Ushauri posa ikubaliwe au ikataliwe

Ushauri posa ikubaliwe au ikataliwe

evangelical

JF-Expert Member
Joined
Nov 21, 2011
Posts
5,970
Reaction score
9,898
Ushauri unahitajika.

Kuna jamaa yangu aliwahi kuzaa anabinti mwezi wa 9 mwaka huu anafikisha miaka 18 huyo binti alimaliza form 4 mwaka 2024. Hakufaulu yupo nyumbani.

Sasa juzi kuna jamaa walikuja nyumbani kwake wakaleta post kwamba kuna kijana wao anataka kumuoa huyo binti wake wakaeleta posa pamoja na sh laki moja.

Sasa jamaa analalamika kwamba binti yake bado mdogo.

Hako kabinti mi mwenyewe nakafahamu bado kana akili za kitoto kabisa .

Jamaa kamuuliza binti yake kasema huyo mtu hamjui kameambiwa kuhusu kuolewa kenyewe kamaebaki kushangaa hakaelewi.

Sasa jamaa kapokea posa majibu hajawapa .

Sasa jamaa anasema alikuwa na mpango ampeleke huyo binti veta akasomee mambo ya mapambo na urembo ilinawe anasaidia kazi na mke wake (mama wa binti) ambaye ana saluni ya kike.
Wamepata taarifa kwamba huyo kijana anaendesha Balaji .

Sasa anajiuliza akubali hiyo posa au aikatae .

Jamaa yupo ana saluni ya kunyoa wanaume anaishi kwenye nyumba yake anawatoto wengine 3 wa mwisho anamiaka 3
 
Inasikitisha sana, hatakiwi kuwa dilemma. Ni kuamua tu kuwa binti yangu bado mdogo, ana malengo ya kusoma zaidi so kijana asubiri kwanza.

Hapo ni kucheza tu kamari, maana mabinti zetu nao wamekuwa chenga sana. Unampeleka shule anarudi na mimba.
 
Kama binti bado mdogo na hamjui jamaa akatae posa la sivyo ataishia kulea wajukuuu bila kupenda maana binti bado mdogo na hajui somo la ndoa na uaminifu. Leo anaolewa na dereva bajaji kesho atajitokeza mwenye hela zaidi ya bajaji akakarubuni ndoa chali
 
Sometimes vitu kama hivi vinanifanya ni question validity ya hekima ya hawa "wazazi".
Ni kitu cha ajabu mtoto awe wako mwenyewe, na awe mdogo and stil ushindwe kufanya maamuz kuhusu welfare yake.
Ingependeza kama hao watu wa posa wangekuja na viboko pia, ili ukishapokea posa wanakucharaza kwanza
 
Ni jamaa yako au ni wewe?
Be specific.
Ni jamaa yangu mimi mtoto wangu wa kwanza ana miaka 11 tena wa kiume nilichelewa kuzaa.
Kutokana na shule I am a seminarian nimesoma hadi philosophy pale salvatorian institute of philosophy and theology ndio nikaachana na seminary nikaenda udsm
 
yan anajua bintiye bado mdogo, ana mpango wa kumpeleka veta, binti anashangaa hao watu hawajui ila bado baba mtu anajiuliza akubali au akatae 😀😀😀😀 ni ajabu
Ni ajabu kidogo kwani hata hiyo posa yenyewe hata hataki watu wengi wafahamu .
Mimi binafsi jioni nikimaliza kazi zangu nitamtafuta nimwambie awarudishie jamaa laki yao.
Yaani seriously hako kabint bado kadogo
 
Ushauri unahitajika.

Kuna jamaa yangu aliwahi kuzaa anabinti mwezi wa 9 mwaka huu anafikisha miaka 18 huyo binti alimaliza form 4 mwaka 2024. Hakufaulu yupo nyumbani.

Sasa juzi kuna jamaa walikuja nyumbani kwake wakaleta post kwamba kuna kijana wao anataka kumuoa huyo binti wake wakaeleta posa pamoja na sh laki moja.

Sasa jamaa analalamika kwamba binti yake bado mdogo.

Hako kabinti mi mwenyewe nakafahamu bado kana akili za kitoto kabisa .

Jamaa kamuuliza binti yake kasema huyo mtu hamjui kameambiwa kuhusu kuolewa kenyewe kamaebaki kushangaa hakaelewi.

Sasa jamaa kapokea posa majibu hajawapa .

Sasa jamaa anasema alikuwa na mpango ampeleke huyo binti veta akasomee mambo ya mapambo na urembo ilinawe anasaidia kazi na mke wake (mama wa binti) ambaye ana saluni ya kike.
Wamepata taarifa kwamba huyo kijana anaendesha Balaji .

Sasa anajiuliza akubali hiyo posa au aikatae .

Jamaa yupo ana saluni ya kunyoa wanaume anaishi kwenye nyumba yake anawatoto wengine 3 wa mwisho anamiaka 3
Huyo binti ni wewe ?
 
Huyo binti ni wewe ?
Ninakaribia robo 3 ya umri wa huyo binti hapa JF kwa akaunti hii nina akaunti nyingini ina zaidi ya umri wa huyo mtoto hapa jf .
Hako kabinti hakana hata smartphone sizani hata kama kanafahamu kuna mtandao unaoitwa jamiiforums
 
Ni jamaa yangu mimi mtoto wangu wa kwanza ana miaka 11 tena wa kiume nilichelewa kuzaa.
Kutokana na shule I am a seminarian nimesoma hadi philosophy pale salvatorian institute of philosophy and theology ndio nikaachana na seminary nikaenda udsm
Kwanini uliachana na issue za kuja kuwa baba paroko mzee 🤔
 
Kwa ulimwengu wa sas ulivyo amuozeshe haraka sana uyo bint miaka 18 sio mdogo tena uyo

Akifanya masihara atazalia apo nyumbani na hakuna atakae muoa tena uyo bint yake.
 
Ni ajabu kidogo kwani hata hiyo posa yenyewe hata hataki watu wengi wafahamu .
Mimi binafsi jioni nikimaliza kazi zangu nitamtafuta nimwambie awarudishie jamaa laki yao.
Yaani seriously hako kabint bado kadogo
Chukua laki yako kanywe Bia
 
Back
Top Bottom