Ushauri: Mchepuko una mimba yangu

Ushauri: Mchepuko una mimba yangu

sitaki raha

Senior Member
Joined
Jun 8, 2016
Posts
127
Reaction score
112
Naomba msaaada kwa hili.

Mimi nina mke wangu ambae yupo mbali alikuwa mama wa nyumbani nikamfanyia mpago wa chuo amesoma amefanikiwa kupata kazi mkoani mimi sasa wakati yuko chuo nilikuwa na mchepuko wangu si unajua huyu ulinipokea nilipopewa uhamisho toka Dar kwenda eneo jipya la kazi.

Mchepuko wangu ulijua mimi sina mke wakati family yangu ilikuwa Dar baada ya muda mke wangu alikuja kukaa na mimi mwaka 1, nikaona nimpeleke chuo hakuna aliyejua kwamba mke wangu yuko wapi maana alinichia mtoto mdogo, majirani wakaanza kusema nimemfukuza mke wangu wala sikujali hilo.

Sasa kipindi hicho yule mchepuko nilikuwa nimeachana nao sasa baada ya kusikia nimeachana na mke wangu ukarudi kwa kasi sana nami nikaendelea nao kumbe sikujua nafanya kosa ukaanza kusema nimuoe nikajitambulishe kwao mwanangu anafahamu?

Sasa mchepuko una mimba daah! Hili balaa na mke wangu anakuja mwezi ujao na mchepuko unalazimisha niende kwao na mke wangu napenda sana kutoa mimba haiwezekani ila mimi nimemwambia nipo tayari kutoa huduma zote nimnunulie kiwanja hataki anataka kuolewa tu hajui kama nipo na mke wangu.

Nifanyeje wandugu?
 
Ulitakiwa uje tukushauri tangu mwanzo kabla hujatenda..now u hv to face tht haipukiki.....
 
Yani ww huitaji hata ushauri maana jina lako lenyewe tu linasadiki matendo yako..!
 
...mchepuko una mimba daaaaah hili balaaaa na mke wng anakuja mwezi ujao na mchepuko unalazimisha niende kwao na mke wng napenda sanaaa ?

Uko serious unampenda mke wako sanaaaa au umeamua tu kujitoaufaham, ungempenda mkeo ungealika mchepuko uje ukae nao tena bila aibu unaishi na mwanao. Hamna namna, inabidi ulipie gharama ya maamuzi yako mkuu, kiufupi unaupenda huo mchepuko kuliko mkeo.
 
eti unampenda mkeo huu unafiki una mwisho
....utavuna ulichopanda wakati unazini mbona hukuomba ushaur...
sikupi ushaur ng'oo
 
Upuuz uufanye mwenyewe uje unatetemeka saiz unatuandikia visivyoelewka .Tuma haya maombi yako upya watu wakuelewe maana naona Unatujaribu na sisi Hatujaribiwi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom