Mojawapo ya eneo ambalo binafsi lina nipa mashaka kwa timu ya Simba ni ulinzi wa kati
Ni kweli ulio wazi kuwa Wawa na Nyoni ni mabeki wazuri .Changamoto kubwa iliyopo ni umri wao. Hawa wanahitaji mtu mbadala wa kuwasaidia na awe na wakiwango kizuri. Ningekuwa kocha ningeanza mapema kuwatumia mara kwa mara Mlipili na Kennedy (aliyetoka Singida) kwa kuwa lolote linaweza kutokea ,na kwa kuzingatia umri wao.
Imekuwa kawaida ya Simba na Yanga kuwasajili vijana na kuishia kusugua benchi na kupotea kabisa .Mohamed Ibrahim,na Isihaka ni mojawao,hawa wangeendelezwa leo Simba isingehitaji Wawa au Shiboub.
Tulishuhudia mwaka juzi Mlipili akiaanza kukomaa kucheza mechi za kimataifa lakini ujio wa Paskal Wawa ulimrudisha nyuma.
Nimeandika haya bila kumjumuisha Mbarazil kwa kuwa kwa historia ya Wabrazil na soka la Afrika lolote laweza kutokea.
Ni kweli ulio wazi kuwa Wawa na Nyoni ni mabeki wazuri .Changamoto kubwa iliyopo ni umri wao. Hawa wanahitaji mtu mbadala wa kuwasaidia na awe na wakiwango kizuri. Ningekuwa kocha ningeanza mapema kuwatumia mara kwa mara Mlipili na Kennedy (aliyetoka Singida) kwa kuwa lolote linaweza kutokea ,na kwa kuzingatia umri wao.
Imekuwa kawaida ya Simba na Yanga kuwasajili vijana na kuishia kusugua benchi na kupotea kabisa .Mohamed Ibrahim,na Isihaka ni mojawao,hawa wangeendelezwa leo Simba isingehitaji Wawa au Shiboub.
Tulishuhudia mwaka juzi Mlipili akiaanza kukomaa kucheza mechi za kimataifa lakini ujio wa Paskal Wawa ulimrudisha nyuma.
Nimeandika haya bila kumjumuisha Mbarazil kwa kuwa kwa historia ya Wabrazil na soka la Afrika lolote laweza kutokea.