Ushauri kwa Sam Mahela, Mtangazaji wa ITV

Ushauri kwa Sam Mahela, Mtangazaji wa ITV

zamlock

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2010
Posts
3,840
Reaction score
660
Ushauri wangu kwa Sam Mahela ni huu hapa;

Kulingana na mambo muhimu ya utoaji wa habari zilizogusa hisia za watu kwa mwaka 2014, tunakuomba ugombee tuzo za mwaka huu, kwa sababu kuna mambo muhimu ya kijamii tisa uliyopambana na habari zikaweza kuifikia jamii na watu wakaguswa na habari zako na ikapelekea hao watu kusaidiwa.

1) Ulifuatilia swala la Bi Salome Mhando, mkazi wa Mabwepande ambaye alitelekzwa na mumewe bwana Ally Nasoro kwa madai ya mkewe kuzaa kupita kiasi, na leo hii yule mama kapata msaada mkubwa mpaka wa kujengewa nyumba na pesa taslimu milioni mbili.

2) Uliweza saidia kufanyika jitihada za kijana wetu, marehemu Sande Mrema, ambaye alikuwa na uzito mkubwa zaidi ya kilo 250 kutaka kusafirishwa, ingawa ilishindikana, lakini kikubwa ulichokifanya ni jitihada zako za kuisaidia ile familia na kupata pesa zao kiasi cha dola 13,802.

3) Alifuatilia sakata la mwanafunzi wa darasa la saba wa kike aliyefungiwa ndani na mwanaume katika eneo la Kinondoni na kumbaka mwanafunzi huyo na kusababisha mwanafunzi huyo kutokufanya mtihani wake wa siku ya pili wa kumaliza darasa la saba mwaka jana, na kubwa zaidi ni mtuhumiwa kupelekwa mahakamani.

4) Swala lingine kubwa ni jitihada zako ulizozifanya kwa kuibua ile habari ya yule kijana aliyekuwa amemfungia kikongwe ndani maeneo ya Manzese zaidi ya miaka 20, ilisemekana kikongwe yule alifariki kumbe alikuwa amewekwa ndani na mtoto wake wa kuzaa, ni habari ambayo iligusa hisia za watu.

5) Ulimsaidia yule mtoto aliyepelekwa India kutibiwa baada ya kunywa kemikali akidhania ni maji na kuharibu mfumo wake wa kuharibu chakula na huyo mtoto saa hizi anaendelea vizuri.

6) Ulimsaidia yule mama aliyekuwa amevimba miguu kwa zaidi ya miaka 15 na yule mama alikuwa na hali mbaya sana, nakumbuka wakati unarusha habari yake inasemekana na harufu alikuwa anatoa mbaya sana, lakini hukujali uliweza mpaka kumshika na kumpa msaada zaidi wa kuhakikisha anakwenda kutibiwa India na jitihada ulizozifanya ni kuchangisha fedha kwa ajili ya matibabu yake mimi mwenyewe nilichanga.

7) Ulifuatilia swala la wanafunzi kuoana wao kwa wao maeneo ya Rorya, Sengerema, Kahama tena ni shule za serikali. Uchafu huo unafanyika kwa sababu ya wanafunzi kukosa mabweni ya kulala matokeo yake watoto huteseka mpaka kufikia hatua hiyo.

8) Pia uliibua habari ya mzee Issa, yule wa Mabibo kufungiwa ndani na watoto wake na mkewe bila msaada, na mzee huyu nakumbuka ile habari alikuwa akijinyea, ulionyesha uvumilivu ukaingia ndani na kujifungia na kumsafisha na kuokoa maisha yake, ni jambo la kupongezwa sana.

WanaJF, ni habari amabazo nimezifuatilia kwa kina na ziko zingine youtube, mnaweza mkaona siyo vitu vya kubuni na ndiyo maana nimeona nimpe ushauri huyu kijana atumie habari hizi kugombea tuzo mwaka huu, kama utabahitika kusoma habari hii ifanyie kazi na usichoke.
 
Huyu kijana anaitaji pongezi sana na ushauri uliyompatia ajitahidi afanye hivyo kwa kweli habari zake zimegusa hisia za watanzania walio wengi habar ya kina yule aliyekuwa na uzito mkubwa iliniumiza sana baada ya kusikia amefariki kwa mashirika ya ndege kutokumbeba kwenda india kwenye matibabu
 
Umeongea point kabisa mkuu itabid afanye hivyo
 
Sam anajitahidi mno,hasubiri press conference akaripoti.

Pasco
 
Last edited by a moderator:
ni kweli kijana huyu ni amkini sana kwenye uandishi wa habari hswa ktk kile kipindi chake cha dk45
 
SAM MAHELA SALAMA? yaani. Hivi ni mtu gani atakaefuatilia habari zako na kuwa na details kiasi hiki. Anyway kwenye marketing inaruhusiwa ila du kama inakupima na reasoning yako vile.
 
Ila ile nyumba yule mama aliyetelekezwa na mumewe aliyopewa na COVENANT BANK haifiki 25mil kama mlivosema ile ni fix tupu, thamani yake hawezi kuzidi 8 Mil like,ila big up unafanya kazi kwa bidii
 
Pamoja na huyo, mwanamama Hoyce Temu wa Channel Ten naye anajitahidi sana kuibua matatizo na kisaidia kuyapatiaufumbuzi ndani ya jamii...

Tafakari...
 
Huu uzi wa mahela hajui km kuna uzi km huu, nakwanini ajidhalilishe kwa kujipigia debe kwa stail hii? Kuna watu wanafiatilia sana habari zake, na wanakumbukumbu nzuri, hivyo tumpongeze. Pia vp yule binti aliyezaa na mhindi kisha wakwe zake, yani wahindi wakamuiba mtoto ,iliishia vp?
 
swali: hivi habari huwa anatafuta sam mahela mwenyewe au anaambiwa na mhariri "fuatilia tukio fulani", na kisha yeye ndio huenda kuripoti?
 
Pamoja na huyo, mwanamama Hoyce Temu wa Channel Ten naye anajitahidi sana kuibua matatizo na kisaidia kuyapatiaufumbuzi ndani ya jamii...

Tafakari...

yap Hoyce Temu dah huyu dada aliibua hadi inshu za uchawi
 
Mapengo 17

Kuna cha uongo hapo? Mbona mimi vyote nimeona vya ukweli na mwandishi ametusaidia wengi ambao tuna mtazamo ka wake kuwa anastahili tuzo!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom