Ushauri: Presidential Delivery Unit (PDU) irejeshwe

Ushauri: Presidential Delivery Unit (PDU) irejeshwe

KARLO MWILAPWA

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2019
Posts
3,117
Reaction score
5,321
Kwako,
Rais wa JMT,
Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan,

Awali ya yote nachukua nafasi huu kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema na huruma kwa kutujalia afya njema na uzima mpaka muda na wakati huu.

Mhe. Rais, ni heshima kubwa kwangu kukuandikia maoni na ushauri wangu katika kusukuma mbele gurudumu la maendeleo ya Taifa letu.

Mhe.Rais, tumemaliza uchaguzi Mkuu ukiwa umepata ushindi wa kishindo na kuaminiwa na watanzania kwa kiwango Cha juu sana, ni jambo la kukupongeza.

Katika kipindi chote Cha kampeni umetoa ahadi za matumaini makubwa kwa kesho ya Taifa letu na wananchi wamezikubali ndio maana wakapiga kura ya ndio na sasa ni wakati wa kufanya utekelezaji wa ahadi hizo.

Katika kutafakari ndio nikakuikumbuka 'Presidential Delivery Unit' (PDU )iliyoundwa na kusimamia sera ya matokeo makubwa sasa (BRN) hivyo kuwa chombo muhimu sana katika ufuatiliaji na kufanikisha malengo ya Serikali hivyo nashauri kurejeshwa upya kwa kitengo hiko Cha PDU ili kisaidie kusimamia kwa karibu utekelezaji wa makusudi ,malengo ,vipaumbele na matarajio ya Serikali yako.

Naomba kuwasilisha.
Ahsante
 
Tunataka katiba mpya sio hizi porojo zenu
 
Hiki chombo kitasaidia na kuharakisha utekelezaji wa

1.ahadi za Rais alizotoa kipindi Cha kampeni
2.sera za muda mrefu na mfupi zilizopo kwenye mpango wa Taifa wa maendeleo
3. kuweka na kupanga vipaumbele kwa kipindi Cha miaka 5 na kusimamia utekelezaji wake
4. Kufanikisha na kusimamia kwa ukaribu wa utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM
5. Pia chombo hiki kitasaidia kuwa nyenzo na daraja la usimamizi, utekelezaji na ufuatiliaji kati ya wizara na ofisi ya Rais ikulu.
 
Back
Top Bottom