USHAURI: Nini cha kufanya baada ya kutoka kazini?

USHAURI: Nini cha kufanya baada ya kutoka kazini?

Mzillar

Member
Joined
Jan 4, 2018
Posts
34
Reaction score
40
Habari wakuu,

Kichwa chajieleza hapo juu,

Mimi ni mfanyakazi wa kampuni nimeajiriwa miezi 6 ilopita, kutokana na ugeni wa eneo ninaloishi hua nikitoka kazini nakua nipo tuu sina cha kufanya home.

Nilikua naomba ushauri naweza kujifunza fani gani au kujishughulisha na biashara gani niendelee kua bize na kujiongezea kipato.

Karibuni kwa mawazo ya hekima
 
Kama unakamtaji, jaribu kufungua kaPUB ili jioni ukitoka job unafungua hapo unakomaa mwenyewe na madada kama wawili watatu wenye mvuto hivi na kuwe na kamziki kazuri..

Tafuta toyota Hiace kama uko dar, asubuhi ukienda job unaenda nayo ukitoka unakomaa jioni ile na trip za mbagala au mbezi mpaka sasa sita usiku tayari hesabu 50000/ imeshapatikana na mafuta juu na poshi umeshajilipa hapo..

NB: USIKIMBILIE KUOA..
 
Tafuta eneo lenye chanzo cha maji, nunua pump yako na mpira, anzisha kilimo cha mbogamboga.. lima eneo kama nusua eka tu kwa kuanzia..lima chunese, michicha, sukuma wiki, mnavu, carotte, hoho, nyanya kiasi na pilipili mbuzi..uwe na kijana wako mmoja tu. Unaenda sokoni unachukua order za wamama wale wauza mboga wanakuwa wanakuja kununua kwako. Trust me, hadi ualize kunyeshea nusua eka jioni muda nao utakuwa umesogea.. hapo utashangaa mwenyewe utakavyoingiza kipato cha ziada. hapo masuala ya vyeti vyako vya degree weka pembeni.. ni kazi ya mikono na pia ni zoezi.. huna haja ya kwenda kupotezea nguvu zako gym..unafanya zoezi hapo hapo unatengeneza kipato.
 
Kama ni Ngara fuata ushauri wa mdau hapo juu, shamba na ufugaji
 
Jiendeleze, ingia Youtube tafuta tutorial za English, fani yako, business writing, excel, lugha nyingine kama Kifaransa etc.
 
Kama unakamtaji, jaribu kufungua kaPUB ili jioni ukitoka job unafungua hapo unakomaa mwenyewe na madada kama wawili watatu wenye mvuto hivi na kuwe na kamziki kazuri..

Tafuta toyota Hiace kama uko dar, asubuhi ukienda job unaenda nayo ukitoka unakomaa jioni ile na trip za mbagala au mbezi mpaka sasa sita usiku tayari hesabu 50000/ imeshapatikana na mafuta juu na poshi umeshajilipa hapo..

NB: USIKIMBILIE KUOA..
Wazo zuri sana. Hivyo ndo vinalipa angalau kidogo kwa sasa.
 
Habari wakuu,

Kichwa chajieleza hapo juu,

Mimi ni mfanyakazi wa kampuni nimeajiriwa miezi 6 ilopita, kutokana na ugeni wa eneo ninaloishi hua nikitoka kazini nakua nipo tuu sina cha kufanya home.

Nilikua naomba ushauri naweza kujifunza fani gani au kujishughulisha na biashara gani niendelee kua bize na kujiongezea kipato.

Karibuni kwa mawazo ya hekima
Fanya mazoezi ya viungo. Unaweza kutembea, kukimbia au kucheza mpira. That will make you physically heath.
 
Back
Top Bottom