cutelove
JF-Expert Member
- Oct 3, 2017
- 3,317
- 7,509
Kuna mkaka alioa mwanamke miaka kadhaa iliyopita,na katika maisha yao ya ndoa walibahatika kuzaa watoto wawili,wa kike na kiume,wakiwa wanaishi Dar kipindi hicho
Bahati mbaya ndoa ikavurugika,mwanamke akakimbia kwenda kusikojulikana ila akawaacha watoto kwa baba yao
Baadae huyo mkaka akahamia Mwanza kikazi na ndo nyumbani kwao
Siku za hivi karibu alipigiwa sim na mwalimu mkuu wa shule ya msingi ambayo ipo huko ukweni, musoma
Akataka kujua kuna nini,lakini huyo mwalimu alimwambia wewe njoo mara moja hapa shuleni
Basi kaka akaona ngoja afikepo,akaandaa safari akamuaga mke wake ambaye alioa baadae akaenda musoma kwa mwalimu mkuu huyo
Kufika pale mwalimu mkuu wa shule akawaita watoto kama watatu hivi,wa kiume wawili na wa kike mmoja,mwalimu akaanza kumuuliza yule mkaka" Wewe ndo William Dotto? William akajibu" Ndiyo ndo Mimi" Mwalimu akaendelea" Sasa hawa watoto wako,Juma William Dotto,Deborah William Dotto na Jonas William Dotto mbona wana maisha ya ovyo sana,viatu hawana,nguo za shule ni shida,mahudhurio ni mabovu"
William alishangaa kuambiwa watoto hao ni wake,akamuuliza mwalimu " Hawa watoto ni wangu kiaje labda mbona sielewi?
Mwalimu akawambia wale watoto watoke nje maana akawa ameelewa kuwa hapa kuna kitu ,ndipo mwalimu akamwambia,"Mzee nashangaa kuwa na wewe huwafahamu hawa watoto,kwanza walihamia hapa kwa uhamisho kutoka Iringa,mama yao aliwaleta hapa wakiwa na majina hayo ambayo ni ya baba yao ambaye ni wewe,basi tukawapokea,na vyeti vyao vya kuzaliwa jina la baba yao ni William Dotto sasa hatujui nini kinaendelea"
Ndipo William akaamua kumuweka mwalimu wazi,kuwa waliachana na huyo mwanamke ,watoto aliomwachia anaishi nao mwanza,sasa huyo mama alikoenda kutembea akazaa watoto wengine na kuwapachika majina yangu lakini si wanangu hao
Nini cha kumshauri William ? Tangu waachane na mke wake wa kwanza hakumpa talaka kwa kuhofia kupoteza assets zake,pia anaambiwa aajibike kuwatunza watoto ambao si wake ila nyaraka za serikali wanatambuliwa kuwa ni wake
Watoto wa kiume wanasoma Darasa la tano na wa kike la tatu
Majina si sahihi kuficha hadhi ya mtu
Bahati mbaya ndoa ikavurugika,mwanamke akakimbia kwenda kusikojulikana ila akawaacha watoto kwa baba yao
Baadae huyo mkaka akahamia Mwanza kikazi na ndo nyumbani kwao
Siku za hivi karibu alipigiwa sim na mwalimu mkuu wa shule ya msingi ambayo ipo huko ukweni, musoma
Akataka kujua kuna nini,lakini huyo mwalimu alimwambia wewe njoo mara moja hapa shuleni
Basi kaka akaona ngoja afikepo,akaandaa safari akamuaga mke wake ambaye alioa baadae akaenda musoma kwa mwalimu mkuu huyo
Kufika pale mwalimu mkuu wa shule akawaita watoto kama watatu hivi,wa kiume wawili na wa kike mmoja,mwalimu akaanza kumuuliza yule mkaka" Wewe ndo William Dotto? William akajibu" Ndiyo ndo Mimi" Mwalimu akaendelea" Sasa hawa watoto wako,Juma William Dotto,Deborah William Dotto na Jonas William Dotto mbona wana maisha ya ovyo sana,viatu hawana,nguo za shule ni shida,mahudhurio ni mabovu"
William alishangaa kuambiwa watoto hao ni wake,akamuuliza mwalimu " Hawa watoto ni wangu kiaje labda mbona sielewi?
Mwalimu akawambia wale watoto watoke nje maana akawa ameelewa kuwa hapa kuna kitu ,ndipo mwalimu akamwambia,"Mzee nashangaa kuwa na wewe huwafahamu hawa watoto,kwanza walihamia hapa kwa uhamisho kutoka Iringa,mama yao aliwaleta hapa wakiwa na majina hayo ambayo ni ya baba yao ambaye ni wewe,basi tukawapokea,na vyeti vyao vya kuzaliwa jina la baba yao ni William Dotto sasa hatujui nini kinaendelea"
Ndipo William akaamua kumuweka mwalimu wazi,kuwa waliachana na huyo mwanamke ,watoto aliomwachia anaishi nao mwanza,sasa huyo mama alikoenda kutembea akazaa watoto wengine na kuwapachika majina yangu lakini si wanangu hao
Nini cha kumshauri William ? Tangu waachane na mke wake wa kwanza hakumpa talaka kwa kuhofia kupoteza assets zake,pia anaambiwa aajibike kuwatunza watoto ambao si wake ila nyaraka za serikali wanatambuliwa kuwa ni wake
Watoto wa kiume wanasoma Darasa la tano na wa kike la tatu
Majina si sahihi kuficha hadhi ya mtu