Ushauri tafadhali

Ushauri tafadhali

silverita

Member
Joined
Jan 26, 2014
Posts
13
Reaction score
2
Habari wana MMU

Ushauri wenu unahitajika wapendwa
Naomba niende moja kwa moja kwenye mada yangu

Mimi ni mwanamke wa miaka 30, nimeolewa ndoa halali na nina mtoto mmoja. Kinachonifanya mpaka niombe ushauri kwenu wadau ni kwamba hapo awali wakati tunaanza maisha na mme wangu mimi sikuwa na kazi, ndo kwanza nilikuwa nimemaliza chuo na mume wangu alikuwa ananihudumia kwa kila kitu, japo hakuwa na kipato kikubwa sana ila Mungu mwema mambo yalienda vizuri.

Mwishon mwa mwaka 2012 niljaaliwa na mimi nikapata kazi na hapo ndo mambo yakaanza,yaan mume wangu anataka mshahara wangu nikipata nimkabidhi yeye ndo aamue matumizi, wadau mwanzon nilijitahidi kufanya hivyo ila kadri siku zilivyoenda nikaona nashindwa kwani pamoja na hayo yeye mshahara wake hataki mie hata niuguse, naishia kuona kwenye salary slip tu.

Maendeleo ya familia anafanya ila ndoo hivyo anachoamua yeye ndo final, wadau mliopo kwenye ndoa naombeni mnishauri nifanyeje juu ya hili kwani ninakoelekea naona hii hali inanishinda kabisaaa.Kuanzia mwezi january mwaka huu niligoma kumkabidhi kadi yangu ya benki ninayochukulia mshahara sasa ndo imekua nongwa yaani hata matumizi ya vitu vya nyumbani hataki kuacha eti kisa mimi nina kazi na ninalipwa, jamani wanawake wenzangu is this fair, tafadhali nishaurini nifanyeje!!!!!!!!!!

NOTE; Kama huna cha kushauri pita kimya tuu. Asanteni
 
subiri kidogo, kuna kero nyingne za mmeo au ni hilo tu?
 
Samahani... Kabla hamjaoana hamkupewa mafundisho ya dini kuhusu matumizi ya fedha zenu??

Hukufanyiwa kitchen party ukaambiwa jinsi ya kuishi na mwanaume in term of financial???
 
mbona hujasema chochote kama ulishawahi mwambia kuhusu tatizo lako?

kwanini uishi na mkuki moyoni dada?!
 
Si bora hata huyu unamkabidhi mshahara wako afu mnaupangia matumizi yanayoeleweka?

Kuna mwingine anahongea mshahara wako na kulewea pombe.

Chongo hutofautiana, zingine hunuka.
 
Mlipendana bila kujali khali zenu za kiuchumi..msiiruhusu pesa kuharibu mahusiano yenu mazuri..ketini mzungumze,ndoa ina milima na mabonde kufikia jubilee ya miaka hamsini si mchezo ati..
 
Its not fair mshirikishe mpango wenu wa matumizi unataka uweje.
 
Suala la matumizi ya vipato vya mume na mke ni makubaliano yenu nyie wenyewe, hakuna formula maalumu. Muhimu ni maelewano na maendeleo ya kiuchumi ya familia yenu yawepo. Mimi binafsi mke wangu akipata mshahara au hela nyingine yeyote huniletea mimi yote then nachanganya na za kwangu tunapanga bajeti ya familia pamoja,na kumkabidhi yeye kiasi kadhaa ikiwa ni kwa ajili ya matumizi yake binafsi pamoja na ishu za nyumbani kama vile chakula;inayobaki tunaweka benki akiba;pia huwa namshirikisha katika matumizi ya hela yetu kama kuna kitu na yeye anahitaji huwa anasema na tunaangalia bajeti yetu ikoje. Ni mwaka wa kumi na nne sasa tunaishi hivyo kwa amani kuu.
Kwa maisha ya sasa hivi kushirikiana ndo mpango mzima mke na mume kusukuma gurudumu la familia; ongea na mume wako na mwambie kuwa huridhiki with what is happening(mwambie hivyo kwa upendo mkuu na unyenyekevu na sio kwa kufoka au jeuri). Tumia uanamke wako; huyo ni mumeo hakuna mwanaume asiye dhaifu kwa mkewe(if you push the right buttons). Mweleze kwa utulivu mkubwa wewe unavyopendekeza iwe then msikilize anasemaje, mtafikia tu muafaka.
 
Back
Top Bottom