Nothing4good
Senior Member
- Feb 19, 2011
- 180
- 55
Tumpe ushauri huyu dada.
Ndoa yangu ina miaka 7 ila uhusiano wetu una miaka11. Nina watoto 2 na sasa ni mama kijacho. Mwaka Jana mwishoni nilipata kuwashwa ukeni nikaenda kupima nikaambiwa nina ugonjwa wa zinaa, nikatibiwa na nikaambiwa na mume wangu akatibiwe, nikamwambia hali halisi, akakataa akidai hajisikii chochote hivyo hawezi kupima, nikamlazimisha sana akakubali kupima akapatiwa dawa. Tangia nikutane na mume wangu sijawahi kuchepuka.
Nikamuuliza mwenzangu ananisaliti? Akakataa katakata hajawahi kunisaliti akadai labda maji wanayoogea huko kazini kwao (yeye yupo mkoa mwingine ni kweli wanatumia maji ya visima) mimi kwa kweli sikurizika na majibu yake nikaanza kufanya uchunguzi wangu nikagundua alikuwa na wanawake 3 ila mmoja wao ameachana naye tena kwa ugomvi mkubwa mpaka amemblock kwani ndiye aliyemuambukiza wale wengine 2 bado alikuwa anaendelea nao.
Nilimuuliza tena akakataa nilipomuonyesha vithibiti vya Picha, SMS, na majina yao akakubali na kuomba msamaha huku akilia na Magoti kapiga, sikumjibu chochote nilikaa tu kimya, aliomba ruhusa kazini wiki mzima akawa tu anaomba msamaha nilimsamehe ila nilipanga kutengana naye kwa mda, na nilikuwa naenda kwetu kulikuwa na sherehe hivyo niliwaza nikienda sitarudi kwake.
Kama alilijua hilo naye akataka tuongozane kwenda harusini hivyo nikawa sina jinsi zaidi ya kwenda na kurudi pamoja. Kipindi chote hicho hatukuwahi kufanya mapenzi mpaka mwaka huu mwanzoni aliponiambia kama nimemsamehe kweli tufanye tendo la ndoa kweli nikamkubalia ila kwa kinga cha ajabu mwezi 2 sikuziona siku zangu nikafanya kipimo nikajikuta nina mimba.
Nikamuuliza umenifanyia makusudi hivyo kwanini? Akadai eti alijua tu asiponifanyia hivyo nitamuacha hivyo anaomba nimsamehe sana. Nikawa sina jinsi ndio hivyo. Sasa hivi juzi nikakagua simu yake nikagundua anamtoto wa miaka 8 anamsomesha na wazazi wake wanajua kwani nimeona kuna mpango wa kumpeleka boarding au aje kwa baba yake kwani mazingira ya kwa mama yake, mtoto hayataki.
Sasa kama nimefichwa hata na hili wananitakia mema kweli?
Ndoa yangu ina miaka 7 ila uhusiano wetu una miaka11. Nina watoto 2 na sasa ni mama kijacho. Mwaka Jana mwishoni nilipata kuwashwa ukeni nikaenda kupima nikaambiwa nina ugonjwa wa zinaa, nikatibiwa na nikaambiwa na mume wangu akatibiwe, nikamwambia hali halisi, akakataa akidai hajisikii chochote hivyo hawezi kupima, nikamlazimisha sana akakubali kupima akapatiwa dawa. Tangia nikutane na mume wangu sijawahi kuchepuka.
Nikamuuliza mwenzangu ananisaliti? Akakataa katakata hajawahi kunisaliti akadai labda maji wanayoogea huko kazini kwao (yeye yupo mkoa mwingine ni kweli wanatumia maji ya visima) mimi kwa kweli sikurizika na majibu yake nikaanza kufanya uchunguzi wangu nikagundua alikuwa na wanawake 3 ila mmoja wao ameachana naye tena kwa ugomvi mkubwa mpaka amemblock kwani ndiye aliyemuambukiza wale wengine 2 bado alikuwa anaendelea nao.
Nilimuuliza tena akakataa nilipomuonyesha vithibiti vya Picha, SMS, na majina yao akakubali na kuomba msamaha huku akilia na Magoti kapiga, sikumjibu chochote nilikaa tu kimya, aliomba ruhusa kazini wiki mzima akawa tu anaomba msamaha nilimsamehe ila nilipanga kutengana naye kwa mda, na nilikuwa naenda kwetu kulikuwa na sherehe hivyo niliwaza nikienda sitarudi kwake.
Kama alilijua hilo naye akataka tuongozane kwenda harusini hivyo nikawa sina jinsi zaidi ya kwenda na kurudi pamoja. Kipindi chote hicho hatukuwahi kufanya mapenzi mpaka mwaka huu mwanzoni aliponiambia kama nimemsamehe kweli tufanye tendo la ndoa kweli nikamkubalia ila kwa kinga cha ajabu mwezi 2 sikuziona siku zangu nikafanya kipimo nikajikuta nina mimba.
Nikamuuliza umenifanyia makusudi hivyo kwanini? Akadai eti alijua tu asiponifanyia hivyo nitamuacha hivyo anaomba nimsamehe sana. Nikawa sina jinsi ndio hivyo. Sasa hivi juzi nikakagua simu yake nikagundua anamtoto wa miaka 8 anamsomesha na wazazi wake wanajua kwani nimeona kuna mpango wa kumpeleka boarding au aje kwa baba yake kwani mazingira ya kwa mama yake, mtoto hayataki.
Sasa kama nimefichwa hata na hili wananitakia mema kweli?