Ushauri kwa vijana

Ushauri kwa vijana

Joined
Nov 22, 2017
Posts
22
Reaction score
11
*NUKUU YA USIKU WA LEO.*


Unayopitia leo katika maisha yako ni matokeo ya ulichokifanya Jana! utakachokifanya Leo ndiyo kitakacholeta matokeo kesho!.

Usitegemee kuacha kusoma ukafaulu, hata ukiangalizia kwenye mtihani ukapata *"A"* bado kazi za hiyo A hutaweza kuzifanya na kazi itakushinda ukifika kazini sababu ulifaulu kwa kuibia, hukusoma, hukuelekezwa,hujui!.

*USHAURI*
Tengeneza maisha yako ingali bado una unguvu, fanya maamuzi yenye manufaa ingali bado una uwezo wa kufikiri, chagua marafiki wanaokuzunguka kulingana na ndoto zako za maisha.

_*Usipofanya maamuzi mazuri Sasa ingali bado kijana na kuchukua hatua, utawachukia vijana wenzio waliofanikiwa mkifika uzeeni sababu ya wivu na hasira ya ugumu wa maisha wakati wote mlikuwa vijana wenye nguvu kipindi cha kupanda mbegu.*_

Muwe na usiku mwema.
 
Tunashukuru mzee!!,ila tunapenda sana kutengeneza maisha tungali vijana ,tunapenda sana ,

Mtihani ni tunaazia wapi? Tukipata pakuazia sisi hatuna shida kabisa
 
Utakapoketi uzeeni ndio pataakisi ulipoketi Ujanani.
 
Back
Top Bottom