Ushauri: Slaa agombee uenyekiti CHADEMA

Ushauri: Slaa agombee uenyekiti CHADEMA

Kutokana na umahiri aliouonyesha mh.slaa kiasi cha yeye kuwa ndio kama nembo ya chama kwa sasa na ili kuepusha makundi na kuondoa mpasuko unaokinyemelea chadema nadhani ni wakati muafaka na pia kwa maslahi ya chama Dr. Slaa agombee uenyekiti wa chama na Mh. Mabere Marando agombee ukatibu mkuu wa chama.

Nina imani hawa wawili wakifanya kazi pamoja kutokana na ukaribu wao chadema itafika mbali sana na kuondoa dhana kwamba chadema ni chama cha kabila fulani tu.

Nawasilisha.

Umeanza lini kumwamini Marando?
 
ushauli mzuri lakini kwa sasa wabaki hivyohivyo,sababu katibu mkuu akiwa legelege nalo ni tatizo! siuliona yule wa magamba povu lilivyokua linamjaa mdomoni!
 
top ten ya wazinz tz slaa anatisha

Sawa Habib Mchange! Kuweni makini na simu zenu jamani kuna wakwapuaji humu! (Mods huyu my web alibadili ID kishamba live ndio maana tunamjua ni nani)
 
Kim Kardashian, wewe kweli unataka kuua chadema. Yaani mtu ukatibu umemshinda unataka apewe uenyekiti!!!
 
Freeman Mbowe Tosha Uenyekiti Chadema
Dr Slaa Tosha Urais 2015

Freeman Mbowe & Wilbroad Slaa is the best combination ever in this world!
Ili kuondosha msuguano na mgongano wa kimaslahi ni bora kofia hizo mbili zikaunganishwa na kuvikwa mtu mmoja ambae ndie nembo ya chama kwa sasa,yote kwa yote huu ni ushauri tu
 
Umeanza lini kumwamini Marando?

kwani lini alikua haaminiki?mi namuamini sana ni mtendaji mzuri kama aliweza kufanya kazi na kilaza mrema kwa mafanikio makubwa nccr mafanikio ambayo hakuna chama cha upinzani kimeweza kuyafikia so far basi hawezi kushindwa kufanya kazi na msomi kidaktari slaa,apewe tu nafasi anaweza na yeye na slaa wataifikisha mbali chadema
 
kama ulikuwa ndani ya mawazo yangu, haya mafanikio ya cdm yametokana na kazi yake nzuri (hilo halina ubishi) pamoja na mwenyekiti freeman, sasa kama freeman anapumzika na kubakia mshauri wa cdm, basi kwa muda huu basi uwenyekiti apewe dr.slaa.

Ingawa hii itakuwa msumari mchungu kwa wana ccm, watafanya kila kiwezekanalo dr. Asiwepe wadhifa huu mzito ndani ya chama chake.




Mmeshuhudia makundi, uchafuzi na menginyewe lakini kwa nguvu ya umma na kwa sababu tunaongozwa na nguvu ya mwenyezi mungu basi isharah tutawashinda mafisadi na mapesa yao.

Mungu akisimama hakuna linaloshindikana, hata daudi aliweza kumsurubu goriath aliyekuwa na siraha zote za kivita kwa manati tu.

Na sisi cdm tutawasurubu ccm kwa manati tu. Cdm for people, cdm kwa haki ya kila mtanzania.


samahani,hivi unajua kipimo cha unafiki?
 
unafiki na ukweli ni vitu viwili tofauti, sasa sijui kama unajua kuvitofautisha.
 
Freeman Mbowe Tosha Uenyekiti Chadema
Dr Slaa Tosha Urais 2015

Freeman Mbowe & Wilbroad Slaa is the best combination ever in this world!
Mkuu wangu Molemo,Mbowe alishasema hatogombea tena!
 
Last edited by a moderator:
Uenyekiti hauna ulaji kama ukatibu mkuu kwenye chama,babu hawezi kukubali labda dau la mshahara kwa mwezi lipande toka Mil 7 mpka 16.
 
Kama unataka chama kife kwa dakika moja huyu jamaa awe katibu mkuu!kamahujui uliza yaliyotokea 1996 kwa NCCR MAGEUZI!
Mkuu TUKUTUKU,huyu si ndio mkuu wa kitengo cha intelejensia wa chama sasa unataka kusema taarifa anazotoa babu za kiintelejensia ni fafa?
 
Mkuu TUKUTUKU,huyu si ndio mkuu wa kitengo cha intelejensia wa chama sasa unataka kusema taarifa anazotoa babu za kiintelejensia ni fafa?
Babu ndiyo nani?tafadhari nijulishe kwanza ili tuendelee na mjadala!
 
CDM sio CCM, Slaa abaki pale pale, na hii itatusaidia kuondoa kasumba kuwa mwenyekiti ndoo mambo yote. Pili Slaa atakavyokura rais CDM hatutampa uenyekiti, mwenyekiti atachaguliwa mwingine, kama mheshimiwa Mbowe atagombea tena au mwanacDM mwingine lakini si Dr. Slaa. CDM hatutachanganya chama na serikali.
 
je huoni kwamba ameshatumia vya kutosha ukatibu mkuu na sasa anatosha kwa uenyekiti?au unataka awe katibu mkuu wa kudumu kama yule seif shariff hamad wa cuf?

Au kwa vile huko MAGAMBANI kwenu mmezoea kubadilisha Makatibu Wakuu kwa sababu za kupwaya, basi lazima na CHADEMA kibadilishe Katibu Mkuu????

CHADEMA mambo hayaendi hivyo. Udhaifu wa MAGAMBANI usitake uwe ndiyo muongozo kwa CHADEMA. Kama chama makini, CHADEMA kina taratibu zake. Hivyo kila jambo litashungulikiwa kulingana na matakwa ya Katiba na hali ya Kimazingira na sio kwa sababu MAGAMBA wanafanya vile basi na CHADEMA kifanye vivyo hivyo. Hapo ndiyo unauona UTOFAUTI wa CHADEMA na MAGAMBACCM.
 
Back
Top Bottom