pili Jitahidi kumueleza ukweli ikiwa pamoja na kumuonesha vielelezo kuwa ni kweli umenuna Viwanja kwa pesa inayolingana na hiyo,na ni jambo jema coz umeamua kufanya Investment badala ya kutumia na ulishauriwa na rafiki yako n ilikuwa fursa kwako .
 
Mmmh kuwa makini isije kuwa yeye ndio anayetafuta nafasi ya kuwa na mwingine.

Pili Jitahidi kumueleza ukweli ikiwa pamoja na kumuonesha vielelezo kuwa ni kweli umenuna Viwanja kwa pesa inayolingana na hiyo,na ni jambo jema coz umeamua kufanya Investment badala ya kutumia na ulishauriwa na rafiki yako n ilikuwa fursa kwako .

Kila kitu nimemuonyesha lakini bado ameshikilia msimamo wake
 
Mpe kiwanja kimoja atatulia, kingine kibaki cha familia au andika jina la mtoto wako
 
hivyo viwanja viko bagamoyo ipi na mimi nataka, kuhusu ndoa itadumu tu, mmbeleze anatingisha kibiriti tu, anadeka mana hata kosa silioni, kwani si umesema vina hati muonyeshe hizo hati zina jina gani. ila jinsi unavyoongea huonekani hata kama una woga na hiyo ndoa, halafu kabila gani wewe MANA HAYO MAJISIFU ULOTOA LOL.
 
Pole sana 'mkodomi' wetu. Ngoja wanaume wenzio wa kushauri Kuwa wao ikiwatokea kama hiyo huwa wana solve vipi.
 
Tumebahatika kupata watoto wawili
katika ndoa mambo kama hayo ni kawaida na si kila mgogolo basi ni kuanza kutafuta watu msuluishe mambo mengne unamaliza kiume
ipo hivi wanawake ni viumbe dhaifu mno kuazia maumbile yao mpk mioyo yao na wakitaka lao lazima liwe na dogo kwao huwa kubwa pia hupendwa zaidi kusikilizwa na kuthaminiwa mawazo yao
najua umefanya jambo la maana sana ila kwa kuwa hujamshilikisha yeye kwake imekuwa kesi kubwa
cha kufanya viwanja si vipo viwili nenda nae vyote mkaandikishe watoto ili aamini kuwa hujamnunulia mchepuko na kama katika hizo pesa kipo kilichobaki kampige shopping kali
au lah pigana kiume kabla mwezi hujaisha ununue hiyo gari kesi iishe mambo yaende
7bu kiukweri ulikosea ulitakiwa umshilikishe ndiyo ni mkeo huyo
hiyo ndo sifa ya ndoa kushauliana.
sasa angekubali angekataa we ungenunua tu hivyo viwanja kama jambo lina maslahi hiyo ndo sifa ya uanaume kuwa na maamuzi ya mwisho
kwa hiyo baba kuwa mpole haina haja kutafuta suluhishi nje maliza kiume
 
Back
Top Bottom