Ushauri please

Ushauri please

Rosely

Member
Joined
Sep 28, 2013
Posts
7
Reaction score
1
Nina watoto wawili yani twins wana 2 years sasa,baba yao kakataa kunisaidia kulea.naomben mnishaur nimfanyeje ili awajal
 
Dah napenda twins sana naomba nipe mimi tafadhali
 
Nina watoto wawili yani twins wana 2 years sasa,baba yao kakataa kunisaidia kulea.naomben mnishaur nimfanyeje ili awajal

Nenda Ustawi wa Jamii au kwa Mama Bisimba (Dr es Salaam) au tafuta wanasheria wa kile Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania.

Kote huko utapata msaada wa kisheria, kwa sheria ya Tanzania wanao wanapaswa wapewe matunzo na mzazi wa kiume hadi wanapofikisha miaka 12 (kama sijakosea).
 
Nataman sana lakini kwa huku kijijini sijui hata nianzie wapi kupata huo msaada
 
Mkuu mleta mada ikiwa kama huyo mzazi mwenzio kipindi chote hicho cha ujauzito jamaa mlikuwa pamoja kwa maana ya kusaidia lakini mara tu ulipojifungua watoto mapacha akaacha kutoa huduma na humsingizii(kumbambikizia) hao Mimi siko mbali na wenzangu waliosema uende Ustawi wa Jamii kumshtaki huyo mwenzio.

Mpaka umekuja hapa jf ni wazi utakuwa umejaribu kumsihi bila muafaka kufikiwa vema pia kuwalea hao watoto wawili lazima bila kuwa na msaada wa mwenzio ni ngumu sana. Nenda nilipokushauri halafu rudi hapa jf kwa mrejesho wa utakachoambiwa kule na wataalam wetu.
 
Nina watoto wawili yani twins wana 2 years sasa,baba yao kakataa kunisaidia kulea.naomben mnishaur nimfanyeje ili awajal

Kwani huna kabisa uwezo wa kuwalea dia? Maana najua ukishaanza sekeseke la kesi utafanya ishu iwe ngum zaidi. Kwa sasa walee tu mwenyewe, baba atapata tu akili baadae aje...
 
Kesi zinahitaji muda na pesa. Kama unayaweza hayo yote just do it. Lasivyo komaa na hao wanao au wawekee hatimiliki kwamba baba yao haruhusiwi kuwasogelea maisha yake yote.

Sent from my Nokia Lumia using Tapatalk
 
Kama una uwezo wa kuwatunza lea mwenyewe wanao, maana hata ukimpeleka usawi wa jamii kama hawajali haitosaidia ingawa atawajibika kifedha tu, ila kihisia kuwepo na kuwajali wanae hakutokuwepo
 
uwezo mdogo sana kwani sina kazi kwani nilipata mimba nikiwa chuo cha ualim na sikuweza kuendelea

Pole sana mamii... kama wewe ni muumini mi nakushauri usali zaidi. Mwenyezi Mungu aliwaleta viumbe hao wazuri duniani kwa mpango mwema na hakika hatawaacha waadhirike.
Tumia tu lugha ya upole na unyenyekevu kumkumbusha baba yao juu ya jukumu lake kushiriki malezi ya wanae. Inawezekana ni umri unamsumbua, lakini hata mapepo. Pengine Mwenyezi Mungu anataka kukutumia wewe umuombee ili ambadilishe. Na pengine Mwenyezi Mungu ataitumia sauti yako kumfikishia ujumbe. Sauti ya Mungu ni sauti ya upole.
Siku ukijisikia kuongea nae kwa upole, jua ni sauti ya Mungu, lakini siku ukigombana nae au kumfokea, jua ni vishawishi vya shetani.
Wapende wanao na mpende baba yao. Hao watoto ni baraka za Mungu, na siku zote Mungu ni UPENDO, sio kesi wala magomvi, sio uchawi wala masengenyo.
 
Kua kijijini haijalishi fika mahakama ya mwanzo eleza tatzo hlo utapewa muongozo from there,but baba watoto atawajibika financially sana sana!
 
ww anatingisha huyo walee mbona atakuja muda si mrefu
 
Aisee wanaume wengine ka wachawi!
Twins jamani dah na me nnavyopenda hmm.
Nenda kamshtaki kama ulivoshauriwa hapo juu
 
Nina watoto wawili yani twins wana 2 years sasa,baba yao kakataa kunisaidia kulea.naomben mnishaur nimfanyeje ili awajal

nini kimetokea hadi afikia kukataa kulea watoto wake...??? Ili ushauriwe vizuri, toa sababu unayodhani imemfanya awe hivyo
 
Aisee wanaume wengine ka wachawi!
Twins jamani dah na me nnavyopenda hmm.
Nenda kamshtaki kama ulivoshauriwa hapo juu
kuendesha maisha kwa kesi kunapoteza muda wa kufanya mengine.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom