Ushauri: Nimeitwa Polisi

Palestina Fc

Member
Joined
Jul 14, 2019
Posts
45
Reaction score
65
Habari wakuu

Nimepokea simu kutoka kwa mtu anasema yuko central kitengo cha cyber na kuna namba inaonekana naongea nayo na wanataka kujua machache kuihusu
Nimewauliza ni ipi niwajibu? wamekataa wamesema niende central au niwaambie nilipo wanifate nimewajibu ntaenda kesho

Hasa hapa najiuliza niende au? maana polisi wetu hawaaminiki unaeza fika yakawa mengine

Ushauri


Sent using Jamii Forums mobile app


 
Kuna jambazi/mhalifu unawasiliana naye au mtu wako wa karibu?

Aliyekuita alijitambulisha vipi na wewe unamwamini vipi kuwa ni polisi na si tapeli au mwenye nia mbaya na wewe?

Kama upo ok chukua mtu wa kukusindikiza ambaye atakuwa nawe in case of anything. Ili ukatoe ushirikiano kwa kile unachokifahamu.chukua jina la askari husika na namba yake. Nenda kituoni uliza kama kuna mtu mwenye jina na namba hiyo.then waambie amekuita kwa simu unataka onana naye ukiwa na mtu amekusindikiza na umeoa taarifa kwa watu wa karibu.

Then waoneshe ushirikiano.

Kama unatembea na mke wa mtu na chats zenu zimeonekana ni issue ujue. Ombea mwenye mke asiwe karibu akakuona na jinsi ulivyokuwa ukitamba kwenye chats kwa kumkunja mkewe pasipo huruma.
 
Me mwananchi wa kawaida sina hata level ya kuwa na mwanasheria

Sent using Jamii Forums mobile app
Kuna wanasheria wanatia ushauri "pro bono", kuna vikundi vya NGO vya kusaidia watu wasio na wanasheria.

Kifupi tafuta ushauri wa kisheria kabla ya kwenda polisi, ukiweza nenda na mwanasheria.

Ukienda bika mwanasheria polisi wataku abuse sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Polisi usiende kama unaenda bar! Unaweza fika pale ukaambiwa vua viatu, vua mkanda, toa ulivyonavyo weka ubaoni alafu ukasikia mweke selo namba 4 ya majambazi huyo mpelelezi wa kesi yake ana udhuru mpaka week ijayo..mjomba fuata ushauri wa Gudume.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…