Ushauri: Mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu itolewe na taasisi za fedha (Benki)

Kididimo

JF-Expert Member
Sep 20, 2016
3,791
3,360
Kwa utamaduni tulivyozoea neno "mkopo"humaanisha deni lililowekewa utaratibu wa kulilipa. Vilevile,ili mkopo uweze kutolewa,lazima mkopeshaji ajiridhishe kuwa mkopaji anao uwezo wa kurudisha kwa kuangalia mazingira,uwezo na aina ya udhamini. Taasisi za kifedha kama benki zinao uwezo mkubwa wa kufanya kazi hii,na zimefanya hivyo kwa maelfu kama sio malaki ya wananchi kama wajasiriamali wadogo,wa kati na hata wakubwa. Muhitaji huchukua mkopo pale anapoona ni lazima kama mtaji wa msingi au kuongezea alionao.

Kwa upande wa Mikopo ya Elimu ya juu,taasisi za kifedha chini ya mikataba maalumu, nashauri kutoa mikopo hii kwa wanafunzi wetu huku bodi ya mikopo ikiwa kama mratibu na serikali pamoja na wazazi au itakavyoonekana inafaa wakawa wadhamini. Nashauri hivi kwa vile sio rahisi bodi ya mikopo ikajua mazingira ya kiuchumi ya wanafunzi na wazazi wao kwa nchi nzima kwa kuangalia taarifa walizopelekewa bila kutokea dosari au udanganyifu. Nia ya serikali ni njema kuwa na bodi ya mikopo lakini haina wawakilishi maeneo yote nchini kuhakiki taarifa hizo kwa usahihi. Ni ukweli kuwa taasisi za kifedha kama benki ya NMB iko kila kona ya nchi hii na kama taasisi ya kifedha yenye uzoefu na utoaji mikopo, ikitumika kwa kushirikiana na Bodi ya mikopo au itakavyoonekana inafaa,kazi hii inaweza kuwa rahisi zaidi. Mfano, continuing students watakaokosa mikopo,na wanatoka familia masikini,wangeweza kudhaminiwa na serikali katika mpango maalumu kupitia taasisi hizi wakamalizia masomo yao.
Haya ni maoni yangu kwa lengo la kuboresha zoezi hili .
 
Ngoja niwaharibie siku....

MSAKO WA WADAIWA SUGU KUANZA KARIBUNI

Bodi ya Mikopo itatangaza majina ya wadaiwa sugu kuanzia mwaka 1994 ambao madeni yao yameiva.

Majina ya Wadaiwa sugu yatawekwa hadharani tarehe 13 Novemba, 2016. Wasugu hao watapewa siku 30 kulipa madeni yao. Baada ya muda huo, hatua za kisheria zitachukuliwa na wahusika watalipia gharama za kuwasaka.

Kwa mawasiliano zaidi piga 0763 459165 au 0767 513208

Imetolewa na:
MKURUGENZI MTENDAJI
BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU
 
Benki unakopa milioni 2-3 kwa dhaman ya nyumba ya milioni 40 , ukichelewa marejesho kadhaa wanataka kuuza nyumba ya milioni 40 kwasababu ya m 2-3 bank bado sana Tanzania..
 
Ngoja niwaharibie siku....

MSAKO WA WADAIWA SUGU KUANZA KARIBUNI

Bodi ya Mikopo itatangaza majina ya wadaiwa sugu kuanzia mwaka 1994 ambao madeni yao yameiva.

Majina ya Wadaiwa sugu yatawekwa hadharani tarehe 13 Novemba, 2016. Wasugu hao watapewa siku 30 kulipa madeni yao. Baada ya muda huo, hatua za kisheria zitachukuliwa na wahusika watalipia gharama za kuwasaka.

Kwa mawasiliano zaidi piga 0763 459165 au 0767 513208

Imetolewa na:
MKURUGENZI MTENDAJI
BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU
Haloo haloo, yametimia sasa (sijawahi kupenda taarabu japo....).
Hivi kama kuna mtu alikopa alafu unamkuta hana hata uhakika wa mlo mmoja kisha unamkamata na kumpeleka Kalanga au Butimba na kuanza kumhudumia kwa pesa za serikali kwenye chakula na ulinzi ...unarudisha mkopo au unauongeza!?
....au, mwingine alimaliza akakosa kazi na kuvuka mpaka mpaka Zambia, Kenya, UAE, USA nk na kupata kazi nzuri tu. Sasa hajalipa na bodi ya mikopo inabahatika kumjua alipo then wanatumia million 10 kumfuatilia huko kumdai million 5!
Mambo yetu mengi hayajakaa sawa na hata wachache wanaotaka kuyaweka sawa bila hata malipo wanazuliwa. Sio ajabu hata remittance za diaspora ni kiduchu ukilinganisha na nchi kama Zambia yenye watu 15m au Kenya na Uganda!
 
Benki unakopa milioni 2-3 kwa dhaman ya nyumba ya milioni 40 , ukichelewa marejesho kadhaa wanataka kuuza nyumba ya milioni 40 kwasababu ya m 2-3 bank bado sana Tanzania..
Maana yangu ni kuwa,kuwe na mpango maalumu wa kushirikisha benki. Sijamaanisha mikopo hii ifananae na ile ya nyumba au biashara yenye riba kubwa. Nimefuatilia kwa karibu aina ya watu wanaoajiriwa na bodi ya mikopo, idadi na uwezo wao na mfumo unaotumika kutoa na kudai mikopo hii nikagundua something must be changed! Pia ijulikane kuwa sio wote wanaoitwa watoto wa yatima wanataka kukopeshwa! na nina mifano. Ikiwa suala la mikopo litakabidhiwa benki,utakuta kuna wazazi wata-opt kutokopa na kutumia rasilimali walizonazo (ambazo bodi ya mikopo haina uwezo wa kuziona) wakalipia pesa taslimu. Juzi niliongea na mzazi mmoja kaniambia kijana wake kachaguliwa kwenda Mzumbe,na hana Mkopo. Nilipomwuliza utafanyaje,akaniambia ni rahisi sana ninaenda kuuza maksai wangu wawili,nalipa tuition fee ya mwaka (1.5 m) na fedha ya kujikimu na malazi tutampatia kwa awamu.( Kama ana maksai 6) kijana wake atakamilisha miaka 3 na kugraduate. Hoja yangu ni kuwa kwa kutumia benki, serikali itapunguza gharama zisizo za lazima na pia itakuwa overseer mzuri na sio direct actor na kupata fursa zaidi ya kushughulikia changamoto zinazojitokeza
 
Benki unakopa milioni 2-3 kwa dhaman ya nyumba ya milioni 40 , ukichelewa marejesho kadhaa wanataka kuuza nyumba ya milioni 40 kwasababu ya m 2-3 bank bado sana Tanzania..

Hulazimishwi kukopa. Kama unaona uwezo wa kulipa huko mbele ni mgogoro achana na mpango huo.

Lakini hii ni better option. Commercial banks zingeweza kukopesha wanafunzi. Malalamiko yangepungua sana.
 
Hulazimishwi kukopa. Kama unaona uwezo wa kulipa huko mbele ni mgogoro achana na mpango huo.

Lakini hii ni better option. Commercial banks zingeweza kukopesha wanafunzi. Malalamiko yangepungua sana.
Ni kweli.
 
Bank ya biashara wanakukopesha mwezi huu mwezi ujao uanze rejesho ni bank gani mkuu itataka itoe fedha marejesho yawe baada ya miaka minne au saba kwa course zingine au unamaanisha nini? sijui labda sijakuelewa unamaanisha nini..?
 
Hapo ni kutengeneza tatizo kubwa kuliko hili la sasa. Niliwahi kusema na narudia tunachambua mchele kwenye chuya badala ya chuya kwenye mchele.
Hivi ni watanzania wangapi wanauwezo wakusomesha watoto wao vyuo vikuu? Ukweli ni kuwa ni wachache sana wanauwezo huo.
Solution ya hili tatizo ni moja tu, Kila mwanafunzi alopata nafasi ya kujiunga na elimu ya juu apate mkopo, basi na hakuna namna nyingine.

Ulisema utumie vigezo ni kutaka kudhulumu wengi haki zao. Kusoma private inaonekana ni utajiri wakati sio. Vijana wengine walifaulu vizuri na hawakupangwa serikalini, wengine walisomeshwa na taasisi za dini, wengine walijisomesha wenyewe, wengine kwa michango ya ndugu, wengine kwa wazazi kuu za kila kitu na wengi wao wameacha madeni walikokuwa wanasoma.

Ishu ya kuwa na wazazi wote sio hoja pia. Kuna watu Wana wazazi wote lakini ni maskini sana na wengine hata milo inawashinda wakati inawezekana Kuna yatima lakini mwenye Mali zaidi kuliko yule mwenye wazazi wote.
Kwakifupi ni kuwa hivi vigezo havitekelezeki hapa Tanzania.

Benki ndio zitafanya Hali kuwa ngumu zaidi. Watataka udhamini kutoka kwa mzazi, wazazi Watatoa wapi mali hizo? Je kwa Hali ajira ya leo unataka mali za wadhamini (kama watapatikana) ziuzwe zote?

Mikopo iwe haki ya kila mwanafunzi then tuweke juhudi kwenye kurudisha Mikopo ilotolewa mwanzo.
 
Hapo ni kutengeneza tatizo kubwa kuliko hili la sasa. Niliwahi kusema na narudia tunachambua mchele kwenye chuya badala ya chuya kwenye mchele.
Hivi ni watanzania wangapi wanauwezo wakusomesha watoto wao vyuo vikuu? Ukweli ni kuwa ni wachache sana wanauwezo huo.
Solution ya hili tatizo ni moja tu, Kila mwanafunzi alopata nafasi ya kujiunga na elimu ya juu apate mkopo, basi na hakuna namna nyingine.

Ulisema utumie vigezo ni kutaka kudhulumu wengi haki zao. Kusoma private inaonekana ni utajiri wakati sio. Vijana wengine walifaulu vizuri na hawakupangwa serikalini, wengine walisomeshwa na taasisi za dini, wengine walijisomesha wenyewe, wengine kwa michango ya ndugu, wengine kwa wazazi kuu za kila kitu na wengi wao wameacha madeni walikokuwa wanasoma.

Ishu ya kuwa na wazazi wote sio hoja pia. Kuna watu Wana wazazi wote lakini ni maskini sana na wengine hata milo inawashinda wakati inawezekana Kuna yatima lakini mwenye Mali zaidi kuliko yule mwenye wazazi wote.
Kwakifupi ni kuwa hivi vigezo havitekelezeki hapa Tanzania.

Benki ndio zitafanya Hali kuwa ngumu zaidi. Watataka udhamini kutoka kwa mzazi, wazazi Watatoa wapi mali hizo? Je kwa Hali ajira ya leo unataka mali za wadhamini (kama watapatikana) ziuzwe zote?

Mikopo iwe haki ya kila mwanafunzi then tuweke juhudi kwenye kurudisha Mikopo ilotolewa mwanzo.
Nimekuelewa na una hoja za msingi. Ila kumbuka zama zimebadilika,serikali haiajiri kila mhitimu wa chuo kikuu! Ina vipaumbele (priorities) na wameshataja. Na ujue kuna idadi kubwa ya wanafunzi walio vyuoni hawako kwenye kozi za vipaumbele. Wazazi wengi wanajua wote ni sawa na wanapaswa kupata mikopo kama maoni yako yanavyolenga. Pia ujue kuna walioko kozi za vipaumbele wamekosa kwa kukosa vigezo ulivyotaja vya uwezo wa kifamilia. Swali ni kuwa,nani kapita katika familia hizo kuhakiki vigezo hivyo? Bodi ya mikopo ina uwezo kiasi gani kufikia familia hizo? Je kama serikali ingeshirikisha taasisi za fedha zilizo karibu zaidi na wahitaji kwa utaratibu (maalumu) ufanisi usingeongezeka? Issue ya kuwa fedha ya benki itakaa miaka 3 sio nyeti! Kuna watu wana mikopo ya hadi miaka 20 ndo wakamilishe. Na ukumbuke,anaelipa sio mzazi ni mhitimu! Mzazi au serikali ni wadhamini kwa upande mwingine. Mhitimu anapojua anadaiwa hatafanya uzembe! Fursa zipo,na kwa vile tayari ni msomi,naamini atazichangamkia alipe deni
 
Tayari kumeshajitokeza majina hewa kwenye list ya wadaiwa sugu! Kama ingekuwa benki,hali hii isingejitokeza,urejeshaji usingesubiri miaka 10 hadi vielelezo kughushiwa
 
Back
Top Bottom