proxy
JF-Expert Member
- Jul 3, 2016
- 1,468
- 1,329
Heshima yenu nyote wapambanaji wenzangu.Matumaini yangu mmeamka na mnaendelea vizuri na majukumu ya kila siku. Tuje moja kwa moja kwenye mada.
Ipo hivi ukitaka kufa masikini kama unafamilia tayari kwepa kuhudumia familia yako au jifanye majukumu yako huyajui na umwachie mkeo ndio atunze familia.
Kuna uhusiano mkubwa sana baina ya fikra za mwanaume katika kuhudumia familia yake na mafanikio yake.
Sijui mnanielewa ndugu zangu wa kiumeni?
Kuhudumia familia kunaleta baraka kwa mwanaume, huamsha ari na shauku, humpa nguvu, humuongezea ubunifu na bidii.
Kila anapoamka asubuhi akijua kuwa watoto wanatakiwa wale, wavae, wasome, wafanikiwe, mke inatakiwa avae, apendeze, ale na kila kitu kiwe sawa kutokana na kipato chake inatosha sana kumfanya aweke juhudi na apambane kuhakikisha hilo linafikiwa na kwa kufanya hivyo inamfungulia mlango wa mafanikio kadiri umri unavyozidi kwenda mbele.
Ila sasa hapo inabidi mwanamke( mke) nae ahakikisha haui hii hamasa ya mume, anatakiwa kumtia moyo na kumuamini kwa vitendo.
Usijaribu kabisa kupuuza juhudi zake wala uwekezaji wake kwako hata kama ni mdogo kiasi gani usijaribu kupuuza nguvu zake usijaribu kuona afanyacho hakina thamani.
Kukuhudumia wewe na watoto wako ni upendo mkuu na mara nyingine mimi husema wanaume wanapo amua kuchagua mke wa kuoa sio kwa ajili ya ngono ni kwa sababu wanahitaji faraja na mtu wa kushea nao maisha.
Good Morning dear Friends
Ipo hivi ukitaka kufa masikini kama unafamilia tayari kwepa kuhudumia familia yako au jifanye majukumu yako huyajui na umwachie mkeo ndio atunze familia.
Kuna uhusiano mkubwa sana baina ya fikra za mwanaume katika kuhudumia familia yake na mafanikio yake.
Sijui mnanielewa ndugu zangu wa kiumeni?
Kuhudumia familia kunaleta baraka kwa mwanaume, huamsha ari na shauku, humpa nguvu, humuongezea ubunifu na bidii.
Kila anapoamka asubuhi akijua kuwa watoto wanatakiwa wale, wavae, wasome, wafanikiwe, mke inatakiwa avae, apendeze, ale na kila kitu kiwe sawa kutokana na kipato chake inatosha sana kumfanya aweke juhudi na apambane kuhakikisha hilo linafikiwa na kwa kufanya hivyo inamfungulia mlango wa mafanikio kadiri umri unavyozidi kwenda mbele.
Ila sasa hapo inabidi mwanamke( mke) nae ahakikisha haui hii hamasa ya mume, anatakiwa kumtia moyo na kumuamini kwa vitendo.
Usijaribu kabisa kupuuza juhudi zake wala uwekezaji wake kwako hata kama ni mdogo kiasi gani usijaribu kupuuza nguvu zake usijaribu kuona afanyacho hakina thamani.
Kukuhudumia wewe na watoto wako ni upendo mkuu na mara nyingine mimi husema wanaume wanapo amua kuchagua mke wa kuoa sio kwa ajili ya ngono ni kwa sababu wanahitaji faraja na mtu wa kushea nao maisha.
Good Morning dear Friends